meddie
JF-Expert Member
- Oct 21, 2010
- 434
- 125
Leo asubuhi Badra masoud akihojiwa channel ten amesema tatizo kubwa ni ukosefu wa fedha kwa ajili ya kuwekeza ktk vyanzo mbadala vya kuzalisha umeme nchini.
kwa upanda wake Jk akihojiwa bbc amesema tatizo ni ukame na kwamba yeye hanauwezo wa kumuomba mungu alete mvua, hasa wakati huu baada ya kuondokewa na msaada wake sheik yakhaya!
Kwa tofauti hii ya maelezo na mtazamo kuhusiana na chanzo cha tatizo la umeme na kwa jk kuamua kutembea nje kipindi taifa lipo gizani, inaashilia hasivyojali na hasivyo kuwa na jibu kamili wala mkakati wa kumaliza tatizo la ukosefu wa umeme nchinii. hii nikusema hatakama serikali itapewa mwaka mzima acha week tatu, hakutakuwa na majibu ya utatuzi wa jambo hili
lkn jambo jingine lakushangaza ni kuona ktk kipindi hiki ambapo taifa limogizani, hali ya maisha ikipanda, raisi wetu akichanja mbuga kama hana akili mzuri. Majeshi yetu yapo kimywa wakiendelea kuponda hela za walipakodi!
Kama kweli jeshi bado ni la wananchi watz nategemea wasikae kimya ktk hali kama hii. Natumai wote tunakumbuka kauli iliyotolewa wakati wa uchaguzi na mkuu wa majeshi kupitia mnadhimu wake mkuu Luteni Jenerali Abdulrahman Shimbo ya kuvitaka vyama vya siasa kukubali matokeo baada ya uchaguzi mkuu wa Oktoba na kuonya kwamba vyombo vya ulinzi na usalama vimejiandaa kikamilifu kupambana na yeyote atakayejaribu kuyakataa matokeo.
Kama kauli hii ilitokana na uzalendo na upendo kwa TZ na siyo unafiki na kumkingia kifua JK na kuwatisha wananchi na vyama vilivyokuwa vikishiriki uchaguzi. basi wakikae kimywa wakati huu, bali watoe tamko pia!!
vinginevyo shiit kwao!!