Tatizo siyo watu wanaoishi "mabondeni" bali ni wale wanaoishi "magogoni"

Sentensi hiyo yaweza kuwa kweli au si kweli; kama unafikiri ina ukweli jadili kwanini na kama unafikiri si ya kweli ina walakini tuelezee kwanini. Clue: watu wa "mabondeni" ni wale wote ambao ambao wamejikuta wakiathirika na mafuriko haya moja kwa moja na watu wa "magogoni" ni watawala wetu.

Nakubaliana na wewe Mwanakijiji, tatizo lipo kwa wapangaji wetu wa Magogoni. Ukitembelea nchi zilizoendelea utakuta viwanja kama vya watu wanaishi mabondeni ni bei ghali mno. Kwanza kipo karibu na mto, pili kuna kama mlima. Nchi zilizoendelea hizo sehemu ni bei ghali kama viwanja vilivyo karibu na Bahari.

Tatizo liliopo hapa kwetu ni kwamba serikali haijali wananchi, haitengenezi miundombinu ya kupitishia maji machafu na safi na mazingira mazuri ya kuwafanya watu wanoishi (mabondeni kama wanavyosema) kupata hizo huduma, ingawa kupata hizo huduma hapa Tanzania ni ndoto kama tukiendelea na wajinga hawa waliotufikisha hapa tulipo kwa upuuzi wa watu wachache, uvivu wao wa kufikiria umefika kikomo zaidi ya kukwapua kodi za Watanzania na kuzitumia kwa matumizi yao binafsi bila ya kuwajali walipa kodi wenyewe.

Hebu angalieni Nyumba zilizo sehemu kama hizo za Mabondeni na hakuna mafuriko, tusiwalaumu wakazi wa sehemu hizo wakati tatizo lipo kwa wapangaji wetu wa magogoni wliofikia kikomo cha kufikiria na Wavivu ndani ya vichwa vyao

South_Africa-Hartbeespoot_dam06.jpg


pecanwood_body7.jpg
 
Daima tumekuwa wa kulalamika badala ya kutimiza sheria za nchi.....kwanza naomba kutanguliza pole kwa wote waliokumbwa na janga hili kwani ndio kawaida ya ubinadamu.

Napenda kuweka wazi mtazamo wangu kuwa jamiiyetu kuwa waliojenga mabondeni ni wavunja sheria na ni sawa na mtu aliyefanya kosa lingine lolote . sasa kuna kundi la watu wamejenga mabondeni na kuvunja sheria bila ya kujua na wengine wamejua na kutenda wakiwa wanajua wazi wanachokifanya. kwa mujibu wa sheria za taifa letu ujenzi wowote lazima upewe kibali ya kujenga jengo hilo, hivyo basi yeyote aliyejenga bila kupewa kibali ni mvunja sheria.

lakini swali kubwa ni kujiuliza mamlaka zinazohusika na mipango miji zilikuwa wapi mpaka sheria za nchi zimevunjwa na kundi kubwa la watu mpaka kupelekea uvunjaji huu wa sheria kuwa haki zao za msingi? hivyo serikali haiwezi kukwepa ulegelege wake uliopelekea majanga haya na uvunjaji mkubwa wa sheria na hasara kubwa katika taifa letu..ni lazima timu kubwa sana inayohusika na mipango miji wafukuzwe kazi na kushitakiwa. lakini wananchi lazima tuanze kuheshimu sheria za mipango miji....na mbeleni tusijekutumia kigezo cha kutojua sheria za ujenzi na makazi eti ndio sababu ya sisi kuzivunja


 
Sentensi hiyo yaweza kuwa kweli au si kweli; kama unafikiri ina ukweli jadili kwanini na kama unafikiri si ya kweli ina walakini tuelezee kwanini. Clue: watu wa "mabondeni" ni wale wote ambao ambao wamejikuta wakiathirika na mafuriko haya moja kwa moja na watu wa "magogoni" ni watawala wetu.

Kwa kukusahihisha mkuu ni viongozi wetu na si watawala wetu kwani tuliishia kutawaliwa kabla ya uhuru
 
Tatzo ni la hawa waishio 'magogoni',kwasababu:-

1. Wanadai watu wanakatazwa kujenga mabondeni,mbona wanawapelekea huduma muhimu kama vile umeme kama kweli watu hawatakiwi kujenga mabondeni wasingewapa huduma hizo muhimu kuonesha kuwa hawatakiwi kuishi kule..

2. Ukiona serikali imewafukuza watu mabondeni ujue wana maslahi na hicho kiwanja(kuna kigogo ana shida nacho/kuna mzungu kapewa kwa jina la uwekezaji)..

CONCLUSION:-
serikali legelege haiwezi ikafanya maamuzi sahii/yenye msimamo..

Umenena kitu sahihi na kitu ambacho kipo heko kwa hilo ur a great thinker
 
Tatizo liko kwa wote,tena hasa wa mabondeni maana at the end of the time wanaokufa ni wao.Watu wa mabondeni wanaelewa kabisa kuwa mvua zikija hapo hapakaliki but still wanaendelea kuishi mabondeni,to me nawaona kama wamekubali liwalo na liwe.MAGOGONI- hawa wana uwezo kabisa wa kuhamisha watu kutoka mambondeni ila wanashindwa kutoa order.Mafuriko yakija wao labda ni kutumia pesa ili kuwahifadhi waathirika.CONCLUSION:Watu wa mabondeni wana matatizo maana wao ndo wanaoathirika directly.Kwa hiyo wanatakiwa wahame haraka iwezekanavyo

Wewe ni zaidi ya Zuzu humu Jf na nilikuwa sijui kama humu Jf kuna watu kama wewe, kwakweli umeandika upupu na inakera kutokuwajali waTz wenzako kwani ulivyoandika utadhani ni mtu ambae hujawahi kuishi Tz hii. Unategemea wangekuwa wanauwezo wakupata kiwanja na kujenga shm nyingine unadhani wangeendelea kukaa wapoteze maisha na mali zao?
 
Watu wa magogoni ni janga la Taifa ambalo halijawahi kutokea Tz na haitatokea tena
 
Tatizo ni kukosekana kwa TOUGH LOVE!!

Pale magogoni, Hakuna hata mmoja mwenyewe UWEZO wa UJASIRI wa Kumchomoa Mgonjwa aliyepigwa Kisu kifuani kikatokea mgongoni! Kila ukimgusa .. mgonjwa anapiga mayowee ya maumivu makali!

Unatakiwa ujasiri uliojaa nguvu ya upendo (Tough Love)... Kumsaidia Mgonjwa kama huyo! Lazima kumpa masaada ambao unaweza kumsababishia maumivu makali yenye kumbatana na matusi na laana kem kem ... Lakini wewe ... Unajua unmsaadia!

Tatizo la Magogoni ... ITS WEAK CHARACTERS! no TOUGH LOVE!! ...

Huu ugonjwa utaliangamiza Taifa na unajionyesha kwenye kila nyanja ya jamii, kuanzia kuwatimua magamba, urafiki kazini, kuteua viongozi mbalimbali, kutowajibika na ulegelege wowote unaolikabili Taifa kwa sasa!

Na huu ugonjwa hauponwi India ... nani anjua DAWA yake???????
 
Hizo nyumba hazikubebwa zikaletwa hapo, zilianza msingi na serikali ipo/ilikuwepo na haikukataza... Tatizo lipo magogoni, wameshindwa kusimamia wananchi wao.

Tatizo ni la watu wa Magogoni kwa sababu zifuatazo:-
1. Wameshindwa kusimamia sheria za mipango miji mpaka wametufikisha hapa tulipo ambapo zaidi ya asilimia sabini ya makazi ya jiji hayajapimwa.
2. Wameshindwa kuweka miundombinu ya maji taka ambayo ingezuia mafuriko kwenye maeneo mengi ya jiji
3.Wameshindwa kuwahamisha wananchi waliojenga katika maeneo hatarishi na kuwapatia maeneo mbadala ya kuishi
Nawasilisha hoja.

Ni vigumu kuwalaumu watu waliojenga mabondeni. Nyumba haijengwi kwa siku moja, serikali ilikuwa wapi wakati wanajenga? Na huwezi kusema kuwa wamevunja sheria kwa kujenga mabondeni kwa sababu serikali ipo! Kama serikali inaweza kutabiri vurugu, na uwepo wa Al-shaabab wanashindwaji kusimamia ujenzi wa nyumba sehemu za mabondeni? Watu hawa wanapata huduma muhimu za jamii, i.e umeme, sasa leo wanawakana kwa vipi?

Magogoni kwa maana ya watawala ndo tatizo kubwa! kama eneo halistahili wanakuwa wapi watu wanajenga mpaka kuingiziwa huduma kama umeme ndani ya nyumba zao? serikali legelege ya kitu kidogo!

Kwa hiyo Magogoni, pamoja na mamlaka aliyokuwa nayo, watu wakikaidi amri halali hana uwezo wa kuwafanya chochote? usitake kuniambia kuwa hatuma mamlaka zenye nguvu za ku-enforce sheria na maagizo halali

Kuishi dalisalama raha!!

Nini maana ya Serikali au Watawala. Hawa wetu ni watawala wanaotumia utawala wa mapenzi. Kama nchi haina sheria, sheria ndogo basi waseme ili tuhamishie lawama kwa wanaojenga mabondeni kwa 100% la sivyo waliojenga mabondeni wanabeba 30% ya lawana na wa Magogoni 70.

Hii serikali bwana! Lipi wataliweza iwapo wameshindwa kuwaondoa ndugu zetu wanaoishi mabondeni na kuwatafutia sehemu zingine ambazo ni salama zaidi? Mimi naona hapa ni lack of seriousness. Serikali ikiwa serious watu wataondoka mabondeni. Najua kuwa watu watasema kuwa wananchi nao wanachangia. Hii si kweli serikali makini husimamia sera na sheria zake. Hapa Tanzania sheria hazifuatwi na hakuna anayezisimamia. Matokeo yake watu wataendelea kuteseka huku serikali ikisingizia kuwa watu watu hawataki kuhama mabondeni.

Watu wa magogoni ni janga la Taifa ambalo halijawahi kutokea Tz na haitatokea tena

Tatizo ni WEAK CHARACTER LEADERSHIP||| Kukosekana kwa Uongozi uliojaa UJASIRI wenye HAKI, UPENDO na DHAMIRA YA KWELI! The TOUGH LOVE!!!
 
Tatizo liko kwa wote,tena hasa wa mabondeni maana at the end of the time wanaokufa ni wao.Watu wa mabondeni wanaelewa kabisa kuwa mvua zikija hapo hapakaliki but still wanaendelea kuishi mabondeni,to me nawaona kama wamekubali liwalo na liwe.MAGOGONI- hawa wana uwezo kabisa wa kuhamisha watu kutoka mambondeni ila wanashindwa kutoa order.Mafuriko yakija wao labda ni kutumia pesa ili kuwahifadhi waathirika.CONCLUSION:Watu wa mabondeni wana matatizo maana wao ndo wanaoathirika directly.Kwa hiyo wanatakiwa wahame haraka iwezekanavyo

Waelewe wapi ndugu yangu;

1. Hawa ndio walalahoi ambao wengi shule hamna.
2. Hawa ndio wenye watoto wanaosoma shule za St. Kayumba, hivyo usitegemee watawashauri chochote wazazi wao.
3. Hawa ndio wenye mlo mmoja kwa siku na huduma mbovu za afya, hawawezi kufikiri sawasawa.
4. Hawa ndio ......................................................

Lawama ziwaendee magogoni walioshindwa:

1. Kusimamia sheria.
2. Kuelimisha watu wao.
3. Kuokoa watu wao.
 
Sentensi hiyo yaweza kuwa kweli au si kweli; kama unafikiri ina ukweli jadili kwanini na kama unafikiri si ya kweli ina walakini tuelezee kwanini. Clue: watu wa "mabondeni" ni wale wote ambao ambao wamejikuta wakiathirika na mafuriko haya moja kwa moja na watu wa "magogoni" ni watawala wetu.

Tatizo sio watu wanaoishi mabodeni, tatizo ni akili inayoishi bondeni, hiyo akili ikifahamu fika hapa bondeni mda wowote kitaeleweka. Lakini, hiyo akili inajaribu kujizingua na kujiridhisha kwamba nitaishi hapa, naamini ikitokea soo jirani atanisitua mapema na kusepa.
 
Wewe ni zaidi ya Zuzu humu Jf na nilikuwa sijui kama humu Jf kuna watu kama wewe, kwakweli umeandika upupu na inakera kutokuwajali waTz wenzako kwani ulivyoandika utadhani ni mtu ambae hujawahi kuishi Tz hii. Unategemea wangekuwa wanauwezo wakupata kiwanja na kujenga shm nyingine unadhani wangeendelea kukaa wapoteze maisha na mali zao?
Ukweli unauma!walishaambiwa wahame na wakawapropose maeneo,wao wakagoma wakasema mbali,tena mbunge wao aliwatetea pia.
 
hivi wandugu,hawa watu wanaojenga mabondeni halafu sisi tunaelekeza lawama kwa serikali ni tabia ya aina gani hii?mbona hatujawaona wakijikata na wembe si ina maana wana akili timamu? hebu tujiangalie tusijenge jamii ya walalamikaji zaidi badala ya kuwa na kizazi kipya kinachotoa suluhisho la matatizo yanayoikumba nchi yetu
 
Kiungo chochote cha mwili kinapopata damage yoyote, cha kwanza kujiuliza ni kua kichwa kilichukua nafasi gani katika hiyo damage!!
Naunga mkono hoja, magogoni ndio tatizo!!!!
 
Back
Top Bottom