Tatizo letu kubwa lipo kwenye mfumo wetu wa Elimu ndiyo maana tunazalisha viongozi dhaifu

JERUSALEMU

JF-Expert Member
Sep 19, 2012
3,106
3,523
Habari wana jamvi,

Nimefuatilia kwa muda mrefu jinsi mambo yanavyo endelea nchini mwetu katika nyanja mbalimbali, nimegundua kuwa tatizo ni kubwa mno hasa kwasababu linaanzia kwenye mfumo wetu wa Elimu. Mwishoni nitajitahidi kufafanua.

Kifupi ni kwamba waliotakiwa kuongozwa ndio wanatuongoza. Wasio na maarifa wala ubunifu ndio waliopewa nafasi kusimamia maendeleo ya nchi yetu.

Watu dhaifu kwenye bongo zao na pengine kimwili ndio wamepewa dhamana ya kutupeleka Nchi ya ahadi. Tazama mfano wa hili nilisemalo. Bunge letu lina taratibu, kanuni na sheria nzuri tu kwa kiwango chake, lakini linasimamiwa na mtu dhaifu kabisa kiakili, kimwili na kiroho.

Matokeo yake tumetengeneza bunge dhaifu na kituko zaidi Duniani. Halistahili kuitwa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ni bunge la Ndugai, mtu dhaifu kabisa kupata kutokea.

Tuna wabunge lukuki wanao ona fahari kumtetea Magufuli kuliko kutetea Nchi yao kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Tumefikishwa mahali ambapo serikali inanunua dawa za masangoma kwa fedha za umma na Bunge limebung'aa tu 'hawakei' ujinga huo. Baadae watawalazimisha wataalamu wa afya wakazigawe kwa wagonjwa? Doctor ataandikaje kwenye cheti cha mgonjwa? Au speaker wa Bunge na Kabudi watazigawa kwa wagonjwa? Kwa niaba ya aliyezinunua?

Hamuoni tunaongozwa na tulio takiwa kuwaongoza?

Tumefika mahali Polisi na pengine vingine vya ulinzi na usalama wanaona fahari kuilinda na kuitetea CCM badala ya Nchi yao! Tatizo hapa siyo watu ni mfumo wa Elimu.

Tumefika mahali watanzani wanaona fahari kumshabikia kiongozi dhaifu ilimradi analipwa fedha.

Naambiwa kuna chama kimeajiri vijana ili kukitetea mitandaoni kwa kuwalipa shs elfu saba. Alas! Graduate kabisa anakubali ujinga huo.

Kiongozi mkubwa ana vunja Katiba mara elfu moja na moja sisi tupo tu tunamshangilia. Kiongozi anatumia ofisi ya umma kujinufaisha bado hatujui kuwa hilo ni kosa.

Kuna haja ya kuufanyia ovehaul mfumo wetu wa Elimu ili wanao graduate wajitambue!
 
Mara zote huwa napingana na wanaosema tatizo la nchi yetu liko kwenye elimu. Tatizo letu haliko kwenye elimu bali liko kwenye sheria. Sheria ndo inasimamia mfumo wa elimu na masuala yote ya nchi.
 
Ndugai yu hoi bini taabani kiakili, kimwili na kiroho. Mimi huwa najiuliza amefikaje pale?
 
Mara zote huwa na pingana na wanaosema tatizo la nchi yetu liko kwenye elimu. Tatizo letu liko kwenye sheria. Sheria ndo inasimamia mfumo wa elimu na masuala yote ya nchi.
Wenye Elimu dhaifu ndio wanao tunga sheria. Sheria pia huhitaji tafsri , asiye na Elimu thabiti ni sawa na maamuma tu.
 
Njaa ni kitu kibaya sana, mtu una graduate hakuna ajira, hakuna mazingira ya biashara mtaani kugumu, njaa ni kali, kwanini nisiwashobokee ccm nipate kula,


nifee njaa kisa uzalendo ambao hata wenye nchi hawana? Hapa ni mwendo wa tumbo kwanza,
 
Limoja limekariri matest tube basi linaona limemaliza kila kitu wkt hamna kitu kichwani....
 
Katiba ndo maana kina lissu walkua wanpgania katiba tunawaona hawafai ooohh xx tntaka maendeleo htutak katiba sasa inchi ilpofika inaongozwa na mhimili uliojinchimbia chini katiba inampa mamlka yote ayo uwez kmshtaki kwaio tutulie hvyhvy aikanyage anvytaka maana kina lissu na wengne walioona katiba Ina umuhimu kipindi kile tliwatukana Sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kosa kubwa aliliotufanyia nyerere ni kutowashirikisha wananchi juu ya mfumo sahihi wa kuendesha nchi yeye aliukopi na kupaste toka kwa swaiba wake dikteta Mao na kutuletea,.Yafaa sasa tutengeneze mfumo sahihi wa kizazi cha sasa na sio kuongozwa na katiba mfu iliyokufa ya 1977
 
Wenye Elimu dhaifu ndio wanao tunga sheria. Sheria pia huhitaji tafsri , asiye na Elimu thabiti ni sawa na maamuma tu.
Sheria zimekuwepo hata kabla ya mfumo rasmi wa elimu. Babu zetu walikuwa na sheria japo hawakuwa na vyuo vikuu.

Shida ilianzia kwenye sheria za mzungu. Ndiyo maana mtu akifanya tofauti na mawazo ya mzungu waliotawaliwa kifikra na mzungu wanamshambulia kuwa kakosea.
 
Back
Top Bottom