Tawala za kifalme zilikuwa bora kuliko za kidemokrasia

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Jan 31, 2021
7,198
12,691
Kwenye utawala wa kifalme, nchi na serikali ilikuwa ni mali ya mfalme. Tofauti na kwenye demokrasia ambapo nchi na serikali ni mali ya wananchi wote, wakimuweka Rais kuwa mdhamini.

Binadamu ni social animal, na kwenye social animals wote kuna pecking order. Zamani waliokuwa wanakuwa wafalme ni wale waliokuwa wababe, kama tu kwenye maisha ya simba, mbwa mwitu nk. Hii ndiyo asili ya social animals wote.

Sasa kwenye ufalme, huyu mbabe na familia yake wanakuwa wanamiliki nchi nzima. Siku zote akili yao ipo macho kuhakikisha mali yao inastawi. Wakikopa ni wao watalipa. Wakipigana vita ni wao watagharamia. Walihakikisha wanatunza vizuri nchi hizo sababu zilikuwa ni urithi wa watoto na wajukuu wao. Mfalme alikuwa na uchungu na mali yake.

Sasa kwenye demokrasia nchi ni mali ya watu wote. Rais ni msimamizi tu. Rais hana uchungu wowote na nchi, yeye ni muangalizi tu, siyo mali yake. Na kwa kuwa msimamizi kuna faida binafsi anapata, hivyo basi, akili ya rais siku zote ni kuhakikisha anaendelea kuwa msimamizi wa mali ya wananchi, hata kama kufanya hivyo ana hatarisha ustawi wa hiyo mali. Kama kutapanya mali kutamfanya aendelee kuwa mdhamini wa mali hiyo atafanya hivyo.

Hivyo basi, binadamu kutoka kwenye mfumo wa kifalme kwenda kwenye mfumo wa kidemokrasia alijirudisha nyuma hatua nyingi sana. Mfumo wa kifalme ni bora kuliko mfumo wa kidemokrasia. Lakini sisemi kwamba mfumo wa kifalme ndiyo bora kabisa kwa binadamu. Binadamu bado hajapata mfumo bora wa kumuongoza.
 
Hakuna kitu kama hicho. Serikali za kifalme na za kidemokrasia hazina tofauti. Tofauti yake ni kuwa za kidemokrasia zinatawalika kwa akili na za kifalme zinatawalika kiimani.

Mfano ni kwamba Enzi za Falme za Kinyankole, Ukabaila mali zilikuwa ni za mfalme na milki yote ya rasilimali ni zake. Raia walitakiwa kuzalisha mali na kuchukua sehemu ya mali kumkabidhi mfalme wazitumie kwa manufaa yao kama chakula na mambo mengine.

Tuje sasa hizi za kidenokrasia mfano Tanzania Jeshi, mahakama, TRA, Fedha na Mabenk yoote ni mali ya Rais na akiamua anatumia anavyotaka bila kuhojiwa na mtu yeyote na ukisema 'Suu' unaondoka au kupotezwa.

Haijaishia hapo tu Wananchi woote wanatakiwa kutoa malia zao( kodi) kwa ajili ya matumizi ya Rais na baraza lake la mawaziri na kundi lake pendwa sana.

Kuna tofauti gani hapo?
 
Hakuna kitu kama hicho. Serikali za kifalme na za kidemokrasia hazina tofauti. Tofauti yake ni kuwa za kidemokrasia zinatawalika kwa akili na za kifalme zinatawalika kiimani...
Umedadavua vyema. Hakuna tofauti sana ila kuna kilicho bora. Ubora wa serikali ya kifalme ni vile mfalme alikuwa anajirestrain. Anajua akifanya vibaya, watoto wake na wajukuu zake watarithi kitu cha hovyo. Anajua utajiri na umaskini wa nchi ni wake, Rais wa kidemokrasia hahusiki na umaskini wala madeni ya nchi, hahusiki yeye wala vizazi vyake.
 
Serikali za kifalme huabudu watu wachache (royal family)... Serikali za kidemokrasia hutengeneza mifumo imara, shirikishi, jumuishi kwa ajili ya maendeleo endelevu.
Kwenye demokrasia kunakuwa tu na illusion ya kutomuabudu mtu, shirikishi, imara, jumuishi na huo uongo wa maendeleo endelevu. Hakuna mfumo upo kinyume na maendeleo endelevu(sustainable development) kama demokrasia.
 
Umedadavua vyema. Hakuna tofauti sana ila kuna kilicho bora. Ubora wa serikali ya kifalme ni vile mfalme alikuwa anajirestrain. Anajua akifanya vibaya, watoto wake na wajukuu zake watarithi kitu cha hovyo. Anajua utajiri na umaskini wa nchi ni wake, Rais wa kidemokrasia hahusiki na umaskini wala madeni ya nchi, hahusiki yeye wala vizazi vyake.
Hahaa basi tuwe kama Putin na Saudia
 
Kwenye demokrasia kunakuwa tu na illusion ya kutomuabudu mtu, shirikishi, imara, jumuishi na huo uongo wa maendeleo endelevu. Hakuna mfumo upo kinyume na maendeleo endelevu(sustainable development) kama demokrasia.
Demokrasia hutoa fursa sawa kwa kila mtu ahusike kwenye maendeleo tofauti na ufalme.

Jifunze hata kwa Zumaridi... yaani yeye peke yake ndo alijua nini cha kufanya wapi, lini, kwanini, kwa nani, kivipi.

Mfumo wa kifalme unazorotesha uwezo wa binadamu wengine! Mwisho wanatengenezwa vilaza wengiii.

Hata kwako au kwenu mkiendekeza mfumo wa kifalme mwenye nguvu akitoweka mjiandae kupoteana!
If you know what I mean.
 
Bado zipo, unaweza kuhamia huko.
Lesotho kwa Mswati, Morocco, Jordan, Saudi Arabia, Thailand.
Kwenye utawala wa kifalme, nchi na serikali ilikuwa ni mali ya mfalme. Tofauti na kwenye demokrasia ambapo nchi na serikali ni mali ya wananchi wote, wakimuweka Rais kuwa mdhamini...
 
Hakujawahi kuwa na Demokrasia ya Kweli since begging of time....

Kitu kimoja kizuri kuhusu huu Usanii ni kuwaaminisha Wananchi kwamba wao ndio wanaongoza hivyo kuridhika..., ila in reality nothing further from the truth....

Its not Power to the People bali Power to the Selected Few.... since its inception...
 
Demokrasia ni nini?
Hakujawahi kuwa na Demokrasia ya Kweli since begging of time....

Kitu kimoja kizuri kuhusu huu Usanii ni kuwaaminisha Wananchi kwamba wao ndio wanaongoza hivyo kuridhika..., ila in reality nothing further from the truth....

Its not Power to the People bali Power to the Selected Few.... since its inception...
 
Hakuna kitu kama hicho. Serikali za kifalme na za kidemokrasia hazina tofauti. Tofauti yake ni kuwa za kidemokrasia zinatawalika kwa akili na za kifalme zinatawalika kiimani.

Mfano ni kwamba Enzi za Falme za Kinyankole, Ukabaila mali zilikuwa ni za mfalme na milki yote ya rasilimali ni zake. Raia walitakiwa kuzalisha mali na kuchukua sehemu ya mali kumkabidhi mfalme wazitumie kwa manufaa yao kama chakula na mambo mengine.

Tuje sasa hizi za kidenokrasia mfano Tanzania Jeshi, mahakama, TRA, Fedha na Mabenk yoote ni mali ya Rais na akiamua anatumia anavyotaka bila kuhojiwa na mtu yeyote na ukisema 'Suu' unaondoka au kupotezwa.

Haijaishia hapo tu Wananchi woote wanatakiwa kutoa malia zao( kodi) kwa ajili ya matumizi ya Rais na baraza lake la mawaziri na kundi lake pendwa sana.

Kuna tofauti gani hapo?
Saudi Arabia
 
Kwenye utawala wa kifalme, nchi na serikali ilikuwa ni mali ya mfalme. Tofauti na kwenye demokrasia ambapo nchi na serikali ni mali ya wananchi wote, wakimuweka Rais kuwa mdhamini.

Binadamu ni social animal, na kwenye social animals wote kuna pecking order. Zamani waliokuwa wanakuwa wafalme ni wale waliokuwa wababe, kama tu kwenye maisha ya simba, mbwa mwitu nk. Hii ndiyo asili ya social animals wote.

Sasa kwenye ufalme, huyu mbabe na familia yake wanakuwa wanamiliki nchi nzima. Siku zote akili yao ipo macho kuhakikisha mali yao inastawi. Wakikopa ni wao watalipa. Wakipigana vita ni wao watagharamia. Walihakikisha wanatunza vizuri nchi hizo sababu zilikuwa ni urithi wa watoto na wajukuu wao. Mfalme alikuwa na uchungu na mali yake.

Sasa kwenye demokrasia nchi ni mali ya watu wote. Rais ni msimamizi tu. Rais hana uchungu wowote na nchi, yeye ni muangalizi tu, siyo mali yake. Na kwa kuwa msimamizi kuna faida binafsi anapata, hivyo basi, akili ya rais siku zote ni kuhakikisha anaendelea kuwa msimamizi wa mali ya wananchi, hata kama kufanya hivyo ana hatarisha ustawi wa hiyo mali. Kama kutapanya mali kutamfanya aendelee kuwa mdhamini wa mali hiyo atafanya hivyo.

Hivyo basi, binadamu kutoka kwenye mfumo wa kifalme kwenda kwenye mfumo wa kidemokrasia alijirudisha nyuma hatua nyingi sana. Mfumo wa kifalme ni bora kuliko mfumo wa kidemokrasia. Lakini sisemi kwamba mfumo wa kifalme ndiyo bora kabisa kwa binadamu. Binadamu bado hajapata mfumo bora wa kumuongoza.
Kwani wewe ulizaliwa ili utawaliwe milele kama kama kondoo,mbuzi,kuku au bata?
 
Mfumo wa kifalme upo sana afrika ingawa hauhitaji ubabe ujanjajanja ndio unao takiwa, mifumo iliyopo ni bosheni eti mfalme akikosea asishitakiwe kwa kosa lolote ananunua maroli Anaua treni,mkuu wa mhimili mwingine anamkosoa anatukanwa na dunia yote.hadi anainua mikono.
 
Back
Top Bottom