Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 37,470
- 46,001
1. Equatorial Guinea
Rais wake Teodoro Obiang Nguema; yuko madarakani kwa miaka 41 sasa. Mbili ya tatu ya wananchi wake wanaishi katika umaskini uliotopea licha ya kuwa nchi namba 3 kwa uzalishaji wa mafuta kusini mwa jangwa la Sahara.
2. Cameroon
Rais Paul Biya; yuko madarakani kwa miaka 38 sasa. Cameroon bado ni maskini haswa ila huwa anashinda chaguzi zote!
Tangu uhuru wa nchi mwaka 1960 Cameroon imeongozwa na chama kimoja na Marais wawili tu.
3. Congo Brazzaville
Rais wao Denis Sassou yuko madarakani kwa miaka 36.Nchi ni maskini na yenye vita kila mara. Congo zote mbili ni kama zina hii laana au bahati mbaya.
4. Uganda jirani yetu
Yoweri Museveni yuko madarakani kwa miaka 34 sasa. Huwa anapenda kuliita taifa lake wajukuu zake! Alipohojiwa mara ya kwanza na BBC punde tu baada ya kuwa Rais kwamba tatizo kubwa la Africa hasa ni nini alisema ni viongozi wanaokaa madarakani muda mrefu!
5. Chad
Idriss Deby yuko madarakani kwa miaka 30. Dikteta kipenzi cha mabeberu wanoamini ni mshirika wao muhimu kupambana na magaidi Africa Magharibi
6. Eriteria
Isaias Afwerki yuko madarakani kwa miaka 27. Wananchi wanalikimbia taifa lake kwa maelfu.
7. Djibouti
Ismail Omar Guelleh anaitawala nchi hiyo kwa miaka 21 sasa. Alichofanikiwa zaidi ni kuigeuza nchi hiyo kuwa kituo pendwa cha kijeshi kwa mataifa makubwa ya nje na sehemu pendwa ya biashara ya ngono.
8. Rwanda
Paul Kagame; Anaitawala nchi hii jirani yetu kwa miaka 20 sasa. Ni bingwa wa propoganda haswa tofauti na madikteta wengine ambao hupenda kutumia nguvu tu.
Amefanikiwa kuimanisha sehemu kubwa ya dunia kwamba Rwanda imepiga maendeleo makubwa sana chini ya utawala wake.
9. Togo
Faure Gnassingbé Eyadéma; Anatawala nchi hiyo kwa miaka 16 sasa akipokea utawala kutoka kwa baba yake Gnassingbé Eyadéma aliyeitawala nchi hiyo kwa miaka 38. Familia moja ya Eyadema inatawala nchi kwa miaka 54 mfululizo!
10. Gabon
Ali Bongo anaitawala nchi hiyo kwa miaka 12 sasa akipokea utawala kutoka kwa baba yake Omar Bongo aliyeitawala nchi hiyo kwa miaka 42. Familia moja ya Bongo imeitawala nchi kwa miaka 54 mfululizo au sawa na miaka mitano ya jiwe uzidishe mara 11!
Hawa wote wanaongoza Jamuhuri sio falme!
Rais wake Teodoro Obiang Nguema; yuko madarakani kwa miaka 41 sasa. Mbili ya tatu ya wananchi wake wanaishi katika umaskini uliotopea licha ya kuwa nchi namba 3 kwa uzalishaji wa mafuta kusini mwa jangwa la Sahara.
2. Cameroon
Rais Paul Biya; yuko madarakani kwa miaka 38 sasa. Cameroon bado ni maskini haswa ila huwa anashinda chaguzi zote!
Tangu uhuru wa nchi mwaka 1960 Cameroon imeongozwa na chama kimoja na Marais wawili tu.
3. Congo Brazzaville
Rais wao Denis Sassou yuko madarakani kwa miaka 36.Nchi ni maskini na yenye vita kila mara. Congo zote mbili ni kama zina hii laana au bahati mbaya.
4. Uganda jirani yetu
Yoweri Museveni yuko madarakani kwa miaka 34 sasa. Huwa anapenda kuliita taifa lake wajukuu zake! Alipohojiwa mara ya kwanza na BBC punde tu baada ya kuwa Rais kwamba tatizo kubwa la Africa hasa ni nini alisema ni viongozi wanaokaa madarakani muda mrefu!
5. Chad
Idriss Deby yuko madarakani kwa miaka 30. Dikteta kipenzi cha mabeberu wanoamini ni mshirika wao muhimu kupambana na magaidi Africa Magharibi
6. Eriteria
Isaias Afwerki yuko madarakani kwa miaka 27. Wananchi wanalikimbia taifa lake kwa maelfu.
7. Djibouti
Ismail Omar Guelleh anaitawala nchi hiyo kwa miaka 21 sasa. Alichofanikiwa zaidi ni kuigeuza nchi hiyo kuwa kituo pendwa cha kijeshi kwa mataifa makubwa ya nje na sehemu pendwa ya biashara ya ngono.
8. Rwanda
Paul Kagame; Anaitawala nchi hii jirani yetu kwa miaka 20 sasa. Ni bingwa wa propoganda haswa tofauti na madikteta wengine ambao hupenda kutumia nguvu tu.
Amefanikiwa kuimanisha sehemu kubwa ya dunia kwamba Rwanda imepiga maendeleo makubwa sana chini ya utawala wake.
9. Togo
Faure Gnassingbé Eyadéma; Anatawala nchi hiyo kwa miaka 16 sasa akipokea utawala kutoka kwa baba yake Gnassingbé Eyadéma aliyeitawala nchi hiyo kwa miaka 38. Familia moja ya Eyadema inatawala nchi kwa miaka 54 mfululizo!
10. Gabon
Ali Bongo anaitawala nchi hiyo kwa miaka 12 sasa akipokea utawala kutoka kwa baba yake Omar Bongo aliyeitawala nchi hiyo kwa miaka 42. Familia moja ya Bongo imeitawala nchi kwa miaka 54 mfululizo au sawa na miaka mitano ya jiwe uzidishe mara 11!
Hawa wote wanaongoza Jamuhuri sio falme!