Tatizo si kukosa sheria, Tatizo letu ni udhaifu na kukosekana uwajibikaji kusimamia sheria na kanuni!

Rev. Kishoka

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
4,526
1,529
Watanzania tuna tatizo moja kubwa sana, nalo ni umaikini, umadhubuti, uwajibikaji wa usimamizi wa kanuni, sheria hata katiba!

Si kweli kuwa sheria nyingi ni dhaifu, butu au hakuna "makali" ya kisheria au hata kikatiba. Tatizo letu ni lile lile usimamizi mzuri wa kanuni, sheria na katiba kwa ufanisi, kuzingatia haki, kufuata taratibu na la zaidi kutimiza wajibu ipaswavyo: Kuwajibika.

Majuzi Benki Kuu ilipitia maduka ya fedha Dar, sawa na ilivyofanya maduka ya fedha Arusha mwaka jana. Matamko ya BOT ni kuwa wenye maduka wanakiuka masharti ya uendeshaji maduka hayo.

Leo naibu waziri wa mawasiliano katoa tamko kukataza usafirishaji wa vifurushi kwa njia binafsi mpaka wasafirishaji wapewe vibali na TCRA.

Naomba nimnukuu Rais Magufuli jana kusmea "Watanzania si wajinga sana... niongezee kiasi hicho! Watanzaia si Wajinga, wala si Wajinga sana au Wajinga kidogo. Tunauwezo wa kuuliza na kuhoji na kuuliza na kuhosi kwetu hata kama kutaishia kubaininsha mapungufu au kukosoa haina maana sisi hatuna uzalendo, ni makuwadi wa mabeberu au tunapiga vita kasi ya maendeleo inayofanywa na Serikali ya awamu ya tano.

Suala la BoT na Vifurushi vimenifanya nipekue mtanda na kupitia sheria za Maduka ya fedha na sheria za Posta.

Nilichokikuta kwenye sheria hizo ni uwepo wa misingi thabiti na imara yenye kubainisha masharti ya uendeshaji wa shughuli hizo za biashara (maduka ya pesa, usafirishaji barua na vifurushi) na udhibiti wake ama kwa namna ingine ukaguzi kutoka kwa wenye majukumu ya ukaguzi (regulatory and licencing bodies) kuhakikisha unyoofu wa shughuli hizo za biashara.

Sheria ya BoT ya Maduka ya fedha ya 2015 na 2017 zinazungumzia wenye maduka kuwa na kumbukumbu za mauzo na manunuzi ya fedha na kila transaction ifuate masharti ya kuendesha biashara pamoja na kumjua mteja (Know your customer) na kuzuia utakatishaji wa fedha (Anti Money Laundry and Anti terrorism policy).

Kwenye sheria za Posta za national Postal Policy ya 2018, Postal regulation act ya 2018 na Electronic and Postal Communication quality of services regulation act of 2017, zinazungumzia kwa kina watoaji wa huduma za usafirishaji wa barua na vifurushi kuwa wamesajiliwa na mamlaka husika na wawe wanafuata kanuni, sheria na wajibu kwa mujibu wa sheria.

Aidha kwa sheria zote za BoT na za Posta, kuna msisitizo wa ukaguzi wa uendeshaji biashara hizo kutoka mamlaka husika: supervision and inspection- audit.

Sasa najiuliza, kama yote haya yapo kwenye sheria zetu, inafikaje kunakuwa na uvunjifu mkubwa wa sheria hizi tena kwa muda mrefu bila woga na kuzaa gonjwa la watu kutokufuata kanuni na sheria?

Je leo tunapoona watendaji wanakimbia kuwasilisha miswaada mipya ya sheria na kulundika mafaili kwa Rais apitishe sheria mpya "kali" ni kuficha madhaifu yao ya kushindwa kuwajibika ipaswavyo an kujitengenezea njoa ya mkato ya kuongeza sheria ambazo kiuhalisia zipo sema utekelezaji wake kutoka kwa regulators ni dhaifu?

Je inakuwaje tunakuwa na watendaji ambao wanashindwa kusimamia kwa dhati kanuni na sheria na badala yake kutoa matamko au kufanya mambo ambayo kwa Ujinga wetu mdogo au kutokuwa wajinga sana tunajiuliza kulikoni?

What does Magufuli need to do to fix this problem of lack of accountability kutoka kwa watendaji ( na sizungumzii mawazirri na wateuliwa, hapa ongeza makatibu wakuu, wakurugenzi wa idara na kadhalika)?

Napenda kutoa hoja!
 
Mkuu ahsante kwa hoja fikirishi sana. Baada ya kukusoma nimebaini tatizo si usimamizi, kuna jingine la ukweli panapotokea tatizo

1. BoT wanakitengo cha ukaguzi kinachoongozwa na sheria husika.
Wakaguzi wamefanya nini kwa mwaka au miaka kiasi cha hali kuwa kama ilivyo sasa?

Sheria huwekwa kama utaratibu unaopaswa kufuatwa lakini pia sheria zinawekwa kukabiliana au kuzuia matumizi mabaya ya fursa au mamlaka. BoT wanazo sheria walizitumia wapi na lini!
Na kwanini hawakuzitumia katika usimamizi wa maduka ya kubadili fedha ambao ni wadau wao

Kwa hili la BoT sidhani kama tatizo linalosemwa ndilo, nadhani kuna jingine tusilojua lakini lipo

2. Kuhusu usafirishaji wa vifurushi, kujisajili TCRA kmelenga nini na kwa nani
Hapa nina maana kwa serikali na wananchi ambao ni wateja pamoja na hao wafanyabiashara

Njia ya kusafirsha vifurushi imekuwepo kwa njia za mabasi na nyinginezo kwa miaka mingi
Shirika la Posta lilikuwa na Monopoly kabla ya soko huru lililowaingiza DHL, UPS n.k
Kitu gani kimeonekana tofauti kwa mujibu wa sheria ulizozipitia na kuainisha?

Lengo la hatua zote mbili, BoT na Posta ni Monoply ili kupitia hilo serikali ipate mapato
Hii ni njia dhaifu sana kwani monoply ya RTC haikufanya kazi zama hizo seuse leo

Yapo ya kufikirisha
 
....
What does Magufuli need to do to fix this problem of lack of accountability kutoka kwa watendaji ( na sizungumzii mawazirri na wateuliwa, hapa ongeza makatibu wakuu, wakurugenzi wa idara na kadhalika)?

Napenda kutoa hoja!

Kwanza niseme I lean heavily on the libertarian side -- keep the government small -- less regulations; decentralization; little interference to private enterprises; protect individual responsibilities and individual rights; the state should be less of Nanny State; government institutions should never be refa-mchezaji. In short, preference to organized chaos. Then, the duty of the government becomes to almost do nothing... leave everything to the populace, just providing boundary conditions.

"Government's view of the economy could be summed up in a few short phrases: If it moves, tax it. If it keeps moving, regulate it. And if it stops moving, subsidize it." Ronald Reagan. Read more at: Ronald Reagan Quotes [edit: Reagan was against too much taxation and overregulation, which hampers growth, forcing the government to subsidize busines])

Probably what needs to be done is ensure everything is chaotically organized, if you hear what I'm sayin', and make sure a lot of bureaucracy is unneeded.
 
Then, the duty of the government becomes to almost do nothing... leave everything to the populace, just providing boundary conditions.

"Government's view of the economy could be summed up in a few short phrases: If it moves, tax it. If it keeps moving, regulate it. And if it stops moving, subsidize it." Ronald Reagan.

Probably what needs to be done is ensure everything is chaotically organized, if you hear what I'm sayin', and make sure a lot of bureaucracy is unneeded.
Mkuu, mfumo tunaofuata ni 'makande' I mean maharage, mahindi, vitunguu, mafuta ya kupikia n.k. vyote kwa pamoja

Kazi ya serikali 'provide boundary conditions' ili kuwe na fairness katika competitions,kuzuia exploitation ya public na kuondoa bureaucracy .

Katika mazingira hayo serikali inabaki na jukumu lake kubwa 'tax it, regulate and subsidize if necessary''

Ninaamini katika serikali kujiondoa katika ''biashara'' na kuacha nguvu ya soko itawale
Hili haliondoi nguvu ya serikali kuwa msimamizi wa shughuli za nchi

Nguvu ya soko inachagiza innovation, creativity,competition, quality and quantity
Vitu hivi huvipati ukiwa na 'monopoly', tulijaribu hatukupata matokeo mazuri

KAMATA, RTC, UDA, KILI MATCH BOX, MRADI WA MABASI DAR, BENKI NBC, THB, TIB na vingine vingi vikufanje ndani ya monopoly na gov subsidy!

Kama lengo ni kupata pesa kwanini hatuangalii maeneo mengine kwa jicho la ukaribu?
Kwanini kuna western Union inayochukua dollar za transmittance za diaspora kupeleka nje

Kwamba serikali haiwezi kutengeneza mazingira yatakayovutia hao diaspora kuchangia pato la nchi na si 'mabeberu' kwa kuwa na mifumo yetu bila yenyewe kujihusisha!

Ni kiasi gani kinachoweza kupatikana ukilinganisha na kusajili wapeleka vifurshi wa mabasi

Kama benki ya Posta imepewa monoply ya kupanga viwango vya Forex hivi hiyo haitachagiza black market kushamiri na hapo serikali itakuwa imetoa suluhu ipi ya tatizo

Umakini ni kuangalia historia, tulipo na tunapokwenda. Kwanini hatujifunzi?
 
Watanzania tuna tatizo moja kubwa sana, nalo ni umaikini, umadhubuti, uwajibikaji wa usimamizi wa kanuni, sheria hata katiba!

Si kweli kuwa sheria nyingi ni dhaifu, butu au hakuna "makali" ya kisheria au hata kikatiba. Tatizo letu ni lile lile usimamizi mzuri wa kanuni, sheria na katiba kwa ufanisi, kuzingatia haki, kufuata taratibu na la zaidi kutimiza wajibu ipaswavyo: Kuwajibika.

Majuzi Benki Kuu ilipitia maduka ya fedha Dar, sawa na ilivyofanya maduka ya fedha Arusha mwaka jana. Matamko ya BOT ni kuwa wenye maduka wanakiuka masharti ya uendeshaji maduka hayo.

Leo naibu waziri wa mawasiliano katoa tamko kukataza usafirishaji wa vifurushi kwa njia binafsi mpaka wasafirishaji wapewe vibali na TCRA.

Naomba nimnukuu Rais Magufuli jana kusmea "Watanzania si wajinga sana... niongezee kiasi hicho! Watanzaia si Wajinga, wala si Wajinga sana au Wajinga kidogo. Tunauwezo wa kuuliza na kuhoji na kuuliza na kuhosi kwetu hata kama kutaishia kubaininsha mapungufu au kukosoa haina maana sisi hatuna uzalendo, ni makuwadi wa mabeberu au tunapiga vita kasi ya maendeleo inayofanywa na Serikali ya awamu ya tano.

Suala la BoT na Vifurushi vimenifanya nipekue mtanda na kupitia sheria za Maduka ya fedha na sheria za Posta.

Nilichokikuta kwenye sheria hizo ni uwepo wa misingi thabiti na imara yenye kubainisha masharti ya uendeshaji wa shughuli hizo za biashara (maduka ya pesa, usafirishaji barua na vifurushi) na udhibiti wake ama kwa namna ingine ukaguzi kutoka kwa wenye majukumu ya ukaguzi (regulatory and licencing bodies) kuhakikisha unyoofu wa shughuli hizo za biashara.

Sheria ya BoT ya Maduka ya fedha ya 2015 na 2017 zinazungumzia wenye maduka kuwa na kumbukumbu za mauzo na manunuzi ya fedha na kila transaction ifuate masharti ya kuendesha biashara pamoja na kumjua mteja (Know your customer) na kuzuia utakatishaji wa fedha (Anti Money Laundry and Anti terrorism policy).

Kwenye sheria za Posta za national Postal Policy ya 2018, Postal regulation act ya 2018 na Electronic and Postal Communication quality of services regulation act of 2017, zinazungumzia kwa kina watoaji wa huduma za usafirishaji wa barua na vifurushi kuwa wamesajiliwa na mamlaka husika na wawe wanafuata kanuni, sheria na wajibu kwa mujibu wa sheria.

Aidha kwa sheria zote za BoT na za Posta, kuna msisitizo wa ukaguzi wa uendeshaji biashara hizo kutoka mamlaka husika: supervision and inspection- audit.

Sasa najiuliza, kama yote haya yapo kwenye sheria zetu, inafikaje kunakuwa na uvunjifu mkubwa wa sheria hizi tena kwa muda mrefu bila woga na kuzaa gonjwa la watu kutokufuata kanuni na sheria?

Je leo tunapoona watendaji wanakimbia kuwasilisha miswaada mipya ya sheria na kulundika mafaili kwa Rais apitishe sheria mpya "kali" ni kuficha madhaifu yao ya kushindwa kuwajibika ipaswavyo an kujitengenezea njoa ya mkato ya kuongeza sheria ambazo kiuhalisia zipo sema utekelezaji wake kutoka kwa regulators ni dhaifu?

Je inakuwaje tunakuwa na watendaji ambao wanashindwa kusimamia kwa dhati kanuni na sheria na badala yake kutoa matamko au kufanya mambo ambayo kwa Ujinga wetu mdogo au kutokuwa wajinga sana tunajiuliza kulikoni?

What does Magufuli need to do to fix this problem of lack of accountability kutoka kwa watendaji ( na sizungumzii mawazirri na wateuliwa, hapa ongeza makatibu wakuu, wakurugenzi wa idara na kadhalika)?

Napenda kutoa hoja!
Wakaguzi ( regulatory authorities ) zipo lakini hazina budget. Zitafanyaje kazi? Sheria hata kama zingekuwa nzuri kiadi gani lakini si kipaumbele haziwezi kufanya kazi.
 
10 Reactions
Reply
Back
Top Bottom