Tatizo tuliruhusu Elimu kuwa Biashara, hilo ni kosa kubwa sana!

Barbarosa

JF-Expert Member
Apr 16, 2015
22,584
27,784
Malalamiko mengi yanayojitokeza sasa hv kwenye sekta ya Elimu hasa kwenye hizi Shule binafsi ni ya kujitakia, kwa sababu tulifanya kosa kubwa sana kuruhusu Elimu kuwa Biashara, yaani mtu anafungua Shule kama kitega Uchumi kama vile anajenga hoteli ambayo anategemea imrudishie fedha zake pmj na kumpatia faida, sasa hilo ni kosa kubwa sana na halisameheki hata kwa Mungu, kwani Elimu ni haki ya binadamu, ni huduma kwa jamii na inapaswa kubakia hivyo!

Matokeo yake ndo hayo unaona kama vile zilivyo Biashara nyingine, wenye Shule wanaweka Mihula mitatu badala ya 2 ili wavune fedha zaidi, wazazi kubebeshwa gharama nyingi za nyongeza hata zisizo za lazima ili Wafanyabiashara wapate faida n.k lkn cha ajabu wakati huo huo wenye Shule hawataki kulipa kodi, sasa kwa nini wkt ni biashara kama nyingine tu?

Mlm.Nyerere hatukumuelewa kwenye mambo mengi sana na ndio maana tumevuruga kila kitu, Dunia nzima Elimu ni huduma kwa jamii na siyo Biashara ya kupata faida!
 
HAPANA.

Huduma zote ni budi zitolewe kwa namna iliyo endelevu. Mojawapo ya njia za kuhakikisha uendelevu ni kufanya vitu kibiashara - ikiwepo na dhana nzima ya uwepo wa faida. Hii siyo dhana ngeni na hata inatumika katika mahospitali, menejment ya ardhi na huduma nyingi zingine.

Angalia hata wenzetu walioendelea unakuta majiji yanaendeshwa kibiashara. Badala ya ukurugeni wa jiji unakutana na corporation, eg City of London Corporation, Halmashauri zinabaki kuwa kama Board of directors.

Angalia hata vilabu vikubwa vya michezo. Zote ni biashara. Pale uapoendesha hizi shughuli ki local zaidi ndiyo unazalisha ubabaishaji.
 
Malalamiko mengi yanayojitokeza sasa hv kwenye sekta ya Elimu hasa kwenye hizi Shule binafsi ni ya kujitakia, kwa sababu tulifanya kosa kubwa sana kuruhusu Elimu kuwa Biashara, yaani mtu anafungua Shule kama kitega Uchumi kama vile anajenga hoteli ambayo anategemea imrudishie fedha zake pmj na kumpatia faida, sasa hilo ni kosa kubwa sana na halisameheki hata kwa Mungu, kwani Elimu ni haki ya binadamu, ni huduma kwa jamii na inapaswa kubakia hivyo!

Matokeo yake ndo hayo unaona kama vile zilivyo Biashara nyingine, wenye Shule wanaweka Mihula mitatu badala ya 2 ili wavune fedha zaidi, wazazi kubebeshwa gharama nyingi za nyongeza hata zisizo za lazima ili Wafanyabiashara wapate faida n.k lkn cha ajabu wakati huo huo wenye Shule hawataki kulipa kodi, sasa kwa nini wkt ni biashara kama nyingine tu?

Mlm.Nyerere hatukumuelewa kwenye mambo mengi sana na ndio maana tumevuruga kila kitu, Dunia nzima Elimu ni huduma kwa jamii na siyo Biashara ya kupata faida!
Kuua elimu ni usaliti usiosameheka mbinguni wala duniani
 
Sasa ni nini kimebadilika?

mbona ada zimepanda tena kwa sana tu....

tatizo lenu mafisi, mnaongeaongea tuuu...mnatisha watu majukwaani....mkiwahadaa maskini afu mambo yanabaki vile vile tu....

hiyo elimu unayosema iligeuzwa biashara...mbona bado iko hivo...? ..


kuwaamini ninyi mafisi...inahitaji uwe mpuuzi na ufikirie kwa makalio kama ninyi...
 
HAPANA.

Huduma zote ni budi zitolewe kwa namna iliyo endelevu. Mojawapo ya njia za kuhakikisha uendelevu ni kufanya vitu kibiashara - ikiwepo na dhana nzima ya uwepo wa faida. Hii siyo dhana ngeni na hata inatumika katika mahospitali, menejment ya ardhi na huduma nyingi zingine.

Angalia hata wenzetu walioendelea unakuta majiji yanaendeshwa kibiashara. Badala ya ukurugeni wa jiji unakutana na corporation, eg City of London Corporation, Halmashauri zinabaki kuwa kama Board of directors.

Angalia hata vilabu vikubwa vya michezo. Zote ni biashara. Pale uapoendesha hizi shughuli ki local zaidi ndiyo unazalisha ubabaishaji.


Hapa naongelea Elimu, tena ya Msingi na Sekondari hakuna nchi iliyoendela ambayo Elimu ni Biashara kama hapa kwetu, na sababu ni kwamba Elimu ni Huduma kwa jamii!
 
Malalamiko mengi yanayojitokeza sasa hv kwenye sekta ya Elimu hasa kwenye hizi Shule binafsi ni ya kujitakia, kwa sababu tulifanya kosa kubwa sana kuruhusu Elimu kuwa Biashara, yaani mtu anafungua Shule kama kitega Uchumi kama vile anajenga hoteli ambayo anategemea imrudishie fedha zake pmj na kumpatia faida, sasa hilo ni kosa kubwa sana na halisameheki hata kwa Mungu, kwani Elimu ni haki ya binadamu, ni huduma kwa jamii na inapaswa kubakia hivyo!

Matokeo yake ndo hayo unaona kama vile zilivyo Biashara nyingine, wenye Shule wanaweka Mihula mitatu badala ya 2 ili wavune fedha zaidi, wazazi kubebeshwa gharama nyingi za nyongeza hata zisizo za lazima ili Wafanyabiashara wapate faida n.k lkn cha ajabu wakati huo huo wenye Shule hawataki kulipa kodi, sasa kwa nini wkt ni biashara kama nyingine tu?

Mlm.Nyerere hatukumuelewa kwenye mambo mengi sana na ndio maana tumevuruga kila kitu, Dunia nzima Elimu ni huduma kwa jamii na siyo Biashara ya kupata faida!
Leo umeachana na ukada, umeleta hoja yenye mashiko. kula like.
 
Sasa ni nini kimebadilika?

mbona ada zimepanda tena kwa sana tu....

tatizo lenu mafisi, mnaongeaongea tuuu...mnatisha watu majukwaani....mkiwahadaa maskini afu mambo yanabaki vile vile tu....

hiyo elimu unayosema iligeuzwa biashara...mbona bado iko hivo...? ..


kuwaamini ninyi mafisi...inahitaji uwe mpuuzi na ufikirie kwa makalio kama ninyi...


Uko nje ya Mada, umechanganyikiwa kwa kuwa umejawa na chuki binafsi mpaka hata unashindwa kuelewa kinachoongelewa, nakushauri unywe maji na kuvuta pumzi ndefu halafu urudi labda kutakuwa na mabadiliko!
 
Ni sera za ccm na serikali zake ndizo zimetufikisha hapo. Watalamu wengi walishauri lkn wabunge wao kila jambo lilikuwa ndiooo 100%.
Hao CCM si ni ndugu zenu, wajomba zenu, shangazi zenu, binamu zenu, babu na bibi zenu, wengine ni baba na mama zenu au hata kaka na dada zenu. Sio kwamba wameshushwa kutoka Mars, mko nao kila siku na hamkuweza kuwashauri nani mnategemea afanye hilo, ifike mahali tuache kulalamikia kila kitu CCM maana hii ni taasisi na sio mtu, makosa yanafanywa na mtu na sio taasisi.
 
Elimu bado ni biashara ndio maana serikali haiziingiliii shule binafs ili wapate mapato.
 
Ni sera za ccm na serikali zake ndizo zimetufikisha hapo. Watalamu wengi walishauri lkn wabunge wao kila jambo lilikuwa ndiooo 100%.
Hao CCM si ni ndugu zenu, wajomba zenu, shangazi zenu, binamu zenu, babu na bibi zenu, wengine ni baba na mama zenu au hata kaka na dada zenu. Sio kwamba wameshushwa kutoka Mars, mko nao kila siku na hamkuweza kuwashauri nani mnategemea afanye hilo, ifike mahali tuache kulalamikia kila kitu CCM maana hii ni taasisi na sio mtu, makosa yanafanywa na mtu na sio taasisi.
muelewe Batale alichokisema...hata wakishauriwa wanasikia basi? wakifika bungeni wao kila kitu ni ndiyooo....haya yote ni kwa sababu ya sera mbovu za chama chakavu,msikwepeshe maneno
 
Hapa naongelea Elimu, tena ya Msingi na Sekondari hakuna nchi iliyoendela ambayo Elimu ni Biashara kama hapa kwetu, na sababu ni kwamba Elimu ni Huduma kwa jamii!
Labda kuna kitu huelewi huwezi kuwa na huduma ya jamii nzuri endelevu kama huna pato endelevu uwe Msikiti kanisa au kituo cha kulea yatima. LAZIMA UENDESHE kibiashara ili upate pesa za kutoa huduma nzuri mfano unataka kutoa Elimu nzuri katika mazingira mazuri unajua wako wazazi wako tayari kusaidiana na wewe watoto wapate Elimu nzuri kwa kulipa gharama unawakubalia. TATIZO KUBWA TULILONALO HASA KWA VIONGOZI WA WIZARA YA ELIMU NI KUDHANI WADAU WA MAENDELEO WANAOTAKIWA KUCHANGIA ELIMU BORA NI WAHISANI WAZUNGU tu! WANASAHAU KUWA MZAZI WA MTOTO NI MDAU WA KWANZA. SHULE BINAFSI ZIMEGUNDUA HILO KUWA UKITAKA KUTOA ELIMU BORA MSHIRIKISHE MZAZI MWAMBIE GHARAMA HII HAPA YA KUMPA ELIMU BORA MWANAO ANALIPA.

TATIZO MAAFISA ELIMU HUJIFUNGIA NDANI NA KUTOA MIONGOZO WAKISHIRIKISHA WANASHIRIKISHA WAHISANI WAZUNGU WIZARA WANASAHAU KUSHIRIKISHA WAZAZI WA WATOTO HILO NI KOSA NA LILIANZA KIPINDI CHA NYERERE
 
..kuirudisha elimu kuwa huduma, tena yenye VIWANGO na UBORA kunahitaji umakini na utulivu.

..sasa nina mashaka sana kama uongozi wa awamu hii has what it takes to fix the mess that is in our education system.

..tatizo la elimu lilianza kwa kuingiza siasa ktk sekta ya elimu. Wataalamu walimuonya Baba wa Taifa kuhusu hatua alizotaka kuchukua, especially ktk kuongeza access on education kwa haraka huku akiwa hana uhakika na means za kudhibiti ubora na viwango. Tangu wakati huo elimu yetu ikaporomoka.

..Awamu zote zilizofuatia zimejaribu kurekebisha makosa lakini badala ya elimu kuboreka yameibuka matatizo mapya tena makubwa zaidi.

..Kwa muda mrefu tumejielekeza kwenye quantity na siyo quality. Kumekuwa na kampeni za kuandikisha wanafunzi wengi zaidi, kujenga madarasa mengi zaidi, kuchonga madawati mengi etc etc. Tumepuuza kabisa kuhakiki kama wanafunzi wetu wanajifunza na wanafikia viwango vya ufaulu ktk kila ngazi wanayopitia.

..ushauri wangu ni kwamba tujirudi na kuzingatia QUALITY ktk mfumo wetu wa elimu. Siku zote tujiulize kama wanafunzi wetu WAMEPIKWA KWELIKWELI.
 
HAPANA.

Huduma zote ni budi zitolewe kwa namna iliyo endelevu. Mojawapo ya njia za kuhakikisha uendelevu ni kufanya vitu kibiashara - ikiwepo na dhana nzima ya uwepo wa faida. Hii siyo dhana ngeni na hata inatumika katika mahospitali, menejment ya ardhi na huduma nyingi zingine.

Angalia hata wenzetu walioendelea unakuta majiji yanaendeshwa kibiashara. Badala ya ukurugeni wa jiji unakutana na corporation, eg City of London Corporation, Halmashauri zinabaki kuwa kama Board of directors.

Angalia hata vilabu vikubwa vya michezo. Zote ni biashara. Pale uapoendesha hizi shughuli ki local zaidi ndiyo unazalisha ubabaishaji.
Unachanganya mada we! Unazungumzia elimu au huduma gani tena huko London?
Mada inasema elimu. Ningetegemea utoe mifano ya elimu kwa hao unaowaita wenzetu, ambako elimu ni biashara.

Mada iko safi na kama unataka iwe biashara, lipa kodi, toa risiti ya EFD! Lini ktk nchi hii elimu ikalipiwa kodi?
 
HAPANA.

Huduma zote ni budi zitolewe kwa namna iliyo endelevu. Mojawapo ya njia za kuhakikisha uendelevu ni kufanya vitu kibiashara - ikiwepo na dhana nzima ya uwepo wa faida. Hii siyo dhana ngeni na hata inatumika katika mahospitali, menejment ya ardhi na huduma nyingi zingine.

Angalia hata wenzetu walioendelea unakuta majiji yanaendeshwa kibiashara. Badala ya ukurugeni wa jiji unakutana na corporation, eg City of London Corporation, Halmashauri zinabaki kuwa kama Board of directors.

Angalia hata vilabu vikubwa vya michezo. Zote ni biashara. Pale uapoendesha hizi shughuli ki local zaidi ndiyo unazalisha ubabaishaji.
Basi wakaguliwe na TRA na walipe kodi...
Siyo kujificha kwenye mgogo wa 'tunaisaidia serikali' kumbe watu wanapiga ma bilioni kwa mwaka
 
..kuirudisha elimu kuwa huduma, tena yenye VIWANGO na UBORA kunahitaji umakini na utulivu.

..sasa nina mashaka sana kama uongozi wa awamu hii has what it takes to fix the mess that is in our education system.

..tatizo la elimu lilianza kwa kuingiza siasa ktk sekta ya elimu. Wataalamu walimuonya Baba wa Taifa kuhusu hatua alizotaka kuchukua, especially ktk kuongeza access on education kwa haraka huku akiwa hana uhakika na means za kudhibiti ubora na viwango. Tangu wakati huo elimu yetu ikaporomoka.

..Awamu zote zilizofuatia zimejaribu kurekebisha makosa lakini badala ya elimu kuboreka yameibuka matatizo mapya tena makubwa zaidi.

..Kwa muda mrefu tumejielekeza kwenye quantity na siyo quality. Kumekuwa na kampeni za kuandikisha wanafunzi wengi zaidi, kujenga madarasa mengi zaidi, kuchonga madawati mengi etc etc. Tumepuuza kabisa kuhakiki kama wanafunzi wetu wanajifunza na wanafikia viwango vya ufaulu ktk kila ngazi wanayopitia.

..ushauri wangu ni kwamba tujirudi na kuzingatia QUALITY ktk mfumo wetu wa elimu. Siku zote tujiulize kama wanafunzi wetu WAMEPIKWA KWELIKWELI.
Ni ishara gani inayoonyesha kwamba ubora wa elimu umeharibika? Nimekuwa Kenya kwa wenye 'swaga' wako hoi na sasa wamempata Dr Matiang'i wananyoosha mikono mbinguni kwa hatua zake. Uganda hoi!

Bila kujali tamaa ya elimu yetu, bado tulistahili control. MBona bia ilipokosekana gongo haikuruhusiwa? Hata kama tulihitaji elimu bora, hiyo haikuwa sababu ya kuruhusu watu kujiingiza na kuanza kutafuta faida kubwaaa! Ukiuliza unaambiwa pesa ya matibabu, kompyuta, ziara za masomo, masomo ya ziada, nembo ya shule, uharibifu, basi la shule mengineyo.
what all these for? Mwenye shule akiona wazazi wana nyodo, anaongeza ziara za nje ya nchi, passport kwa form iv na vi, nk. nk. nyoooooro! elimu gani hiyo?
 
Back
Top Bottom