Tatizo letu ni uwepo wa nafasi ya Ukuu wa Wilaya au ni wale waliomo kwenye hizo nafasi?

denooJ

JF-Expert Member
Mar 31, 2020
18,511
68,141
Salaam,

Nimekuwa nikiona mijadala mingi baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia S. Hassan, kufanya uteuzi wa Wakuu wa Wilaya siku ya Jumamosi, tarehe, 19.06.2021.

Kabla wengi walikuwa wakilaumu uwepo wa hicho cheo cha Ukuu wa Wilaya kama kitu kilichopitwa na wakati kwani kimekuwepo toka enzi za ukoloni.

Lakini kinachonishangaza naona wengi sasa wameanza kujadili aina ya watu waliopata teuzi kwenye hizo nafasi kama wao ndio tatizo kutokana na historia zao za elimu, uwajibikaji, n.k. na kusahau hitaji letu la msingi.

Hivyo nimekuwa nikijiuliza; hivi tatizo letu ni ukuu wa wilaya kama nafasi? au ni wakina nani waliopo kwenye hiyo nafasi?

Najiuliza hivi ili nijue ni kipi hasa tunachokihitaji, inawezekana tunataka kitu kiondolewe kumbe kinaweza kutufaa hata sisi wengine mbele ya safari kama tukibahatika kuwa miongoni mwa wateuliwa.
 
Vyote ni tatizo kwa sasa,ila uwepo wa hizo nafasi ni tatizo kubwa,na hizi nafasi kutokuwa na maana(kama ambavyo tumekuwa tukidai tangu zamani),kumethibitishwa na aina ya watu wanaoendelea kuteuliwa kushika hizi nafasi.
Hizi nafasi,huko nyuma wakati zinawekwa watu wenye taaluma maalum kama wanajeshi,wahandisi,madokta,au watu wenye mchango mkubwa kwenye jamii kama alivyokuwa Betty Mkwasa,zilikuwa zinaleta umaana kidogo.
Sasa unateua mtu kama Nick wa pili,almasi Nyangasa,watu hawajawahi hata kuongoza kijiji,au taasisi yoyote maishani mwao,unataka wakawe viongozi Wilayani!wakaonyeshe mfano gani?na hatuwasemi kwa vile ni vijana tu,wapo watu wengine wa hovyo tu,Binilith Mahenge,alikuwa Recturer DIT,akawa Mbunge,akawa RC,lakini alikuwa mtupu kabisa,hakuna mchango alioleta,Anthony Mavunde,alikuwa waziri Awamu iliyopita,baada ya kuwa waziri,hakutaka kabisa kukutana na vijana kwenye jimbo lake,mpaka alipotumbuliwa,
Hizi nafasi,Mama amechemka,anaongoza kishikaji,kwa viongozi hawa hii nchi hata usalama wake upo mashakani,maana kudukua,hawa viongozi ni rahisi
 
Vyote ni tatizo kwa sasa,ila uwepo wa hizo nafasi ni tatizo kubwa,na hizi nafasi kutokuwa na maana(kama ambavyo tumekuwa tukidai tangu zamani),kumethibitishwa na aina ya watu wanaoendelea kuteuliwa kushika hizi nafasi.
Hizi nafasi,huko nyuma wakati zinawekwa watu wenye taaluma maalum kama wanajeshi,wahandisi,madokta,au watu wenye mchango mkubwa kwenye jamii kama alivyokuwa Betty Mkwasa,zilikuwa zinaleta umaana kidogo.
Sasa unateua mtu kama Nick wa pili,almasi Nyangasa,watu hawajawahi hata kuongoza kijiji,au taasisi yoyote maishani mwao,unataka wakawe viongozi Wilayani!wakaonyeshe mfano gani?na hatuwasemi kwa vile ni vijana tu,wapo watu wengine wa hovyo tu,Binilith Mahenge,alikuwa Recturer DIT,akawa Mbunge,akawa RC,lakini alikuwa mtupu kabisa,hakuna mchango alioleta,Anthony Mavunde,alikuwa waziri Awamu iliyopita,baada ya kuwa waziri,hakutaka kabisa kukutana na vijana kwenye jimbo lake,mpaka alipotumbuliwa,
Hizi nafasi,Mama amechemka,anaongoza kishikaji,kwa viongozi hawa hii nchi hata usalama wake upo mashakani,maana kudukua,hawa viongozi ni rahisi
Umemaliza.

Vyeo vya hisani na sandakarawe ndani ya karne ya 21 kwa nchi ya watu 60M vimepitwa na wakati.

Vinajenga taifa la kinafiki sana.
 
Back
Top Bottom