Tazama foleni hii ya wanunuzi wa sukari Morogoro. Juzi Waziri Bashungwa kapitishiwa bajeti ya hovyo iliyoungwa mkono na wanaccm wote Bungeni

Kwa siku kadhaa kumekua na uadimikaji "feki" wa sukar hapa nchini,chanzo,au tatizo hili ni lack of leadership.nimesikitishwa sana na picha zinazosambaa mtandaon zikionesha wakaz wa manispaa ya morogoro wakipanga folen kwenye duka linalosadikiwa ni la mbunge wa morogoro mjin ili kujipatia bidhaa "adimu"ya sukari.kimsingi,na kimkakati nchi yetu haikupaswa kua na uhaba wa sukar,wala kuagiza sukar toka ng'ambo...mkoa wa morogoro pekee km viongoz wetu wangekua serious ungeweza kutosheleza mahtaj ya sukar kwa nchi yote hi(sizungumzii tpc,wala kagera sugar).

Kwanza ningependa ku-diklea intrest kwmba mm nna mashamba ya miwa ya sukar ktk bonde la kilombero.hd msimu wa mavuno wa mwaka2019-2020 unafungwa mnamo mwez February mwaka huu,kampuni ya sukar illovo group (makaburu)ilikua haijaweza kuvuna japo 50%ya miwa yote ya wakulima wa nje(outgrowers)tatizo likiwa ni udogo wa kiwanda kulingana na mashamba yaliyopo...imefikia hatua vyama vya msingi vya ushirika vya wakulima kuwazuia wakulima kuendelea kupanua mashamba yao kwa kigezo kwamba soko hakuna,(at the same time we have a shortage of sugar)ilhali serikali yetu imejinasibu kuinua/kuendeleza viwanda.

Kule kilombero wako wakulima wakubwa wenye uwezo wa kutengeneza sukar bila kusubir kiwanda/mwekezaj.ila tatizo lipo serikalin/sera zetu za kulinda wawekezaj.as we speak miwa ya wakulima imelala mashamban(mingine more than 2yrs)uwezo wa watu kutengeneza sukar upo,ila hatujui kaburu kaifanyaje serikali yetu... yaan kuhus uhaba wa sukar,na hali ilivyo ktk vijiji vya kolodeko,kidodi,ruhembe,ilundo,msindaz...

Mie roho inaniuma kwakweli.hapo sijazungumzia wakulima wa mtibwa,na mashamba mapya yaliyoko mbigili ambako uwekezaj wa kiwanda bdo ni kizungumkut,japo Kuna maelf ya ekar za miwa,na hakuna kiwanda,pia Kuna bagamoyo ambako mzee bakresa kawekeza maheka ya miwa ila uzalishaj wa sukar uko ktk hatua ya sintofaham.HONESTLY,IF KUNA MDAU YEYOTE MWENYE KIWANDA CHA SANITIZER HUM JF ANICHEK PM TUFANYE BIASHARA YA ETHARNOL ITOKAYO NA MIWA.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wachumi tumefeli wapi??
Mbona tunaelekea kubaya??
Control si iendane na upatikanaji??
Waruhusu wafanyi biashara walete sukari toka nje ya nchi, waache kutaifisha na kudhulumu na kufilisi watu!!
 
Sukari sukari sukari.... Nyumbani no sukari,
kwenye migahawa no sukari, kwa mama ntilie no sukari madukani no sukari.
Sukari mbona umekuwa hivi tena? Au unatumiwa na mabeberu? 😀😀
 
Mi nilikuwa najiuliza siku zote ni nini hasa tatizo mpk sukari iwe adimu? Kama viwanda vyetu vya ndani havikidhi mahitaji ya (wa)Tanzania, kwanini basi tusiagize kutoka nje? Lakini leo jibu mujarabu nimelipata na kuondokana na sintofahamu, ahsante sana mkuu ubarikiwe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
viwanda vilitakiwa vijengwe na serikali kwa kutumia taasisi kama nssf ppf lakini wanajenga majengo zaidi miaka 2 kuna mpangaji mmoja tu, 👇

1589173095761.png
 
Hii ni foleni ya wanaonunua sukari Morogoro mjini ndani ya duka la mbunge wao.

Kinachonikera zaidi juzi waziri wa viwanda na biashara kapitishiwa bajeti mbovu sana huku wabunge wa CCM pamoja na spika wakijikita kuishambulia Chadema.

Aidha hawa ni wanunuzi wa jumla. Unapata Corona na sukari halafu ukitoka hapo wanakuja watu wa serikali za mitaa wanataifisha.

Kishindo cha awamu ya tano kwelikweli!

ACHENI UZUSHI HII FOLENI NI YA NIDA USAJILI WA LAINI KIPINDI KILE

CCM DAMUDAMU!!!,CHAMA CHA MAMA &BABA
 
Watu mmekuwa wajing* sana. Kila kitu mnakipeleka kwenye mambo ya vyama. Mimi nakupa ushauri wa kitaalam kuwa sukari siyo nzuri kwa mwili. Wewe unaona mimi ni mwanachama wa chama fulani. Hii mentality ya kuona kila kitu kwa kupitia lenzi ya vyama ni ya hovyo sana. Tubadilike. Mimi wala sihusiki na nchi. Niko nje ya Tanzania.

Kama watu kwa ujumla wao wakielimika kuhusu madhara ya sukari na kuacha ama kupunguza matumizi ya sukari, mamalishe atataka sukari ya nini? Mbona unashindwa ku-reason vitu vidogo kama hivi? Waasia kama Wajapan na Wachina unywa chai bila sukari. Sasa mamalishe wa Japan atataka sukari ya nini?
Unamaanisha biashara zote za mama ntilie zifungwe ?

Acheni kutafuta cheap option kwenye suala la msingi kama hili.

Kama nchi imewashinda achieni watu wenye akili waje waongoze.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mambo yamekorogeka, mjini wavijana wa UVCCMwanaolipwa Posho kwa Siku , yaani buku saba kupitia kwa kijana wao Peter Msacky ambaye pia ni mtumishi wa NMB Mtongani wamepanga kufanya maaandamano dhidi ya Waziri wa Viwanda na biashara pamoja na Waziri wa kilimo ili waondoshwe .

Miaka 4 iliyopita hawa MATAGA .

Mwezi Machi, tulipiga marufuku uingizaji Wa Sukari kutoka nje ya nchi ili kulinda viwanda vyetu
WATU: weweeeeeeee safi sana, hongera jembe letu, Wewe ndie tuliekuwa tunakuhitaji, Mungu akulinde.

BAADA YA MWEZI MMOJA.
Tumeagiza Sukari tani 70,000 kutoka nje ya nchi na kati ya hiyo tani 11,000 zimeshawasili.
WATU; weweeeeeeeee, hongera sana umetuokoa Jembe letu, Wewe Ni Wewe hakuna mwingine kama Wewe. piga pushapu hapo tione kama Lowassa atalipa, mgonjwa tu yule

BODI YA SUKARI: -imejaa makada wa chama, haina wataaluma, ipo kisiasa na ili upewe kandaraasi ya kuagiza sukari nje lasma uwe mchanhaji wa chama na wana bodi huchukua hivyo vibali na kuviuza kwa wa-Tanzania wenye asili ya asia

Ewe Mtanzania nani amekuloga?
 
Nyama,chumvi,mafuta na wanga sio vizuri pia mimi nakupa ushauri wa kitaalam ule majani na matunda kama ngedere mwituni.
Watu mmekuwa wajing* sana. Kila kitu mnakipeleka kwenye mambo ya vyama. Mimi nakupa ushauri wa kitaalam kuwa sukari siyo nzuri kwa mwili. Wewe unaona mimi ni mwanachama wa chama fulani. Hii mentality ya kuona kila kitu kwa kupitia lenzi ya vyama ni ya hovyo sana. Tubadilike. Mimi wala sihusiki na nchi. Niko nje ya Tanzania.

Kama watu kwa ujumla wao wakielimika kuhusu madhara ya sukari na kuacha ama kupunguza matumizi ya sukari, mamalishe atataka sukari ya nini? Mbona unashindwa ku-reason vitu vidogo kama hivi? Waasia kama Wajapan na Wachina unywa chai bila sukari. Sasa mamalishe wa Japan atataka sukari ya nini?
 
Back
Top Bottom