Tatizo sio Uwingi wa Majukumu na Jina la “TFDA”: Urasimu, Tozo na Rushwa ni Hujuma kwa Uchumi

X-bar

JF-Expert Member
Mar 20, 2019
1,002
1,146
Watanzania,

Serikali imedhamiria kuipunguzia Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) majukumu ya udhibi wa vyakula na vipodozi na kuibadilisha jina kuwa Mamlaka ya Udhibiti wa Dawa na Vifaa Tiba (TMDA). Hatua hii ya Serikali ni kutokana na kufanyia kazi malalamiko ya wafanyabiashara juu ya utendaji wa mamlaka husika.

Hata hivyo, kwa maoni yangu sioni hatua hii ya serikali italeta tija na kuondoa malalamiko kwa biashara dawa na vifaa tiba. Ukiangalila juu juu unaweza kudhani watendaji wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) wako “serious” na wazalendo kweli kweli wa nchi yao katika udhibiti wa ubora wa bidhaa husika. Ukweli ni kwamba, sio kero kwa wafanyabiashara tu, watendaji wa mamlaka hii wanaihujumu serikali. Tatizo ni hujuma, urasimu na rushwa iliyokithiri kwa watumishi wa mamlaka hii. Leo nitaelezea urasimu, hujuma na rushwa zinazofanywa na watumishi wa mamlaka hii.

HUJUMA

Kwa mujibu wa kananuni na taratibu Za kufanya malipo kwa TFDA (Tanzania Food, Drugs and Cosmetics (Fees and Chargees) Regulations) inaelekeza hivi; nanukuu.

  • Fees and charges paid under these Regulations shall be paid in Tanzanian shillings or US$ equal to the amount of Tanzania shillings or any convertible shilling equal the amount payable in Tanzania Shillings
Maana yake ni kwamba shilingi ya Tanzania inatakiwa itumike kama kigezo (standard) kwa malipo yote, lakini pale inapobidi (mathalani kwa wateja walio nje ya Tanzania), wanaweza kufanya malipo kwa dolari ya Marekani au shilingi nyingine yoyote (ya Kenya au Uganda) kwa thamani ambayo ni sawa na kiwango kile kinachopaswa kulipwa kwa shilingi ya Tanzania.

Kinyume chake, viwango vya malipo vimekadiriwa kwa dolari ya Kimarekani peke yake. Maana yake ni kwamba viwango vya malipo kwa wateja walio ndani ya nchi (wanaotumia shilingi ya Tazania) hubadilika kila wakati kutegemea na thamani ya dolari ya Marekani dhidi ya shilingi ya Tanzania. Sasa kutokana na kubadilika mara kwa mara kwa shilingi ya Tanzania dhidi ya dolari, TFDA huweka kipindi cha wiki moja tu cha uhalali wa proforma invoice wanazotoa kwa waombaji wa vibali.

Kwa kufanya hivi TFDA sio tu wanakiuka utaratibu wa kisheria na sera za nchi, bali wanahujumu uchumi na kuwaumiza wateja wao wa ndani na kuwapa nafuu wale wa nje. Huu si uzalendo. Lakini, endapo shilingi yetu ingetumika kama kigezo, dola ndio ingekuwa inabadilika na kusingekuwa na haja ya kuweka kipindi maalumu cha uhalali wa invoice kwa wateja wa ndani.

URASIMU

Ingawa zaidi ya 80% ya maombi ya vibali vitolewavyo na mamlaka hii hufanyika kwa mfumo wa kielektroniki kwa ajili ya kurahisisha na kuharakisha michakato, matumizi ya mfumo huo haisaidii kwakuwa kuna urasimu wa kiwango cha juu. Kuna wakati mteja hulazimika kupiga simu au hata kufika kwenye ofisi za mamlaka ili kuwajulisha au kuwahimiza wafanyie kazi maombi yaliyotumwa kwa njia ya kielektroniki. Na maombi yanapopokewa, bado hayawezi kuidhinishwa mara moja; lazima watoe “query” na kila query itakayojibiwa lazima izae query nyingine na nyingine.

Query ni wito unaomtaka mteja kukamilisha matakwa Fulani, vielelezo au ufafanuzi kuhusu bidhaa inayoombewa kibali ambavyo bila kufanya hivyo mamlaka haitoi kibali kinachoombwa. Mathalani, unapotaka kuingiza bidhaa ambayo ni kifaa tiba utajaza fomu ya maombi na kuambatanisha nakala zote zinazohitajika ikiwa ni pamoja na risiti ya malipo, utapokea query inayosema “bidhaa hiyo haijasajiliwa na TFDA na kwahiyo hairusiwi kuingizwa nchini bila usajili”. Majibu ya query hii kwa mtuma maombi ni kusema “Bidhaa hii ni kwa ajili ya matumizi ya utafiti”. Mamlaka itakutumia tena query kukutaka uambatanishe “ethical clearance” ya kufanya utafiti. Wewe kama mfanyabiashara utajibu ethical clearance haikuhusu bali mteja wako aliyekutaka umsambazie ndiye anayehusika. Ukijibu hivyo TFDA watatoa query inayokutaka usajili hiyo bidhaa ndipo upate kibali cha kuingiza.

Ili muombaje asipoteze biashara itamlazimu kusajili. Sasa kwa bidhaa hiyo hiyo moja utalazimika kujaza fomu ya maombi ya usajili na mwishowe unapewa proforma invoice ya kulipia ambayo ina thamani ya $1500. Kumbuka usajili ni mchakato na unatakiwa utengeneze “dossier” na wakati Fulani uambatanishe na sampuli ya hiyo bidhaa. Sasa mbali na kulipia registration fee ya $1500, itakubidi pia uagize bidhaa andalau moja kwa ajili ya kuwasilishwa kwenye mamlaka kama sample.

Muombaji akiweza kutimiza hayo yote ni heri kwake; lakini je ataweza kupata usajili wa hiyo bidhaa ndani ya mweizi mmoja ili aweze kumsambazia mteja wake? Uzoefu unaona kuwa TFDA huwachukua miezi 6 hadi 10 kukamilisha usajili wa bidhaa. Vile vile ikumbukwe kuwa ukiweza kulipia ada ya usajili na wakifanyaa evaluation wa dossier uliyowasilisha, bado huwezi kupata kibali kwasababu utakapofuatilia utaulizwa (query nyingine), je ulilipia gharama kufanya GMP inspection? GMP ni good manucturing practice yaani ili bidhaa husika ipate kibali sharti kwanza kiwanda kinachozalisha hiyo bidhaa kikaguliwe na TFDA kuona kama mchakato wa uzalishaji unakidhi viwango vyake vya ubora. Gharama ya kufanya GMP inspection ni $6000 – 8000 kwakuwa kiwanda cha bidhaa husika kiko Ulaya au Markani. Kiwango hiki ni gharama ya kuwatuma wakaguzi kwenda nje ya nchi kufanya ukaguzi.

Kwa kweli huu ni urasimu usio wa lazima. Bali TFDA wanafanya kusudi kutoa invoice ya malipo ya usajili wa bidhaa bila kujumlisha na gharama ya ukaguzi wa GMP. Wanafanya hivyo ili kuficha gharama halisi ya kusajili bidhaa. Ukweli ni kwamba, kusajili kifaa tiba cha daraja C, mathalani kaseti za kipimo cha malari (Malaria RDT), gharama yake si $1500, bali ni $9500, sawa na shilingi 21,850,000. Sasa jiulize mfanyabiashara mmoja ana bdhaa ngapi za daraja C anazotakiwa za kulipia ilia pate idhini ya kuingiza na kuuza hapa nchini. Je, huku si kukomoana? Lakini je kwa gharama hizi ni mfanya biashara gani anaweza kusajili kila bidhaa anayoingiza nchini?



RUSHWA

Siku zote urasimu gharama kubwa za huduma huzaa rushwa. Hebu jaalia mfano hizo query hapo juu na wewe ni mfanyabiashara (muingizaji na msambazaji wa vifaa tiba, dawa na vitendanishi) umepata mkataba na mteja umsambazie bidhaa hizo kwa ajili ya matumizi ya utafiti wake unaotarijiwa kuanza ndani ya mwezi mmoja baada ya mkataba kutolewa. Je, huyo mteja bado atakuwa anasubiri tu muda wote wa miezi 6 hadi 10?

Kiufupi hakuna mtu anaweza kufuata mlolongo huu wote. Hakuna mfanyabiashara ambaye yuko tayari kupoteza mauzo kwa vikwazo hivi vya TFDA. Wahenga wanasema penye udhia penyeza rupia. Maana yake ni kwamba wafanyabishara wanalazimika kuwapa rushwa watendaji wa mamlaka ya TFDA ili wapate vibali kwa wepesi. Bali watumishi wa mamlaka hiyo wanajifanya wako serious kusimamia sheria kumbe wanafanya hivyo ili wapewe rushwa.

Wafanyabiashara wamejifunza kwamba ili mpokea maombi ya vibali huko TFDA asitoe query katika maombi ya vibali inatakiwa wapatiwe pesa. Makampuni makubwa yanapata vibali na wanaingiza vifaa tiba vipya vya kila aina bila usajiliwa. Ukiangalia kwenye mtandao wa mamlaka hiyo utaona orodha ya vifaa tiba na vitendajishi vilivyosajiliwa ni vichache kuliko vinavyoingizwa kutoka nje ya nchi kila siku.

MWISHO

Tatizo kubwa si uwepo wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) wala sio uwingi wa majukumu ya mamlaka hiyo. Kuipunguzia majukumu ya kudhibiti ubora na biashara ya vyakula na vipodozi na kuibadili jina kutoka TFDA na kuiita TMDA hakutasaidia kuondoa changamoto kwa wafanyabiashara zinazotokana na utendaji wa mamlaka hii. Kuna haja kwa serikali kuifumua na kuisuka upya Mamlaka hii ili iendane na mabadiliko kutoka TFDA na kuwa TMDA. Vile vile viwango vya tozo na ada viangaliwe upya kwani ni kubwa sana. Vinginevyo mabadiliko hayo haya hataleta tija kwa serikali na wafanyabiashara bali ni kuendeleza kuwanufaisha watendaji wa mamlaka.
 
Ngoja ni summarize na kuchangia moja kwa moja.
1. Serikali itoe maelekezo mahususi kwamba kodi fulani inalipwa kwa currency ipi na ikipendeza kodi zote zilipwe kwa fedha yetu wenyewe.

Sasa hili sio kwa mamlaka hii tuu, usumbufu huu uko kwenye makusanyo yanayosimamiwa na mamlaka karibia zote. Hivyo hii ni kero mtambuka sio mahususi kwa TFDA pekee.

Hapa wizara ya fedha inapaswa kutimiza wajibu wake

2. Pili, kuna kodi nyingi sana. Hata hili ni kama hapo mwanzo, serikali inapotengeza mamlaka hizi ijikumbushe kwamba lengo ni kuihudumia wananchi na itambue sio kila kitu lazima wananchi walipie hasa ukizingatia tayari wanalipa kodi nyingi zinazosimamiwa na mamlaka ya mapato.

Sekta ya afya inapaswa kuwa sekta ambayo inakatwa kiwango cha kodi cha chini zaidi sababu inahusika na uhai wa wananchi moja kwa moja.

Wakati serikali inaangaika kutoa bei helekezi kwenye mazao ya biashara naishauri itoe bei elekezi kwenye huduma na bidhaa za kiafya. Itoe bei elekezi kwenye vipimo vya maradhi, itoe bei elekezi kwenye bei za madawa.

Hivyo hata katika hili, nalo ni tatizo mtambuka.

3. Urasimu na Rushwa.
Rushwa ni ushenzi tu, na Urasimu ni ushenzi tu.

Urasimu umekuwa ni utaratibu mahususi wa kiutendaji kwa wafanyakazi duniani kote. Rushwa ni Mazalia ya Urasimu, hivyo tatizo la msingi hapa ni rushwa.

Kuna aina ya urasimu ambao ni sahihi, urasimu wa kisera, TFDA ni moja ya mamlaka ambayo binafsi nategemea uwepo urasimu wa kisera au wa kiutu.

Yaani hata mimi ningekuwa mtumishi wa TFDA kutokana na mahusiano mazuri tuliyonayo na wachina au wamarekani ningeweka urasimu wa kuua mtu pale ambapo mfanyabiashara anataka kuingiza dawa ambazo ninahisi zinamadhara ya kiafya kwa wananchi.

Hapa ndio narudi kwenye tatizo la rushwa. Tunaweza kaa hapa nakulaumu watumishi woooote wa UMMA mpaka mheshimiwa Rais lakini kuna kiwango cha pesa ukiwekewa mezani kama rushwa ukikikataa kila mtu anaweza kukuona wewe ni mjinga.
 
Ngoja ni summarize na kuchangia moja kwa moja.
1. Serikali itoe maelekezo mahususi kwamba kodi fulani inalipwa kwa currency ipi na ikipendeza kodi zote zilipwe kwa fedha yetu wenyewe.

Sasa hili sio kwa mamlaka hii tuu, usumbufu huu uko kwenye makusanyo yanayosimamiwa na mamlaka karibia zote. Hivyo hii ni kero mtambuka sio mahususi kwa TFDA pekee.

Hapa wizara ya fedha inapaswa kutimiza wajibu wake

2. Pili, kuna kodi nyingi sana. Hata hili ni kama hapo mwanzo, serikali inapotengeza mamlaka hizi ijikumbushe kwamba lengo ni kuihudumia wananchi na itambue sio kila kitu lazima wananchi walipie hasa ukizingatia tayari wanalipa kodi nyingi zinazosimamiwa na mamlaka ya mapato.

Sekta ya afya inapaswa kuwa sekta ambayo inakatwa kiwango cha kodi cha chini zaidi sababu inahusika na uhai wa wananchi moja kwa moja.

Wakati serikali inaangaika kutoa bei helekezi kwenye mazao ya biashara naishauri itoe bei elekezi kwenye huduma na bidhaa za kiafya. Itoe bei elekezi kwenye vipimo vya maradhi, itoe bei elekezi kwenye bei za madawa.

Hivyo hata katika hili, nalo ni tatizo mtambuka.

3. Urasimu na Rushwa.
Rushwa ni ushenzi tu, na Urasimu ni ushenzi tu.

Urasimu umekuwa ni utaratibu mahususi wa kiutendaji kwa wafanyakazi duniani kote. Rushwa ni Mazalia ya Urasimu, hivyo tatizo la msingi hapa ni rushwa.

Kuna aina ya urasimu ambao ni sahihi, urasimu wa kisera, TFDA ni moja ya mamlaka ambayo binafsi nategemea uwepo urasimu wa kisera au wa kiutu.

Yaani hata mimi ningekuwa mtumishi wa TFDA kutokana na mahusiano mazuri tuliyonayo na wachina au wamarekani ningeweka urasimu wa kuua mtu pale ambapo mfanyabiashara anataka kuingiza dawa ambazo ninahisi zinamadhara ya kiafya kwa wananchi.

Hapa ndio narudi kwenye tatizo la rushwa. Tunaweza kaa hapa nakulaumu watumishi woooote wa UMMA mpaka mheshimiwa Rais lakini kuna kiwango cha pesa ukiwekewa mezani kama rushwa ukikikataa kila mtu anaweza kukuona wewe ni mjinga.
Hahaha huwezi kuweka bei elekezi kwenye vifaa tiba, vifaa huvitengenezi wewe hujui costs za material zitumikazo, upatikanaji wake production costs, distribution costs, storage costs, hata technologia inayotumika kutengeneza huijui hivyo huwezi kuja na bei elekezi. Hata ukaguzi wao hauko sahihi, ni urasimu tu. Kama hujui au huna knowledge ya utengenezaji wa kitu unakaguaje ubora wake?! Ingekuwa rahisi kuziomba mamlaka za udhibiti wa ubora zinazojitosheleza kutusaidia kwenye hili, tuna copy vitu na ku vi implement nchini hata hatujui vina fanyaje kazi.
Kuna mashine zina operaye properly katika a certain temperature and humidity, na kuna chemical zinakuwa stored frozen at a certain temperature lakini hapa kwetu, tunakagua tunapohitaji pesa au kumkomoa mtu au taasisi na tunakagua vitu hata knowlege yake hatuna ni urasimu tu. Siwezi kutaja specifics ila ni mengi naweza kuandika hapa.
Anyway ndiyo nchi yetu ilivyo.
 
Ngoja ni summarize na kuchangia moja kwa moja.
1. Serikali itoe maelekezo mahususi kwamba kodi fulani inalipwa kwa currency ipi na ikipendeza kodi zote zilipwe kwa fedha yetu wenyewe.

Sasa hili sio kwa mamlaka hii tuu, usumbufu huu uko kwenye makusanyo yanayosimamiwa na mamlaka karibia zote. Hivyo hii ni kero mtambuka sio mahususi kwa TFDA pekee.

Hapa wizara ya fedha inapaswa kutimiza wajibu wake

2. Pili, kuna kodi nyingi sana. Hata hili ni kama hapo mwanzo, serikali inapotengeza mamlaka hizi ijikumbushe kwamba lengo ni kuihudumia wananchi na itambue sio kila kitu lazima wananchi walipie hasa ukizingatia tayari wanalipa kodi nyingi zinazosimamiwa na mamlaka ya mapato.

Sekta ya afya inapaswa kuwa sekta ambayo inakatwa kiwango cha kodi cha chini zaidi sababu inahusika na uhai wa wananchi moja kwa moja.

Wakati serikali inaangaika kutoa bei helekezi kwenye mazao ya biashara naishauri itoe bei elekezi kwenye huduma na bidhaa za kiafya. Itoe bei elekezi kwenye vipimo vya maradhi, itoe bei elekezi kwenye bei za madawa.

Hivyo hata katika hili, nalo ni tatizo mtambuka.

3. Urasimu na Rushwa.
Rushwa ni ushenzi tu, na Urasimu ni ushenzi tu.

Urasimu umekuwa ni utaratibu mahususi wa kiutendaji kwa wafanyakazi duniani kote. Rushwa ni Mazalia ya Urasimu, hivyo tatizo la msingi hapa ni rushwa.

Kuna aina ya urasimu ambao ni sahihi, urasimu wa kisera, TFDA ni moja ya mamlaka ambayo binafsi nategemea uwepo urasimu wa kisera au wa kiutu.

Yaani hata mimi ningekuwa mtumishi wa TFDA kutokana na mahusiano mazuri tuliyonayo na wachina au wamarekani ningeweka urasimu wa kuua mtu pale ambapo mfanyabiashara anataka kuingiza dawa ambazo ninahisi zinamadhara ya kiafya kwa wananchi.

Hapa ndio narudi kwenye tatizo la rushwa. Tunaweza kaa hapa nakulaumu watumishi woooote wa UMMA mpaka mheshimiwa Rais lakini kuna kiwango cha pesa ukiwekewa mezani kama rushwa ukikikataa kila mtu anaweza kukuona wewe ni mjinga.
Ni kweli kwamba mamlaka za usimamizi wa ubora wa bidhaa lazima zisimamie Sera za nchi. Kwa mfano, TFDA wanachofanya ni kukadiria viwango vya juu vya tozo na ada kwa bidhaa zinazoingizwa toka nje ya nchi kuliko zile zinazotengenezwa hapa nchini. Lengo la kufanya hivi ni kutekeleza Sera ya ku-discourage uingizaji wa bidhaa za nje na ku-encourage wawekezaji kuanzisha viwanda hapa nchini.

Hata hivyo, "approach" hii sio sahihi kwa vifaa tiba na dawa ambazo ni muhimu kwa Afya za wananchi. Nasema hivi ni kutokana na ukweli kwamba zaidi ya 98% ya bidhaa hizi tunategemea kuagiza kutoka nje ya nchi. Kukadiria viwango vya juu kupitia kiasi maana yake ni kuonheza gharama katika huduma ya Afya. Gharama zote za uingizaji wa bidhaa hizi zinafidiwa na waingizaji kwa watumiaji wa mwisho ambao ni wananchi.

Vile vile hii gharama ya $6000 hadi $8000 kwa ajili ya kufanya quality audit kwa viwanda vya nje ni kuonheza mzigo wa gharama ambao so wa lazima.

Lakini ikumbukwe kwamba katika kusajili au kuingiza bidhaa kwa mujibu wa mamlaka hii, nyalaka za "Quality Certification" na "Declaration of Conformity" za kimataifa (ISO, EC, n.k) lazima ziambatanishwe kwenye maombi (dossier). Sasa Kama bidhaa imekidhi viwango vya ubora wa kimataifa kwanini iwe ni lazima TFDA nao iende kufanya ukaguzi wa ubora kwenye viwanda vya nje ya nchi? Yaani wanataka kutuambia mamlaka zetu Zina viwango Bora vya ubora kuliko hizi za kimataifa ambazo bidhaa husika imekidhi? Huu no urasimu usiohitajika. Tena TFDA huwa wanadai malipo ya kufanya ukaguzi wa ubora hata kwa bidhaa ambavyo tayari imefikishwa kwao Kama sampuli. Au wakati mungine bidhaa inayoombewa kibali tayari kwenye solo la kimataifa na haijawahi kuripotiwa kuwa na madhara kwa watumiaji.
 
Hahaha huwezi kuweka bei elekezi kwenye vifaa tiba, vifaa huvitengenezi wewe hujui costs za material zitumikazo, upatikanaji wake production costs, distribution costs, storage costs, hata technologia inayotumika kutengeneza huijui hivyo huwezi kuja na bei elekezi. Hata ukaguzi wao hauko sahihi, ni urasimu tu. Kama hujui au huna knowledge ya utengenezaji wa kitu unakaguaje ubora wake?! Ingekuwa rahisi kuziomba mamlaka za udhibiti wa ubora zinazojitosheleza kutusaidia kwenye hili, tuna copy vitu na ku vi implement nchini hata hatujui vina fanyaje kazi.
Kuna mashine zina operaye properly katika a certain temperature and humidity, na kuna chemical zinakuwa stored frozen at a certain temperature lakini hapa kwetu, tunakagua tunapohitaji pesa au kumkomoa mtu au taasisi na tunakagua vitu hata knowlege yake hatuna ni urasimu tu. Siwezi kutaja specifics ila ni mengi naweza kuandika hapa.
Anyway ndiyo nchi yetu ilivyo.
Okay, sasa huu sio urasimu mkuu hili unalozungumzia ni tatizo kubwa kuliko urasimu.

Ni kwamba TFDA hawana uwezo wa kitaalamu kutimiza wajibu wao, na kwa namna umeelezea hapa ni sawa na kusema TFDA ni useless kabisa.

Na kama ni hivi inawezekana kupunguziwa majukumu ikawa ni jambo sahihi ili waweze kutekeleza yale yaliyo ndani ya uwezo wao. Ama sivyo haya ni madhara ya umasikini, serikali yetu haina uwezo wa kuwekeza kwa rasilimali watu na vifaa na nyenzo zinazoendana na mabadiriko ya kisayansi na ubunifu usiokoma katika sekta ya afya.

Lakini swala la kupanga bei elekezi bado naona kuwa ni la msingi, mathalani, chukulia dawa kama panadol, kwa nini kidonge kimoja kisiuzwe shilingi ishirini?

Nyie wafanyabiashara wa sekta ya afya mnatengeneza faida kubwa sana bila kujali kwamba mnasababisha wananchi wengi kukosa huduma za afya.

Mnavipimo vingine kama Ct Scan mfano,inagharimu karibia shilingi 500,000 kupata hiki kipimo, huu si ubaguzi wa makusudi hii, wengi wa wanaohitaji kipimo hiki hawawezi kumudu bei matokeo yake wanapoteza maisha.
 
Hayo ni kero kwa biashara kubwa, hata wadogo hajaachwa na tfda. Mama Lishe analipishwa sh 50000 kupata cheti cha ubora wa chakula, wakati si mzalishaji, na kila siku anapika vyakula tofauti!Hata muuza duka reja reja?
 
Ni kweli kwamba mamlaka za usimamizi wa ubora wa bidhaa lazima zisimamie Sera za nchi. Kwa mfano, TFDA wanachofanya ni kukadiria viwango vya juu vya tozo na ada kwa bidhaa zinazoingizwa toka nje ya nchi kuliko zile zinazotengenezwa hapa nchini. Lengo la kufanya hivi ni kutekeleza Sera ya ku-discourage uingizaji wa bidhaa za nje na ku-encourage wawekezaji kuanzisha viwanda hapa nchini.

Hata hivyo, "approach" hii sio sahihi kwa vifaa tiba na dawa ambazo ni muhimu kwa Afya za wananchi. Nasema hivi ni kutokana na ukweli kwamba zaidi ya 98% ya bidhaa hizi tunategemea kuagiza kutoka nje ya nchi. Kukadiria viwango vya juu kupitia kiasi maana yake ni kuonheza gharama katika huduma ya Afya. Gharama zote za uingizaji wa bidhaa hizi zinafidiwa na waingizaji kwa watumiaji wa mwisho ambao ni wananchi.

Vile vile hii gharama ya $6000 hadi $8000 kwa ajili ya kufanya quality audit kwa viwanda vya nje ni kuonheza mzigo wa gharama ambao so wa lazima.

Lakini ikumbukwe kwamba katika kusajili au kuingiza bidhaa kwa mujibu wa mamlaka hii, nyalaka za "Quality Certification" na "Declaration of Conformity" za kimataifa (ISO, EC, n.k) lazima ziambatanishwe kwenye maombi (dossier). Sasa Kama bidhaa imekidhi viwango vya ubora wa kimataifa kwanini iwe ni lazima TFDA nao iende kufanya ukaguzi wa ubora kwenye viwanda vya nje ya nchi? Yaani wanataka kutuambia mamlaka zetu Zina viwango Bora vya ubora kuliko hizi za kimataifa ambazo bidhaa husika imekidhi? Huu no urasimu usiohitajika. Tena TFDA huwa wanadai malipo ya kufanya ukaguzi wa ubora hata kwa bidhaa ambavyo tayari imefikishwa kwao Kama sampuli. Au wakati mungine bidhaa inayoombewa kibali tayari kwenye solo la kimataifa na haijawahi kuripotiwa kuwa na madhara kwa watumiaji.
Huu ni urasimu dhahiri kabisa.huu naupinga. Sisi ni sehemu ya jumuiya ya kimataifa, cha kufanya tujitahidi kuwa active members kwenye hizi standard setting boards ama sivyo hiyo redundancy ya ukaguzi haina umuhimu, haiongezi tija zaidi ya kusababisha usumbufu na kutengeneza mazingira ya rushwa na uzembe.

Mambo kama haya mheshimiwa magufuri binafsi akiyaelewa sawasawa anauwezo wa kuyarekebisha mara moja.
 
Mlolongo ni mrefu sana...


Cc: mahondaw
Ni kweli ugomvi wa TFDA na wafanyabiashara wa " Madawa na Vipodozi" ilikuwa ni huo mlolongo na tozo!!??
Personally siamini, huko walikohamishiwa hizo tozo zimefutwa au zitapunguzwa?
Kwa tusifikirie nje ya box? Wafanya biashara lazima waichukie TFDA hasa hasa hao wa Madawa na vipodozi...TFDA walikuwa wakiwabana mno kwenye dawa na vipodozi fake, wafanya biashara wengi walioingia ndani ya kumi na nane za TFDA walikiona,jamaa mostly walikuwa hawahongeki wameteketeza sana mafake yao. Walichofanya ni kuanzisha figisu kwa kuituhumu TFDA lakini hakuna ukweli hapo, walikuwa wanabanwa hawapumui.
Na kwa sasa tujiandae kwa kulishwa dawa na vipodozi fake!!!!
Hizo tozo na urasimu ni gelesha tu tunaletewa,ukweli ni kibano cha TFDA kiliwanyoosha wafanya biashara.
 
Okay, sasa huu sio urasimu mkuu hili unalozungumzia ni tatizo kubwa kuliko urasimu.

Ni kwamba TFDA hawana uwezo wa kitaalamu kutimiza wajibu wao, na kwa namna umeelezea hapa ni sawa na kusema TFDA ni useless kabisa.

Na kama ni hivi inawezekana kupunguziwa majukumu ikawa ni jambo sahihi ili waweze kutekeleza yale yaliyo ndani ya uwezo wao. Ama sivyo haya ni madhara ya umasikini, serikali yetu haina uwezo wa kuwekeza kwa rasilimali watu na vifaa na nyenzo zinazoendana na mabadiriko ya kisayansi na ubunifu usiokoma katika sekta ya afya.

Lakini swala la kupanga bei elekezi bado naona kuwa ni la msingi, mathalani, chukulia dawa kama panadol, kwa nini kidonge kimoja kisiuzwe shilingi ishirini?

Nyie wafanyabiashara wa sekta ya afya mnatengeneza faida kubwa sana bila kujali kwamba mnasababisha wananchi wengi kukosa huduma za afya.

Mnavipimo vingine kama Ct Scan mfano,inagharimu karibia shilingi 500,000 kupata hiki kipimo, huu si ubaguzi wa makusudi hii, wengi wa wanaohitaji kipimo hiki hawawezi kumudu bei matokeo yake wanapoteza maisha.
Hahaha ni rahisi kusema "bei elekezi" hiki kitu mkiacha siasa siyo rahisi na hakitekelezeki PASIPO MSAADA.,
Huduma nyingi ziko subsidized na serikali, Panadol ni rahisi ukiiona lakini gharama za utengenezaji wake zinaongezeka kila siku,, ct scan ni rahisi lakini service na maintenance zake ni very expensive, lakini mgonjwa hajui hayo, wewe na mimi tunapenda first class services lakini serikali hazina uwezo wa kuzitoa, hivyo tunapata subsidy kutoka kwa donor countries wao hulipia pakubwa panapobaki tunachangia kupitia health insurances na costs sharing zingine.
Kwa mazingira yaliyopo huwezi kupata huduma nzuri 100% ni uongo.
Hayo ma TFDA ni sehemu ya ukandamizaji unaomuongezea mlaji gharama za huduma, kazi yao hata bila kuwa na taasisi inafanyika, lakini kuna majengo, wakurugenzi na takataka nyiingi unnecessarily. Jiulize unadhani tunahitaji jeshi la zimamoto lenye mabrigedia ,makamishna na vyeo vyote vile mabegani?! Moto unazimwa na brigedia au nyota mabegani?! Lakini siku hizi kuna tozo za kuzuia moto, unadhani anaumizwa nani kama siyo mwananchi?!
Hayo mataasisi sisi tuna copy na ku implement kwetu hata hayafunction kama yalivyokuwa intended, TBS,TFDA, OSHA, ni mizigo to, tuunde vyetu vyenye uhalisia wetu, kama wazungu wanataka tuwe navyo wavifund wao 100% na waweke operational policies na procedures of how to use na tupate training nzuri, othewise tutalia mpaka kiama. Mnatengeneza kazi kwa watu lakini system hazifanyi kazi.
 
Ni kweli ugomvi wa TFDA na wafanyabiashara wa " Madawa na Vipodozi" ilikuwa ni huo mlolongo na tozo!!??
Personally siamini, huko walikohamishiwa hizo tozo zimefutwa au zitapunguzwa?
Kwa tusifikirie nje ya box? Wafanya biashara lazima waichukie TFDA hasa hasa hao wa Madawa na vipodozi...TFDA walikuwa wakiwabana mno kwenye dawa na vipodozi fake, wafanya biashara wengi walioingia ndani ya kumi na nane za TFDA walikiona,jamaa mostly walikuwa hawahongeki wameteketeza sana mafake yao. Walichofanya ni kuanzisha figisu kwa kuituhumu TFDA lakini hakuna ukweli hapo, walikuwa wanabanwa hawapumui.
Na kwa sasa tujiandae kwa kulishwa dawa na vipodozi fake!!!!
Hizo tozo na urasimu ni gelesha tu tunaletewa,ukweli ni kibano cha TFDA kiliwanyoosha wafanya biashara.
Inapolalamikiwa TFDA haimaanishi kuifanyia figisu. Mambo yanayozungumzwa kuhusu mamlaka hii yapo kweli. Mathalani wanaoingiza bidhaa wako hapa nchini Sasa kwanini wawekewe viwango vya malipo kwa thamani ya Dola? Kwanini TFDA inakata 2% ya FOB price ya mzigo unaoingizwa wakati bidhaa husika imeshalipiwa Ada ya usajili na tayari imesajaliwa?

Kwa taarifa yako linapokuja suala la ubora wa vifaa tiba ni watumiaji wenyewe ambao ndo wana utaalam wakujua. Kwa lugha nyingine, bidhaa Fulani inaweza kuidhinishwa/kusajiliwa na TFDA kwa maana imekidhi ubora lakini bidhaa hiyo hiyo inaweza kukataliwa na mtaalam anayetumia kwamba haina ubora. Mara nyingi wataalum wa Afya wanapohitaji kununua vifaa tiba wanakuwa tayari wanajua nini wanachokitaka na hivyo Basi huainisha sofa za kiufundi (technical specifications) za bidhaa husika.

Ukweli ni kwamba idhini ya TFDA haitoi garantii ya ubora, usalama na UFANISI wa bidhaa husika. Hata TFDA wenyewe wanalijua hilo, ndio maana wanafanya kitu kinachoitwa "post-market surveillance" kwa bidhaa zilizosajiliwa ili wachukue hatua stahiki inapotokea bidhaa iliyosajiwa na kuingiza sokoni imebainika na watumiaji kuwa sio bora.

Hii maana yake ni kwamba TFDA Kama mamlaka haimaanishi wako "perfect" Kama unavyodhani.

Labda nikupe mfano hai kuthibitisha udhaifu wa mamlaka hii. Kuna mtaalam mmoja kutoka MUCE alifanya utafiti juu ya "prevalenve" ya sumukuvu (aflatoxin) kwenye mafuta na masudu ya arizeti hapa nchini na kubaini uwepo wa sumu hiyo kwa kiwango kikubwa. Mamlaka ililaani kuchapishwa kwa ripoti ripoti ya utafiti huu na ikapiga maruku kufanya tafiti Kama hizi kwenye vyakula bila kuitaarifu mamlaka kww kisi gizio kwamba ripoti unaweza kuleta hofu na taaruki kwa jamii, bali wao ndio wenye mamlaka ya kutoa taarifa za usalama wa bidhaa za vyakula na ikawataka jamii kupuuza taarifa hiyo kwavile hakutolewa na TFDA.

Cha ajabu Sasa, TFDA wenyewe wanafanya kampeni ya kuelimisha wakulima na wafanyabiashara wa nafaka na arizeti kutuambia na kutekeleza njia Bora za utunzaji wa bidhaa hizo kuepuka sumukuvu. Sasa mtu makini anaweza kuhoji ikiwa waliwataka jamii kupuuza taarifa ya uwepo wa sumukuvu kwenye nafaka na arizeti kwanini Sasa wanatia elimu kuzuia tatizo Hilo?
 
Mimi siyo mfanyabiashara wala mtaalamu wa Dawa na vifaa tiba. Ila kwa jinsi ulivyoeleza naona kuna matatizo pande zote mbili. Upande wa wafanyabiashara na upande wa TFDA.

Kwa Wafanyabiashara.
1. Nafikiri kabla hujaagiza mzigo inabidi ucheki kwanza kama bidhaa unayo agiza imeandikishwa au la. Ili kama haijaandikishwa ufanye utaratibu wa kuandikisha. Uandikishaji wa bidhaa za dawa huchukua muda mrefu. Hivyo unawajibu wa kumshirikisha mteja wako katika hili na kama inawezekana aangalie alternative product.
2. Usajili wa bidhaa za dawa na vifaa tiba unatakiwa ufanywe na mtengenezaji wa bidhaa, au wakala aliyethibitishwa na mtengenezaji. Hii maana yake ni kwamba gharama inatakiwa kubebwa na mtengenezaji au wakala wake na siyo muuzaji. Na kama wewe ni mfanyabiashara unataka kuagiza bidhaa ambayo haijaandikishwa Tanzania, basi ni vyema kwanza ukawasiliana na mtengenezaji ili akupe uwakala. Maana yake ni kwamba ukishakuwa wakala na ukasajili dawa, mfanyabiashara yeyete ambaye ataagiza hiyo dawa itabidi aagize kupitia wewe wakala.
3. Import permit inatakiwa kupatikana kabla ya kuagiza mzigo, ili mzigo usikae muda mrefu bandarini.

Kwa TFDA
1. Nadhani kuna haja ya kufanya kitu kinaitwa process re-engineering. Ukiangalia maelezo yako ni kama vile michakato (processes) haijaandishwa vyema na kujua ni taarifa gani unatakiwa uwasilishe katika mazingira fulani. Hili ni tatizo la taasisi nyingi za umma.
2. Sina uhakika kama wateja wao yaani wafanyabiashara wana access ya kuangalia kwenye mtandao/mfumo taarifa za dawa zilizo sajiliwa kabla ya kuagiza. hii inatakiwa iwe open access.
3. Dawa na vifaa tiba vipya vinagunduliwa na kutengenezwa kila siku. Sdhani kama TFDA wana uwezo kwa maana wa idadi ya watumishi, vitendea kazi na ujuzi wa kuthibitisha kila dawa na kifaa tiba ikiwa ni pamoja na kusafiri huko nje ya nchi kukagua viwanda. Nadhani kila nchi ina FDA yake. Hizi FDA zinatakiwa zifanye kazi kwa ushirikiano, kwa sababu zote zinatumia miongozo ya WHO. Hivyo basi TFDA wanatakiwa kuwa na makubaliano na FDA zingine, ili kutumia sasa...kama kifaa au dawa imesajiliwa na mamlaka ambayo wana makubaliano nayo basi moja kwa moja na wao waipe usajili, hata kama ni usajili wa awali wakati wakiendelea na mchakato mrefu wa usajili wa kudumu.
4. Serikali ilishatoa maaelekezo kwamba huduma zote zilipiwe kwa TZS
Ni hayo tu
 
Kuna Bodi ya Maziwa na Nyama, wale ni TFDA Nyingine...

Sijui kwanini Serikali iliziacha hizo taasisi. Hazijulikani zinafanya nini..

Waziri wa Viwanda na Biashara aziangalie hizo taasisi mbili
 
Hahaha huwezi kuweka bei elekezi kwenye vifaa tiba, vifaa huvitengenezi wewe hujui costs za material zitumikazo, upatikanaji wake production costs, distribution costs, storage costs, hata technologia inayotumika kutengeneza huijui hivyo huwezi kuja na bei elekezi. Hata ukaguzi wao hauko sahihi, ni urasimu tu. Kama hujui au huna knowledge ya utengenezaji wa kitu unakaguaje ubora wake?! Ingekuwa rahisi kuziomba mamlaka za udhibiti wa ubora zinazojitosheleza kutusaidia kwenye hili, tuna copy vitu na ku vi implement nchini hata hatujui vina fanyaje kazi.
Kuna mashine zina operaye properly katika a certain temperature and humidity, na kuna chemical zinakuwa stored frozen at a certain temperature lakini hapa kwetu, tunakagua tunapohitaji pesa au kumkomoa mtu au taasisi na tunakagua vitu hata knowlege yake hatuna ni urasimu tu. Siwezi kutaja specifics ila ni mengi naweza kuandika hapa.
Anyway ndiyo nchi yetu ilivyo.

Mkuu umeongea maneno kuntu.
Huwa najiuliza kwann ukaguz unakuja mpk mtu aombe Permit ya kitu fulan!?
Mf nilikuwa nataka Export Permitt ya kusafirisha samaki nje ya nchi nmefatilia huo mlolongo wake na presha nkapata
Yaani wanakwambia mpk kiwanda au eneo linalotoa/kukaushwa hap samaki likaguliwe.
Sasa hoja yangu cyo kukaguliwa, hoja kwann ukaguzi unakuja baada ya mtu kuomba LESENI ya kitu fulani...!?
Kyo wananchi wa tz hawahitaji ubora wa samaki, utengenezwaji na michakato yote ila wakiskia samaki inaenda nje nd wanahaha” ooh lazma tukague kiwanda chako c unajua ukipeleka samaki wabovu/ wenye sumu serikali nd italaumiwa na si ww”
Kwann kusiwe na utaratibu wa kukagua viwanda vyetu na maeneo yote kwanz hii itapunguza urasimu sana.
Wakt mwengne naungana na Zitto Kabwe hii nchi inakwama kwa Viongoz wake kukosa Maarifa tu
Tunakwama wapi sisi jamn hata ktk mambo ya kawaida tu tunashindwa
 
Mwandishi ana ajenda mbaya sana. Mfumo unaotumiwa na TMDA ni wa kimataifa ( soma kwenye website IMDRF/ GHTF). Msingi huu unatumika na WHO Prequalification Program. Kwa taarifa mfumo huu umeifanya WHO kuitambua TFDA kuwa ya kwanza Africa kufika level 3 maturity kwenye medicine na kwenye vitendanishi Ndiyo best in Africa. Mfano mzuri WHO huchukua miezi 6-9 kupitisha dawa au kitendanishi. Tukifuata ushauri wako nchi yetu itatumia vifaa vya Afya vilivyo hatari sana.
 
Mwandishi ana ajenda mbaya sana. Mfumo unaotumiwa na TMDA ni wa kimataifa ( soma kwenye website IMDRF/ GHTF). Msingi huu unatumika na WHO Prequalification Program. Kwa taarifa mfumo huu umeifanya WHO kuitambua TFDA kuwa ya kwanza Africa kufika level 3 maturity kwenye medicine na kwenye vitendanishi Ndiyo best in Africa. Mfano mzuri WHO huchukua miezi 6-9 kupitisha dawa au kitendanishi. Tukifuata ushauri wako nchi yetu itatumia vifaa vya Afya vilivyo hatari sana.
Ndugu yangu sina ajenda mbaya, lakini ikiwa wewe ni mtumishi wa mamlaka hii ni haki yako kutetea. Hata hivyo, ningekuomba uyachukulie maoni yangu na yale ya wachangiaji kama "customer feedback" juu ya utendaji wenu ili kuboresha zaidi. Kumbuka maoni yangu yanatokana na uzoefu wangu na taratibu za mamlaka hii. Lakini unaposema ushauri wangu wa kuisuka upya na kupunguza viwango vya tozo eti haufai kwasababu utatoa mwanya kwa bidhaa hatarishi kuingizwa kwenye soko letu, ni kudhihirisha hofu uliyonayo juu ya usalama wa maslahi yako kama mtumishi katika mamla hii.

Nakubaliana na wewe kwamba TFDA inatambuliwa na WHO kama Maturity Level 3 Regulator, bali ni mamlaka ya kwanza Africa kuingia kwenye category hii. Naipongeza TFDA kwa mafanikio haya. Hata hivyo, madai yako kwamba kutambulika huko ni kutokana na TFDA kutumia "mfumo wa IMDRF/GHTF" ni upotoshaji wa makusudi au kutokujua. Ukweli ni kwamba, ingawa vinashirikiana, WHO na IMDRF/GHTF ni vitu viwili tofauti. Wala WHO hawatumii mfumo wa IMDRF/GHTF kufanya hicho unachokiita "Prequalification Program".

Karibu kila mtu anafahamu WHO ni nini, lakini wengi huenda hawafamu kuhusu IMDRF na GHTF. Kirefu cha IMDRF ni International Medical Devices Regulators Forum, ni jukwaa linalozikutanisha mamlaka za udhibiti wa vifaa tiba kutoka nchi mbali mbali hapa duniani ili kujadili na kufikia maazimio juu ya udhibiti wa vifaa tiba. Jukwaa hili lilianzishwa 2011 na mamlaka kutoka nchi za Marekani, Ulaya, Brazil, Japani Korea, Canada n.k. Kwa upande mwingine, GHTF ni kifupi cha Global Harmonization Task Force. Hiki ni Kikosi kazi cha IMDRF chenye jukumu la kuratibu ulinganifu katika taratibu za udhibiti wa vifaa tiba miongoni mwa nchi wanachama. Kiufupi shabaha ya IMDRF/GHTF ni kuleta usawa au ulinganifu wa taratibu za udhibiti wa vifaa tiba, yaani majina, makundi na viwango vya ubora vya vifaa tiba visitofautiane kati ya nchi na nchi. Uhusiano wa WHO na IMDRF ni kwamba katika mikutano ya IMDRF, WHO hualikwa kama muangalizi (observer)

Sasa unaposema WHO wanatumia mfumo wa IMDRF/GHTF kufanya categorization za regulatory boards sio kweli. WHO ni organization ya muda mrefu, wakati IMDRF hadi sasa haijatimiza hata muongo mmoja. Ukweli ni kwamba, tangu mwaka 1997 WHO imekuwa ikihakiki national regulatory systems zote zikiwemo zinazounda IMDRF na kuzipanga kwenye categories za maturity level. Kiufupi tunaweza kusema WHO ni mdhibiti wa wadhibiti wote wa vifaa tiba duniani. Nyenzo inayotumiwa na WHO kuhakiki na kuzipangia madaraja mamlaka za udhibiti wa vifaa tiba inaitwa Global Benchmarking Tool (GBT) na sio mfumo wa IMDRF/GHTF kama unavyosema.

Lakini tunapozungumzia kutambulika kwa TFDA na WHO kama ni maturity level 3 regulator maana yake ni kwamba, TFDA kama mamlaka ya udhibiti, ina mfumo imara na uwezo wa kutekeleza majukumu yake. Kuwa na mfumo imara na uwezo wa kutekeleza majukumu ya udhibiti haimaanishi TFDA inatoa huduma bora kwa wateja wake (customer expectations). Kumbuka kwamba, TFDA kama organization, inakabiliwa na mambo mawili kuhusu ubora wake; regulatory requirements (WHO/GBT) na quality standards (ISO). Regulatory requirements haziko pale ili kumridhisha mteja wa organization, jambo linalomlenga mteja ni quality system.

Kwa bahati nzuri, TFDA ina mfumo wake wa ubora unaokidhi viwango vya ISO9001. Kwa maana hiyo, TFDA inapasa kutambua kanuni zifuatazo kuhusu quality system:

1. It is not possible to achieve perfection. Yaani hakuna organization iliyokamilika katika ubora na malalamiko ya wateja kuhusu tozo, urasimu na rushwa ndo kielelezo cha "imperfection". Kwa maana hiyo kufanikiwa kutambuliwa na WHO au ISO kusiwape kiburi TFDA dhidi ya wateja wake kwa kujiona wako sawa. Bado wana safari ndefu.
2. Organizations should continually strive to be better through learning and problem solving. Changamoto za ubora huwa haziishi hata kama organization imefikia kiwango fulani cha ubora. Kwa kujifunza na kutatua changamoto

Kwa kumalizia nikupe changamoto. Kama kweli TFDA/TMDA wanatumia hicho unachokiita "mfumo wa kimataifa wa IMDRF/GHTF" katika utaratibu wa udhibiti kwanini basi hawasajili vifaa tiba vilivyoidhinishwa na vinavyotoka kwenye viwanda vilivyo katika nchi zenye mamlaka za udhibiti zinazounda IMDRF mpaka waende wenyewe kufanya ukaguzi?
 
Mwandishi ana ajenda mbaya sana. Mfumo unaotumiwa na TMDA ni wa kimataifa ( soma kwenye website IMDRF/ GHTF). Msingi huu unatumika na WHO Prequalification Program. Kwa taarifa mfumo huu umeifanya WHO kuitambua TFDA kuwa ya kwanza Africa kufika level 3 maturity kwenye medicine na kwenye vitendanishi Ndiyo best in Africa. Mfano mzuri WHO huchukua miezi 6-9 kupitisha dawa au kitendanishi. Tukifuata ushauri wako nchi yetu itatumia vifaa vya Afya vilivyo hatari sana.
evidences za hizo Tanzanian ranks?
 
Back
Top Bottom