Tatizo la vyama vya upinzani kushindwa kulinda kura zao nini suluhisho lake?

FUTURE HUNTER

JF-Expert Member
Apr 30, 2018
2,022
2,591
Wanajukwaa poleni na majukumu.
Mimi niende moja kwa moja kwenye mada yangu hapo juu.Tangu nianze kukua na kuijua siasa imekuwa bahati nzuri nimekuta vyama vingi ndio vipo hot kweli kweli hivyo nimeona chaguzi kadhaa namna hali inavyokuwa haswa baada ya kupiga kura.
Kumekuwa na wimbi kubwa sana la vyama vya upinzani kulalamika kudhurumiwa matokeo yao halisi(haswa wabunge na madiwani) katika majimbo mbali mbali.
Mfano nakumbuka mwaka 2015 sehemu nyingi sana akishinda mpinzani ilikuwa ni kwa utata sana mpaka atangazwe mshindi tofauti na pale anaposhinda mtu wa chama dola.
Njoo kwa haya tuliyoyaona k/ndoni ya box la kura kutoka nje ya kituo na kurudishwa baadae,kunyimwa barua za wasimamizi, au kukataa kupokea fomu za wagombea toka upinzani.
Lakini juu ya hili mara nyingi vyama vya upinzani huhimiza raia kujitokeza kwa wingi kuwapigia kura kipindi cha chaguzi lakini wakishapiga kura naona kabisa vyama havina namna ya kuzilinda kura hizi ili haki itendeke.Wananchi wanabaki wanalishwa matumaini feki tu.(Nakumbuka huyu edo 2015 alisema pigeni kura kwa wingi kuhusu kuiba ondoeni shaka) lakini mwisho wa siku bado vyama vinaangukia pua.
Kwa kuhitimisha,Je imekosekana njia sahihi kutoka vyama pinzani kulinda kura za wanyonge baada ya kutumbukizwa sandukuni?.Wenzetu nchi zingine wanafanyaje kuepuka hili?.
Maana naona kabisa kama haina haja ya kupiga kura maana inaonekana hata ikipigwa haiwezi amua nani mshindi isipokuwa chama kaisali.
Karibuni Kwa michango.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nguvu ya mwenyekiti wa ccm kama amiri jeshi mkuu ndio hasa sababu ya yote hayo. Tume ya uchaguzi inalipa fadhila kwa mamlaka ya uteuzi, vyombo vya dola vinajiona vina wajibu wa kuhakikisha mgombea wa chama cha rais anatangazwa mshindi hata kwa kumwaga damu. Kwahiyo wapinzani kulinda kura ni kama kutangaza vita na tume ya uchaguzi na vyombo vya dola. Na mpinzani atakayekilinda kura ajiandae kupata kilema cha maisha, kupoteza uhai, kubambikiziwa kesi, au kuharibiwa shughuli yake.
 
Nguvu ya mwenyekiti wa ccm kama amiri jeshi mkuu ndio hasa sababu ya yote hayo. Tume ya uchaguzi inalipa fadhila kwa mamlaka ya uteuzi, vyombo vya dola vinajiona vina wajibu wa kuhakikisha mgombea wa chama cha rais anatangazwa mshindi hata kwa kumwaga damu. Kwahiyo wapinzani kulinda kura ni kama kutangaza vita na tume ya uchaguzi na vyombo vya dola. Na mpinzani atakayekilinda kura ajiandae kupata kilema cha maisha, kupoteza uhai, kubambikiziwa kesi, au kuharibiwa shughuli yake.
Kwa hiyo hakuna namna ya kuepukana na hili kabisa?. Maana kubadili namna ya tume ya uchaguzi inavyoteuliwa napo ni mtihani mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nguvu ya mwenyekiti wa ccm kama amiri jeshi mkuu ndio hasa sababu ya yote hayo. Tume ya uchaguzi inalipa fadhila kwa mamlaka ya uteuzi, vyombo vya dola vinajiona vina wajibu wa kuhakikisha mgombea wa chama cha rais anatangazwa mshindi hata kwa kumwaga damu. Kwahiyo wapinzani kulinda kura ni kama kutangaza vita na tume ya uchaguzi na vyombo vya dola. Na mpinzani atakayekilinda kura ajiandae kupata kilema cha maisha, kupoteza uhai, kubambikiziwa kesi, au kuharibiwa shughuli yake.
Nini ushauri wako mkuu tindo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom