Tatizo letu ni moja, nalo ni mgawanyo mbovu wa rasilimali za taifa

Tutor B

JF-Expert Member
Jun 11, 2011
9,025
6,554
Watanzania tuko hivi kwa sababu zifuatazo:-
Tulielezwa tangu uhuru kwamba maadui zetu ni watatu, ujinga - maradhi na umaskini. Hivi inakuwaje miaka zaidi ya 50 watu zaidi ya milioni hamsini tunapambana na maadui watatu wanatushinda? Na badala yake wanaibuka maadui wengine mara hoo mafisadi, mara wasiojulikana?

Kama taifa tujitathmini na tuanze mapambano ya pamoja; tuache tofauti zetu za kidini, kisiasa na kikabila / kikanda. Tujue moja tu ambalo linatuponza; tatizo letu moja ni hili ...

"Tatizo sio umaskini, bali ni mgawanyo mbovu wa rasilimali za taifa"

Leo hii utasikia mara hoo kingozi fulani alijilimbikizia mali na sasa zinapigwa mnada. Jambo la kujiuliza ni hili ... wakati anajilimbikizia mali hizo taasisi / vyombo husika vya kuzuia mtu asijilimbikizie mali vilikuwa wapi?

Au ni mpango mzima wa kujipatia kazi za kufanya kila baada ya kipindi fulani?

Tujitafakari upya!
 
Siasa uwanja wa mafisi mkuu..
Mwengine kila siku anakaza shingo.....ooh tumeibiwa sna hii nchi..wakati yeye mwenyewe alikuwa ndani ya mfumo wa hao wezi.

Shithole kantriizi ni headache!
 
This is Africa...viongozi wengi wapo kwajili ya matumbo yao..usiamini mwanasiasa.
 
Unamaanisha keki ya taifa haigawanywi kwa usawa?
Tuko pamoja ... iweje mtu anamiliki mabilioni wakati kuna mwingine anahangaikia mlo mmoja na anaukosa.

Iweje mtu anamiliki magari zaidi ya kumi .. mwingine hata baiskeli hana?

Iweje mtu anamiliki maghorofa mjini (tena wengine wameyajenga nje ya nchi) wakati mwingine hata hela kulipia chumba kimoja cha kujihifadhi hana?

Alafu hawa wanaomiliki mali za hatari ndo wanasimama kwenye majukwaa kuwalaghai wenzao eti nchii hii ni yetu sote ...

Alafu hawa wasiokuwa na kitu wanashangilia tu! TUTAFIKA KWELI?
 
Tuko pamoja ... iweje mtu anamiliki mabilioni wakati kuna mwingine anahangaikia mlo mmoja na anaukosa.

Iweje mtu anamiliki magari zaidi ya kumi .. mwingine hata baiskeli hana?

Iweje mtu anamiliki maghorofa mjini (tena wengine wameyajenga nje ya nchi) wakati mwingine hata hela kulipia chumba kimoja cha kujihifadhi hana?

Alafu hawa wanaomiliki mali za hatari ndo wanasimama kwenye majukwaa kuwalaghai wenzao eti nchii hii ni yetu sote ...

Alafu hawa wasiokuwa na kitu wanashangilia tu! TUTAFIKA KWELI?
Mkuu hapo ndipo umuhimu wa kumpiga vita kwanza adui ujinga ulihitajika, tatizo ni kwamba the majority are illiterates, wao hushangilia tu na kufuata mkumbo wa wasiyoyajua toka kwa tabaka la watawala ilhali hali zao kimaisha ni za kusikitisha!
 
Mkuu hapo ndipo umuhimu wa kumpiga vita kwanza adui ujinga ulihitajika, tatizo ni kwamba the majority are illiterates, wao hushangilia tu na kufuata mkumbo wa wasiyoyajua toka kwa tabaka la watawala ilhali hali zao kimaisha ni za kusikitisha!
Mkuu hapo ndipo umuhimu wa kumpiga vita kwanza adui ujinga ulihitajika, tatizo ni kwamba the majority are illiterates, wao hushangilia tu na kufuata mkumbo wa wasiyoyajua toka kwa tabaka la watawala ilhali hali zao kimaisha ni za kusikitisha!
Nimekuelewa vyema! majority hawajitambui kabisa!
 
Jiamini mwenyewe pigania maisha yako na generation yako.
Sikiliza mkuu ...
Mimi ni mimi kama mimi na wanaonizunguka ni familia yangu (mke wangu na watoto wangu)

Baada ya hapo ni wale majirani zangu tunaohishi wote pale kwenye mtaa...

Baada ya hapo ni wale tunashirikiana kwenye mambo ya kijamii kwenye kata ...

Baada ya hapo ni wale wa jimboni kwangu hadi taifa.

Sasa unaongelea generation ipi wakati hata kwenye familia bado kuna mizizi ya wale wasiojitambua? Wanaimba nyimbo za wale wanaotusababishia matatizo kwenye jamii?

Nijuavyo mimi ukiwa na jirani mwenye dhiki ni dhahili hata wewe unadhiki tu.

Angali dhiki za wenzetu nchi jirani zinavyo tusababishia wakimbizi mikoa ya pembezoni.
 
Back
Top Bottom