Tatizo la umeme ndilo litakuwa janga kuu la kura za CCM 2025. Mabadiliko ya haraka ya sekta hii ni muhimu

Dr Akili

JF-Expert Member
Aug 21, 2011
4,953
4,326
CCM imekamilisha kupanga timu ya kusaka kura kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2025. Mabadiliko ya watendaji serikalini yanatarajiwa kufanyika hivi punde kwa lengo hilo hilo la kuvutia kura za wananchi.

Katika harakati zao hizo ni vyema wakazingatia ushauri ufuatao:
- Janga namba moja kuu litakalowakosesha kura nyingi ni hili tatizo la umeme. Linazidi kujenga chuki ya wananchi kila siku tatizo hili linapoendelea na hivyo kupeperusha kura. Linabidi limalizwe haraka. Angalao wananchi wangependa kuona kwamba mabadiliko ya watendaji serikalini yanayotarajiwa yanafanyika kwenye sekta/ wizara hii. Waliopo sasa hata kama ni wazuri lakini wananchi walishapoteza imani nao. Mambo mengine huwa ni ya kisaikolojia. Jitihada zinatakiwa si tu kufanyika bali kuonekana zinafanyika.

- Janga kuu la pili ni kupanda kwa bei ya mafuta (gasoline). Ni kweli kwamba jambo hili linatokana na vita ya Ukraine ambayo inaweza kuendelea kwa miaka kadhaa. Hata hivyo jambo hili lisipodhibitiwa haraka litapeperusha kura nyingi za wananchi. Imeshuhudiwa hata huko ulaya, jambo hili limesababisha mfululizo wa mabadiliko ya mawaziri wakuu hasa huko Uingereza. Mbinu mbali mbali zinaweza kutumika, pamoja na kutumia shirika letu la TPDC kununua mafuta hayo moja kwa moja toka Uarabuni au Urusi badala ya makampuni ya binafsi kama tunavyofanya sasa. Tusiogope kununua mafuta haya toka Russia ambako bei yake ni nafuu sana. China na India wanafanya hivyo. Hata ulaya magharibi wanaendelea kununua mafuta haya na gesi toka Urusi. Sisi kitu gani tunakiogopa?

- Jambo kuu la tatu ni mfumuko mkubwa wa bei hasa wa chakula. Wananchi haiwaingii kichwani wakiona chakula kikipelekwa Kenya na Somali wakati wao wakiwa hawana chakula cha kutosha. Kwani bei nzuri kwa wakulima wetu haiwezi kupatikana bila vyakula hivyo kupelekwa Kenya na Somali?

- Hili la wananchi kudhani ufisadi na rushwa imeongezeka halina shida kubwa.
 
tatizo la mgao wa umeme lina sababishwa na ukame pamoja na uchakavu wa mitambo, tusitake kumsulubu waziri kwa hili.

Vinginevyo kama sio ukame na uchakavu wa mitambo basi kuna watendaji mdani ya shirika ndio wanao ihujumu serikali kwa kwa kutengeneza matatizo na kukatakata umeme.

waziri amejitahidi sana kusafisha vidudu mtu ndani ya shirika lakini bado wamo ndio wanao leta kero kwa wananchi.
 
tatizo la mgao wa umeme lina sababishwa na ukame pamoja na uchakavu wa mitambo, tusitake kumsulubu waziri kwa hili.

Vinginevyo kama sio ukame na uchakavu wa mitambo basi kuna watendaji mdani ya shirika ndio wanao ihujumu serikali kwa kwa kutengeneza matatizo na kukatakata umeme.

waziri amejitahidi sana kusafisha vidudu mtu ndani ya shirika lakini bado wamo ndio wanao leta kero kwa wananchi.
Huyo waziri alishawaudhi sana wananchi kwa kauli zake za kigeugeu kuhusiana na tatizo la umeme lililojitokeza mara tu baada ya yeye kuchukua nafasi hiyo. Kwa takribani miaka 5 mfululizo wananchi walikuwa wamelisahau hadi alipoingia waziri huyu. Kama ni ukame hata huko nyuma ulikuwa unatokea lakini umeme ulikuwa haukatiki. Kama ni mitambo na transmission systems, hata huko nyuma ilikuwa inaharibika lakini ilikuwa ikitengenezwa bila umeme kukatika katika. Sasa tumeambiwa hii katika katika itaendelea hadi 2025.

Kwani kumhamishia wizara nyingine ni kumsulubu? Waziri wa nishati ana tofauti gani mawaziri wengine? Akipewa kwa mfano wizara ya michezo na utamaduni atakuwa amepungukiwa kitu gani? Baba yake atakasirika na ulimi wake utateleza tena? Kwanini chama kinyimwe kura 2025 kwa sababu ya kitu kama hiki? Bila shaka wewe ni kati ya wale wasiopenda chama hiki kishinde uchaguzi wa 2025, utakuwa unatokea kule upinzani.
 
Imenichukua miaka miwili ya machozi jasho na damu kukamilisha project yangu ambayo ilihitaji umeme wa njia tatu miezi miwili imepita ndo nimemaliza kufunga system yote lakini kwa masikitiko makubwa mgao wa umeme ni mkali kuliko maelezo na hata ukija unakuja single.Asikuambie mtu maumivu ninayopitia ni Makubwa sana hela yote imekata wafanyakazi wote sita amebaki mmoja mfukoni nina buku mbili tuu, natakiwa kutuma hela home watoto wapate hata chochote sina mama yao akipiga simu machozi yanatoka jaman mlio kalibu na hawa viongozi waanbieni hali ni mbaya kifo kipo mlangoni kwetu.Naomba niishie hapo maumivu no makali sana sjw nini kitatokea ee Mungu niokoe
 
CCM imekamilisha kupanga timu ya kusaka kura kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2025. Mabadiliko ya watendaji serikalini yanatarajiwa kufanyika hivi punde kwa lengo hilo hilo la kuvutia kura za wananchi.

Katika harakati zao hizo ni vyema wakazingatia ushauri ufuatao:
- Janga namba moja kuu litakalowakosesha kura nyingi ni hili tatizo la umeme. Linazidi kujenga chuki ya wananchi kila siku tatizo hili linapoendelea na hivyo kupeperusha kura. Linabidi limalizwe haraka. Angalao wananchi wangependa kuona kwamba mabadiliko ya watendaji serikalini yanayotarajiwa yanafanyika kwenye sekta/ wizara hii. Waliopo sasa hata kama ni wazuri lakini wananchi walishapoteza imani nao. Mambo mengine huwa ni ya kisaikolojia. Jitihada zinatakiwa si tu kufanyika bali kuonekana zinafanyika.

- Janga kuu la pili ni kupanda kwa bei ya mafuta (gasoline). Ni kweli kwamba jambo hili linatokana na vita ya Ukraine ambayo inaweza kuendelea kwa miaka kadhaa. Hata hivyo jambo hili lisipodhibitiwa haraka litapeperusha kura nyingi za wananchi. Imeshuhudiwa hata huko ulaya, jambo hili limesababisha mfululizo wa mabadiliko ya mawaziri wakuu hasa huko Uingereza. Mbinu mbali mbali zinaweza kutumika, pamoja na kutumia shirika letu la TPDC kununua mafuta hayo moja kwa moja toka Uarabuni au Urusi badala ya makampuni ya binafsi kama tunavyofanya sasa. Tusiogope kununua mafuta haya toka Russia ambako bei yake ni nafuu sana. China na India wanafanya hivyo. Hata ulaya magharibi wanaendelea kununua mafuta haya na gesi toka Urusi. Sisi kitu gani tunakiogopa?

- Jambo kuu la tatu ni mfumuko mkubwa wa bei hasa wa chakula. Wananchi haiwaingii kichwani wakiona chakula kikipelekwa Kenya na Somali wakati wao wakiwa hawana chakula cha kutosha. Kwani bei nzuri kwa wakulima wetu haiwezi kupatikana bila vyakula hivyo kupelekwa Kenya na Somali?

- Hili la wananchi kudhani ufisadi na rushwa imeongezeka halina shida kubwa.
CCM haihitaji kura ya mtu, tayari mama ameshinda kwa kishindo wanajiandaa kumapisha.
 
Nikimnukuu wakili msomi aliyesimamishwa kufanya kazi Shangazi Fatma Karume( mzanzibar) alisikika akiandika wakati ule Mwl Bashiry Ally amenena kuhusu sifa za anaupiga mwingi. Alisema Bashir " Ni kama anachochea moto petroli wakati huu ambao Approval rating ya mkubwa ni very record low ever happened in the history of URT sababu ya matatizo ya maji na umeme. Mwisho wa kunukuu. Kwamba kukubalika kwa ccm baada ya maji na umeme kuwa washida kumeshuka sana kuwahi kutojea huko nyuma.

Kama wakili msomi, mzanzibar kaliona hilo mimi nani nikanushe. Watu wamechoka swna na haya mambo ya umeme na kama kweli wanaongeza bei ya unit kwenda 550. Hali itazidi kuwa isiyo ya furaha. Tutashuhudia ya Kenya ya very low voters turnout.
 
..matatizo ya umeme na maji hayatakuwepo 2025.

..matatizo sugu yatakuwa ukosefu wa ajira, mfumuko wa bei, na hali ngumu ya maisha haswa wakulima
 
Imenichukua miaka miwili ya machozi jasho na damu kukamilisha project yangu ambayo ilihitaji umeme wa njia tatu miezi miwili imepita ndo nimemaliza kufunga system yote lakini kwa masikitiko makubwa mgao wa umeme ni mkali kuliko maelezo na hata ukija unakuja single.Asikuambie mtu maumivu ninayopitia ni Makubwa sana hela yote imekata wafanyakazi wote sita amebaki mmoja mfukoni nina buku mbili tuu, natakiwa kutuma hela home watoto wapate hata chochote sina mama yao akipiga simu machozi yanatoka jaman mlio kalibu na hawa viongozi waanbieni hali ni mbaya kifo kipo mlangoni kwetu.Naomba niishie hapo maumivu no makali sana sjw nini kitatokea ee Mungu niokoe
Sasa kwa hayo yaliyokupata, wewe na familia yako mtawapa kweli kura zenu kama hali hii itaendelea?
 
..matatizo ya umeme na maji hayatakuwepo 2025.

..matatizo sugu yatakuwa ukosefu wa ajira, mfumuko wa bei, na hali ngumu ya maisha haswa wakulima
Hata kama matatizo haya ya umeme watakuwa wameyatatua ifikapo mwaka 2024 kama walivyoahidi, watakuwa tayari wameshapoteza kura nyingi.
 
Hata kama matatizo haya ya umeme watakuwa wameyatatua ifikapo mwaka 2024 kama walivyoahidi, watakuwa tayari wameshapoteza kura nyingi.

..kikwazo kikubwa ni fedha na resources walizonazo.

..vyombo vyote vya habari vinawatangaza wao.

..wasanii asilimia 98% wako upande wa watawala.

..wasimamizi wa uchaguzi kwa maana ya wakurugenzi ni makada wao.

..jeshi la Polisi liko upande wao kuwalinda wakati wakifanya mambo yao.

..pia Watanzania hawana utamaduni wa kuonyesha hisia zao, au kushinikiza mabadiliko, kupitia sanduku la kura.

..hata wakiharibu kiasi gani, ni vigumu kuwashinda kutokana na advantages walizo nazo.
 
Siyo suala la umeme peke yake ndugu mleta mada. Hakuna Jambo ambalo ccm imefanikiwa .

Wanachojivunia ni tume kutokuwa huru na vyombo vya dola kuwa sehemu ya hujuma ya uchaguzi
 
Hv unadhan wanategemea box la kura????
Huyo waziri alishawaudhi sana wananchi kwa kauli zake za kigeugeu kuhusiana na tatizo la umeme lililojitokeza mara tu baada ya yeye kuchukua nafasi hiyo. Kwa takribani miaka 5 mfululizo wananchi walikuwa wamelisahau hadi alipoingia waziri huyu. Kama ni ukame hata huko nyuma ulikuwa unatokea lakini umeme ulikuwa haukatiki. Kama ni mitambo na transmission systems, hata huko nyuma ilikuwa inaharibika lakini ilikuwa ikitengenezwa bila umeme kukatika katika. Sasa tumeambiwa hii katika katika itaendelea hadi 2025.

Kwani kumhamishia wizara nyingine ni kumsulubu? Waziri wa nishati ana tofauti gani mawaziri wengine? Akipewa kwa mfano wizara ya michezo na utamaduni atakuwa amepungukiwa kitu gani? Baba yake atakasirika na ulimi wake utateleza tena? Kwanini chama kinyimwe kura 2025 kwa sababu ya kitu kama hiki? Bila shaka wewe ni kati ya wale wasiopenda chama hiki kishinde uchaguzi wa 2025, utakuwa unatokea kule upinzani.
 
kikwazo kikubwa ni fedha na resources walizonazo.
Fedha siyo kikwazo kwani serikali ina uwezo wa kukopa kiasi cho chote inachokitaka mahali po pote na wakati wo wote. Ndiyo uzuri wa serikali ya sasa ukilinganisha na zote zilizopita. Big up kwa hili
 
Fedha siyo kikwazo kwani serikali ina uwezo wa kukopa kiasi cho chote inachokitaka mahali po pote na wakati wo wote. Ndiyo uzuri wa serikali ya sasa ukilinganisha na zote zilizopita. Big up kwa hili

..uko sahihi kwa uliyoyasema kuhusu serikali.

..lakini mimi nilikuwa nalinganisha uwezo wa kifedha na rasilimali wa Ccm ukilinganisha na washindani wao.
 
..uko sahihi kwa uliyoyasema kuhusu serikali.

..lakini mimi nilikuwa nalinganisha uwezo wa kifedha na rasilimali wa Ccm ukilinganisha na washindani wao.
CCM ni chama tawala na ndiyo yenye serikali. Maamuzi yanafanywa na ccm, hela za utekelezaji na watekelezaji wa maamuzi hayo ni serikali. Hivyo huwezi kuilinganisha ccm na hao washindani wao. Ili waendelee kuwa chama tawala, waamuzi ni wananchi hapo kwenye kura za 2025. Tunachoitahadhalisha ccm ni kuwa ikiendelea kuwazengua wananchi kwa kuwakatia katia umeme watapigwa chini 2025. Tegemeo la vyama shindani ni kuwa ccm iendelee kuwazengua wananchi.
 
CCM ni chama tawala na ndiyo yenye serikali. Maamuzi yanafanywa na ccm, hela za utekelezaji na watekelezaji wa maamuzi hayo ni serikali. Hivyo huwezi kuilinganisha ccm na hao washindani wao. Ili waendelee kuwa chama tawala, waamuzi ni wananchi hapo kwenye kura za 2025. Tunachoitahadhalisha ccm ni kuwa ikiendelea kuwazengua wananchi kwa kuwakatia katia umeme watapigwa chini 2025. Tegemeo la vyama shindani ni kuwa ccm iendelee kuwazengua wananchi.

..uko sahihi kwa upande wa serikali.

..lakini mimi hoja yangu iko upande wa vyama vya siasa.

..Na ninajaribu kuangazia uwezo wa KIFEDHA wa Ccm ukilinganisha na washindani wake wakati wa kampeni.

..tofauti kati Ccm na mshindani wake wa karibu ni kubwa kupita kiasi.

..kwenye nchi za wenzetu, hata hapo Kenya, kampeni za wagombea wakuu wawili zilikuwa zinalingana au zinakaribiana kiuwezo.

..Kampeni zilikuwa hazitofautiani sana kifedha, rasilimali, matangazo, kutangazwa ktk vyombo vya habari, etc etc.

..Ndoto yangu ni siku moja Tanzania iwe na uchaguzi wenye USHINDANI wa kweli. Labda hata matokeo yakaribiane tuwe na uchaguzi wa marudio[ sheria zetu haziruhusu.]
 
..uko sahihi kwa upande wa serikali.

..lakini mimi hoja yangu iko upande wa vyama vya siasa.

..Na ninajaribu kuangazia uwezo wa KIFEDHA wa Ccm ukilinganisha na washindani wake wakati wa kampeni.

..tofauti kati Ccm na mshindani wake wa karibu ni kubwa kupita kiasi.

..kwenye nchi za wenzetu, hata hapo Kenya, kampeni za wagombea wakuu wawili zilikuwa zinalingana au zinakaribiana kiuwezo.

..Kampeni zilikuwa hazitofautiani sana kifedha, rasilimali, matangazo, kutangazwa ktk vyombo vya habari, etc etc.

..Ndoto yangu ni siku moja Tanzania iwe na uchaguzi wenye USHINDANI wa kweli. Labda hata matokeo yakaribiane tuwe na uchaguzi wa marudio[ sheria zetu haziruhusu.]
Hiyo itatokea tu pale ccm itakapokosa mwelekeo na wananchi kuipiga chini kama ilivyo tokea kwa KANU huko Kenya na Zambia. Tatizo CCM wako makini na utasubiri zaidi ya miaka 100 jambo hili liwapate, kama ilivyo huko China na Afrika kusini. Ni mahodari wa kufunga goli hata kama ni kwa mikono.
 
Back
Top Bottom