Tawi la CHADEMA nje ya nchi

RayB

JF-Expert Member
Nov 27, 2009
2,752
196
Wakuu,

Kwa wale ambao wanaishi nje ya nchi watakubaliana nami kuwa kumekuwa na utitiri wa matawi ya CCM ambayo mengine si matawi bali ni vijikundi. Tena matawi haya yamekuwa na access kubwa sana na balozi zetu as if Ubalozi ni wa CCM.

Ningependa mwongozo kutoka kwa viongozi wa chadema ni jinsi gani ya kuanzisha tawi na natakiwa kufata mlolongo gani? Ningependa sana niwe pioneer katika hii movement. Manake imekuwa sasa kama unataka mambo yako yashine basi uwe na link ya CCM na wakati mwengine CCM inakuwa na influence kubwa hata kwenye vyama vya kitanzania katika nchi hizi.

Wahusika wakiniPM na kunipa maelekezo itakuwa safi sana.


Nawasilisha kwani naamini members wako wengi sana
 
Best wazo zuri sna hata mie nataka uanachama hehe hehe ikiwezekana uweka hazina kabisaa:teeth::teeth::teeth:
 
Wahusika wakiniPM na kunipa maelekezo itakuwa safi sana.
wahusika wanye mamlaka ya kusajili tawi la CHADEMA wanatumia njia rasmi za mawasiliano, tafuta anwani zao kwenye tovuti yao, kama uko serious, badala ya kubandika post JF eti CHADEMA wawasiliane nawe humu kuhusu kuanzisha tawi, ridiculous
 
wahusika wanye mamlaka ya kusajili tawi la CHADEMA wanatumia njia rasmi za mawasiliano, tafuta anwani zao kwenye tovuti yao, kama uko serious, badala ya kubandika post JF eti CHADEMA wawasiliane nawe humu kuhusu kuanzisha tawi, ridiculous

Thanks, but yeah I mean it na JF ni public forum wakiona watanijibu. I do not see a problem on that.

NB: What if I do not have the contacts you think I have?
 
Best wazo zuri sna hata mie nataka uanachama hehe hehe ikiwezekana uweka hazina kabisaa:teeth::teeth::teeth:
I second you.Wazo zuri na nina uhakika as far as ughaibuni is concerned Upinzani wana wanachama wengi kuliko hao sis emu ila tu hawako kimaslahi zaidi kama hawa wenzetu.
 
Best wazo zuri sna hata mie nataka uanachama hehe hehe ikiwezekana uweka hazina kabisaa:teeth::teeth::teeth:

Mh wewe ndo ulikokimbilia huko, chama kinaanza na mchango wako upo tayari? Then utaanza kuitunza hazina utakayoitoa wewe
 
msithubutu kufanya hii...CHADEMA yetu haihusiki na mambo ya nje.....HATA AMBAYE ANGEKUWA RAIS WETU ALIKWISHA PIGA MARUFUKU HII.....KUWA ASINGESAFIRI KUJA HUKO MLIKO LABDA NYIE NDO MJE HUKU NDANI......and off-course TUNGEKULA KASAVA KWA KWENDA MBELE
 
msithubutu kufanya hii...CHADEMA yetu haihusiki na mambo ya nje.....HATA AMBAYE ANGEKUWA RAIS WETU ALIKWISHA PIGA MARUFUKU HII.....KUWA ASINGESAFIRI KUJA HUKO MLIKO LABDA NYIE NDO MJE HUKU NDANI......and off-course TUNGEKULA KASAVA KWA KWENDA MBELE

Hapo kwenye Cassava nakuunga mkono
 
DINGSWAYO......! naomba nikukumbushe kitu kimoja kuhusu mimi.....I AM FLEXIBLE.....I AM TANZANIAN....(mimi si CHADEMA,CCM,CUF,UDP,TLP,DP,NCCR-MAGEUZI,SAU,UMD,APPT-MAENDELEO,JAHAZI WALA MTUMBWIjoke) MIMI NAJITAHIDI KUWEKA MASLAHI YA TAIFA/NCHI MBELE kulio vitu viwezavyo kutugawa(DR.XAVIER LWETAMA) KAMAHUYU BWANA KWENYE MABANO.....inapokuja hoja ya msingi ambayo inajenga mimi nipo humo(CCM,CUF,TLP,CHADEMA,SAU,DP etc)....IKIWA HOJA YA MASLAHI YA CHAMA HUSIKA TU MIMI SIMO HUMO......!
KAMA SIJAJIELEZEA VYA KUTOSHA NAOMBA HOJA
 
msithubutu kufanya hii...CHADEMA yetu haihusiki na mambo ya nje.....HATA AMBAYE ANGEKUWA RAIS WETU ALIKWISHA PIGA MARUFUKU HII.....KUWA ASINGESAFIRI KUJA HUKO MLIKO LABDA NYIE NDO MJE HUKU NDANI......and off-course TUNGEKULA KASAVA KWA KWENDA MBELE
Acha hizo wewe endelea kunywa rangi ya kijani.Au umekunywa mwarubaini ghafla ukawa CHADEMA?
 
Hili wazo limesimama
Tuwe kama wenzetu waliostaaribika na siasa duniani, tuanzisheni na sisi na tuwasihi balozi zetu ziwe na ustaarabu na uungwana wa kuwahudumia watz bila kujali itikadi zao maana Tz si ccm bali watanzania wa vyama vyote

Bila kusahau uanzishwaji wenye kujali sheria vilivyo:A S crown-1:
 
Ahsante muungwana niwazo zuri lakini kwa mtizamo wangu CHADEMA wasifuate makosa ya CCM.Kama ni mtawi ambayo watu wanaweza kukutana na kujadiri mambo mbalimba ambayo yanamuafaka katika ujenzi wa nchi yetu it is ok kama matawi yatakayokutana na kujadiri jinsi gani ya kukisaidia chama it is ok.TUSIFUATE MKUMBO WA MATAWI YA CCM YANAYOZUKA KAMA UYOGA KWANI HAYA YA CCM NI MRADI WA WAJANJA WACHACHE AMBAO WANATUMIA FEDHA ZA WALALA HOI KUDHAMINI MATAWI HAYO CHINI YA KIVULI CHA TAWI LA CCM.Inakua vigumu kuelewa ofisi za ubalozini ughahibuni[ zinapokua sehemu ya CCM.Mfano katika tangazo lao Tawi linalohitwa la CCM Moscow lilipo andaa sherehe ya kumpongeza JK katika jengo la ubalozi nani aliipia gharama za sherehe hiyo!???Of course UBALOZI vinginenyo wangekodi ukumbi.Je CHADEMA au CUF n.k wakitaka kuandaa sherehe hiyo wataruhusiwa?Nimehudhuria kwa hizo zinazohitwa sherehe HAKUNA ZAIDA YA MNUSO Nawakati mwingine hata hao wanaohitwa wakereketwa wa CCM ukiwauliza hawawajui hata wabunge wa majimbo yao.WATANZANIA UGHAIBUNI TUNAPASHWA KUUNGANA KAMA WATANZANIA CCM INAPITA NA CHADEMA INAKUJA NA ITAPITA LAKINI WATANZANIA TUNABAKI KUA WATANZANIA.HAYO MATAWI YA CCM UGHAIBUNI NI MIRADI YA WATU (UFISADI),UNAFIKI,KUJIPENDEKEZA...........MUNGU IBARIKI TANZANIAQUOTE=RayB;1313024]Wakuu,

Kwa wale ambao wanaishi nje ya nchi watakubaliana nami kuwa kumekuwa na utitiri wa matawi ya CCM ambayo mengine si matawi bali ni vijikundi. Tena matawi haya yamekuwa na access kubwa sana na balozi zetu as if Ubalozi ni wa CCM.

Ningependa mwongozo kutoka kwa viongozi wa chadema ni jinsi gani ya kuanzisha tawi na natakiwa kufata mlolongo gani? Ningependa sana niwe pioneer katika hii movement. Manake imekuwa sasa kama unataka mambo yako yashine basi uwe na link ya CCM na wakati mwengine CCM inakuwa na influence kubwa hata kwenye vyama vya kitanzania katika nchi hizi.

Wahusika wakiniPM na kunipa maelekezo itakuwa safi sana.


Nawasilisha kwani naamini members wako wengi sana[/QUOTE]
 
msithubutu kufanya hii...CHADEMA yetu haihusiki na mambo ya nje.....HATA AMBAYE ANGEKUWA RAIS WETU ALIKWISHA PIGA MARUFUKU HII.....KUWA ASINGESAFIRI KUJA HUKO MLIKO LABDA NYIE NDO MJE HUKU NDANI......and off-course TUNGEKULA KASAVA KWA KWENDA MBELE

Do not spoil it cos we know you are not among of us
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom