Tatizo la ujio wa Lowassa CHADEMA ni chama kubadilika kufiti ujio wa Lowasa badala ya Lowasa kubadilika kufiti misingi

Kalamu Huru

Member
Dec 2, 2017
11
8
Wasalaam,

Kalamu huru imevutika kuandika kidogo kuhusu mjadala wa muda mrefu wa Lowasa kuhamia CHADEMA.


Ikumbukwe kuwa, ni haki ya kikatiba kila mwananchi kujiunga au kuachana na chama chochote cha siasa. Hivyo, kuhama chama kwa kwenyewe, sio tatizo.

Kikubwa, tunaamini anajiunga kwa kuwa anakubaliana na misingi, falsafa na itikadi ya chama ajiungacho. Sote twajua hizi sio sababu zilizompeleka Lowasa CHADEMA. Ila sitajikita kwenye hilo leo.

Pamoja na yote hayo, ilipaswa mwenye kuja chamani abadilike kulingana na misingi, falsafa na itikadi ya chama.

Tatizo la ujio wa Lowasa CHADEMA ni chama kubadilika kufiti ujio wa Lowasa badala ya Lowasa kubadilika kufiti misingi, falsafa na itikadi ya chama. Hilo tu.

Ni muhimu sasa kwa chama kutengeneza (nurture and mould) vijana ambao wataweza si tu kuwa wagombea, bali viongozi wa nchi. Hii pokea pokea makapi ya CCM na kuyaamini na kuyapa nafasi nyeti bila hata kuwachunguza kwa kina dhimira zao hakukisaidii chama katika kipindi cha muda mrefu (in the long run). Matokeo yake ndio haya ya watu kuacha nafasi za uwakilishi na kumuunga mkono Rais.

Ni muhimu chama kuukubali ukweli, kuupokea na kufanya jitihada kurekebisha ili tuwe na upinzani wenye afya.

The Quill.
 
Mimi kama mkereketwa wa sera za upinzani leo najitokeza hadharani kuhoji hiki kinachoendelea ndani ya CHADEMA.

Kabla ya ujio wa Edward Lowassa, CHADEMA tulitamba sana kwa kutetea wananchi masikini, siku zote tulitetea wamachinga, mama ntilie, wakulima, na wafugaji. Mitaani CHADEMA tulikuwa na mvuto wa kipekee kwa sababu ya hoja na sera zetu za kuifikirisha serikali.Tulikuwa ukivaa magwanda na kupita nayo mtaani unashangiliwa kila kona.

Mara baada ya Edward Lowasa kujiunga chadema, mambo mengi yamebadilika ndani ya chama. CHADEMA ya leo haina mvuto kwa wananchi kabisa, hata ukivaa magwanda na kupita nayo mtaani unaonekana kama lofa fulani tu.

Kwa nini imekuwa hivi?

1.Ni kwa sababu CHADEMA ya leo si mtetezi wa wanyonge tena. Watu maskini wanabomolewa nyumba zao lakini hutasikia wakiwatetea .

CHADEMA ya leo ni rafiki na mtetezi wa wakwepa kodi, wauza madawa, wala rushwa, majangili na wachawi.

2. Imezuka falsafa mpya ndani ya CHADEMA kuwa chama ni watu, kwa hiyo ili mradi tu wewe ni mtu hata kama ni fisadi, mchawi, mkwepa kodi, muuza madawa ya kulevya na mchawi njoo CHADEMA utapokewa.

Je maadili na miiko ya CHADEMA imeenda wapi?

Kutokana na sababu hizo hapo juu nimeamua kutema nyongo kwa Edward Lowassa aturudishie chama chetu, hii siyo chadema tuliyoizoea
 
Chadema vs Lowasa vs pesa
Kwamaana aliingia wa ajili ya kugombea nafasi ya urasi kwa garama zake sio za chama matokea yake haya tunayoshuhudia sasa
 
Chadema vs Lowasa vs pesa
Kwamaana aliingia wa ajili ya kugombea nafasi ya urasi kwa garama zake sio za chama matokea yake haya tunayoshuhudia sasa
Inasemekana mbowe alikikopesha chama billion 7 kwa ajili ya kampeni, Imekuwaje leo unasema Lowasa alitumia gharama zake?
 
Magufuli alimwambia Spika awashughulikie huko Bungeni alafu wakija huku Uraiani yeye atapambana nao.

Isitoshe mikutano yote ya hadharani alipiga marufuku.

Kumekuwa na uminyaji mkubwa wa Demokrasia na uhuru wa kujieleza haya yote huyaoni Mkuu.
Vyama vya Siasa vipo kisheria tulipoanza mfumo wa vyama vingi inaonekana CCM hawakuwa tayari kuupokea.
 
Ni matokeo gani mabaya ambayo hayakuletwa na dhamira ya rais ya kuua upinzani? Kwani CUF kuna Lowassa? Mbona wamewekwa kitanzi bila sababu kwa maagizo ya juu?
Hebu tuone wapewe haki saw kama ccm hawatalia.
Sisi wapiga kura tunaelewa linofanywa naccm. Wachawi hao dawa yao iko jikoni.
 
Ni matokeo gani mabaya ambayo hayakuletwa na dhamira ya rais ya kuua upinzani? Kwani CUF kuna Lowassa? Mbona wamewekwa kitanzi bila sababu kwa maagizo ya juu?
Hebu tuone wapewe haki saw kama ccm hawatalia.
Sisi wapiga kura tunaelewa linofanywa naccm. Wachawi hao dawa yao iko jikoni.
Wenye akili za kushikiwa hawawezi kuelewa maana ya ulichokiandika zaidi ya walichomezeshwa.
Wananunua wanaoonekana wakisahau chuki dhidi yao ziko mitaani.
 
Ccm mumepambana.sana na Mbowe mkitaka kumfilisi bila sababu. Makampuni mengi ya wahindi yameingia ubia na NHC kumnyanganya Mbowe Bilicanas ilikuwa siasa tu hamna kingine. Mpaka kungoa mazao yake. Hata kama ni baada ya miaka 10 hiyo haki itapatikana. Mzee Mbowendiye aliyejenga ccm. Kwaccm kumharass Mbiwe ni dhambi kubwa.
 
Inasemekana mbowe alikikopesha chama billion 7 kwa ajili ya kampeni, Imekuwaje leo unasema Lowasa alitumia gharama zake?
Mboe hakuanza kukopesha wakati wa lowasa alianza enzi za dr slaa huyu yeye kama unaosema ilisemeka garama zote za uchaguzi juuyake ndo kupitishwa bila kupingwa na chama kua mgombea wake wa urasi 2015 na 2020 kwa matarajio yajayo.
 
Magufuli alimwambia Spika awashughulikie huko Bungeni alafu wakija huku Uraiani yeye atapambana nao.

Isitoshe mikutano yote ya hadharani alipiga marufuku.

Kumekuwa na uminyaji mkubwa wa Demokrasia na uhuru wa kujieleza haya yote huyaoni Mkuu.
Vyama vya Siasa vipo kisheria tulipoanza mfumo wa vyama vingi inaonekana CCM hawakuwa tayari kuupokea.
mkuu umesoma mada na kuielewa
 
Ni matokeo gani mabaya ambayo hayakuletwa na dhamira ya rais ya kuua upinzani? Kwani CUF kuna Lowassa? Mbona wamewekwa kitanzi bila sababu kwa maagizo ya juu?
Hebu tuone wapewe haki saw kama ccm hawatalia.
Sisi wapiga kura tunaelewa linofanywa naccm. Wachawi hao dawa yao iko jikoni.
Kimsingi, duniani kote, siasa zina fitna. Chama Tawala hufanya fitna ili kudumaza Upinzani na chama Pinzani chatakiwa kubuni mbinu mbadala kila uchwao kuhakikisha hakinaswi katika fitna za chama tawala. Ndivyo ilivyo duniani kote, wanatofautiana mbinu tu. Kwa kila chama, watafanya kulingana na maeneo ya udhaifu wa chama husika. Mbinu zitumikazo dhidi ya CUF haziwezi kuwa sawa na zile zitumikazo CHADEMA.


Baada ya kusema haya, sisi kubaki kulalamikia namna ambavyo tunafanyiwa ni sawa tu na kukiri kuwa hatuna namna mbadala ya kupambana na kuleta tija katika mazingira halisi ya sasa.

Hatupaswi kubaki kulalamika. Tunapaswa kutafuta namna ya ku-survive.

The Quill.
 
nilidhani ntakuta uchambuzi makini kulingana na kichwa cha habari na kina la mwandishi ila nimepoteza tuu muda wangu masikini
 
Wakati wa kampeni za uchaguzi viongozi wa cdm walianzisha kauli mbiu " weka jiwe huku weka ccm tutalichagua jiwe"

Tafsiri ya kauli hiyo ni kuwa "cdm waliishiwa sera za kuuza mbele ya wapiga kura"
 
In brief ni kwamba CHADEMA walitaka madaraka ya kuongoza nchi tu na si kujiandaa kuongoza nchi kupitia viongozi walio nao kwenye nyadhifa mbalimbali.
Tamaa za kutaka kuchukua dola ndio sababu kuu ya kumtwaa lowasa na kumpa nafasi nyeti kabisa ya kupeperusha bendera ya chama kama mgombea wao na pia kumbuka jambo hili halikuamuliwa na kamati kuu/ kikao cha wanakamati kumpitisha kuwa mgombea ila ilitumika mbinu chafu kumpitisha moja moja kwa Maelezo kuwa Katibu mkuu ambaye ndiye alikua ana hiyo nafasi kwa asilimia kubwa Dr. Slaa kuwa karidhia.
Ujio wa lowasa ulikua unatarajiwa kuwa na massive impacts in the short run hasahasa kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2015. KUMPOKEA lowasa ndani ya chama ikionekana kama ni ticket ya moja kwa moja kwenda ikulu kutokana na ukweli kuwa alikubalika kuliko mgombea yeyote wa CCM.
Mara baada ya uchaguzi kumalizika ndio ile hoja ya Dr. Slaa kuwa is he a liability or assets ikaanza Ku apply.
My point
Ujio wa lowasa ndani ya CHADEMA umesababisha hali ya sintofahamu kutokana na baadhi ya viongozi kutokubaliana na ujio na nyadhifa kuu aliyopewa kinyemela. Hii inasababisha baadhi ya vijana wenye weledi kukosa pakusimamia au pakusemea baadhi ya masuala ambayo ndio agenda kuu ya chama.
Ujio wa lowasa hauwezi kufiti na hautafiti ndani ya chadema kutokana na misingi ya chama kilichojijengea ukilinganisha na namna mitazamo ya WATANZANIA kuhusu makandokando yake.
 
Wasalaam,

Kalamu huru imevutika kuandika kidogo kuhusu mjadala wa muda mrefu wa Lowasa kuhamia CHADEMA.


Ikumbukwe kuwa, ni haki ya kikatiba kila mwananchi kujiunga au kuachana na chama chochote cha siasa. Hivyo, kuhama chama kwa kwenyewe, sio tatizo.

Kikubwa, tunaamini anajiunga kwa kuwa anakubaliana na misingi, falsafa na itikadi ya chama ajiungacho. Sote twajua hizi sio sababu zilizompeleka Lowasa CHADEMA. Ila sitajikita kwenye hilo leo.

Pamoja na yote hayo, ilipaswa mwenye kuja chamani abadilike kulingana na misingi, falsafa na itikadi ya chama.

Tatizo la ujio wa Lowasa CHADEMA ni chama kubadilika kufiti ujio wa Lowasa badala ya Lowasa kubadilika kufiti misingi, falsafa na itikadi ya chama. Hilo tu.

Ni muhimu sasa kwa chama kutengeneza (nurture and mould) vijana ambao wataweza si tu kuwa wagombea, bali viongozi wa nchi. Hii pokea pokea makapi ya CCM na kuyaamini na kuyapa nafasi nyeti bila hata kuwachunguza kwa kina dhimira zao hakukisaidii chama katika kipindi cha muda mrefu (in the long run). Matokeo yake ndio haya ya watu kuacha nafasi za uwakilishi na kumuunga mkono Rais.

Ni muhimu chama kuukubali ukweli, kuupokea na kufanya jitihada kurekebisha ili tuwe na upinzani wenye afya.

The Quill.
Kinachokera zaidi anapita kwenye kampeni badala ya kumnadi mgombea anajinadi mwenyewe kuwa atashinda urais 2020. Swali nani alimteua kuwa mgombea urais 2020? Hii ndiyo Demokrasia ya Sasa ya chama? Katika hili viongozi wakuu hakuna anayekemea. Inakera sana.
 
Back
Top Bottom