Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 17,871
- 33,236
Hii mada ni ya kisiasa ingawa nimeitoa bila ya kuwa na msukumo wa kisiasa bali kwa kufuata dhamira yangu ya kuitaka Tanzania njema huko tuendako. Ni uzalendo wangu tu ndiyo umenisukuma kuandika hiki ninachoandika. Kama kuna mtanzania anaona tumekwama basi ajue kwamba kukwama kwetu kunatokana na CCM kuwepo madarakani ama laana inayoiandama CCM kwa jinsi inavyoingia madarakani!
Wazazi wa CCM,TANU na ASP ni vyama vilivyojengwa katika misingi ya kupigania uhuru na haki za Mwafrika lakini baadaye vikageuka kuwa kandamizi kwa uhuru na Haki za waafrika wenzao. Tabia hiyo ndiyo iliifanya TANU ifute kwa hila vyama vingine vya siasa hapo mwaka 1965 na ASP kukaa madarakani kwa miaka zaidi ya 16 bila ya kufanya Uchaguzi hata wa kuigiza huko Zanzibar.
Tabia ya viongozi wa CCM na wanachama wao kutokupenda kupingwa inatokana na Uasili wa chama hicho. Kamata kamata, kupenda kuonesha ukuu wa chama (Party Supremacy) chao ni mambo ambayo CCM haitaacha kuyafanya mpaka ilazimishwe kuacha. Hata mfumo wa vyama vingi uliporudi, CCM haikusajiliwa bali ilijisajili na kujipa upendeleo wa kuwa chama cha kwanza kuwepo kwenye mfumo wa vyama vingi.
Nchi hii haijawahi kutawaliwa na chama kingine chochote cha siasa zaidi ya CCM.Kwa hiyo kama kuna wapiga Dili, kama kuna Elimu duni, Huduma za Afya zisizokidhi vigezo, Kama sehemu kubwa ya Ardhi yetu haijapimwa, kama kuna ujenzi holela mijini na vijijini, kama kuna jambo lolote unaloliona ni tatizo kwenye jamii yetu watanzania basi ujue chanzo chake ni CCM.
Sheria mbovu na kandamizi zoote zimepitishwa ama kuridhiwa na CCM. Kama kuna udhaifu wa Mahakama zetu jua chanzo chake ni sheria zilizotungwa na CCM, kama serikali ni onezi jua inatokana na mfumo unaolelewa na CCM kwa faida ya chama hicho. Hakuna namna kama watanzania tunataka kuibadili Tanzania yetu ni lazima kwanza tuiondoe CCM madarakani. Tuachane na wale watu ambao kila mara wanatuaminisha kwamba bado CCM kuna watu "wema" na "Bora" kuliko Upinzani, lakini baadaye tena hujiunga na sisi kulalamikia wale wale waliotuminisha kwamba ni Bora na ni watu wema!
Tatizo la Tanzania ni CCM na Tatizo la CCM ni CCM yenyewe!!
Wazazi wa CCM,TANU na ASP ni vyama vilivyojengwa katika misingi ya kupigania uhuru na haki za Mwafrika lakini baadaye vikageuka kuwa kandamizi kwa uhuru na Haki za waafrika wenzao. Tabia hiyo ndiyo iliifanya TANU ifute kwa hila vyama vingine vya siasa hapo mwaka 1965 na ASP kukaa madarakani kwa miaka zaidi ya 16 bila ya kufanya Uchaguzi hata wa kuigiza huko Zanzibar.
Tabia ya viongozi wa CCM na wanachama wao kutokupenda kupingwa inatokana na Uasili wa chama hicho. Kamata kamata, kupenda kuonesha ukuu wa chama (Party Supremacy) chao ni mambo ambayo CCM haitaacha kuyafanya mpaka ilazimishwe kuacha. Hata mfumo wa vyama vingi uliporudi, CCM haikusajiliwa bali ilijisajili na kujipa upendeleo wa kuwa chama cha kwanza kuwepo kwenye mfumo wa vyama vingi.
Nchi hii haijawahi kutawaliwa na chama kingine chochote cha siasa zaidi ya CCM.Kwa hiyo kama kuna wapiga Dili, kama kuna Elimu duni, Huduma za Afya zisizokidhi vigezo, Kama sehemu kubwa ya Ardhi yetu haijapimwa, kama kuna ujenzi holela mijini na vijijini, kama kuna jambo lolote unaloliona ni tatizo kwenye jamii yetu watanzania basi ujue chanzo chake ni CCM.
Sheria mbovu na kandamizi zoote zimepitishwa ama kuridhiwa na CCM. Kama kuna udhaifu wa Mahakama zetu jua chanzo chake ni sheria zilizotungwa na CCM, kama serikali ni onezi jua inatokana na mfumo unaolelewa na CCM kwa faida ya chama hicho. Hakuna namna kama watanzania tunataka kuibadili Tanzania yetu ni lazima kwanza tuiondoe CCM madarakani. Tuachane na wale watu ambao kila mara wanatuaminisha kwamba bado CCM kuna watu "wema" na "Bora" kuliko Upinzani, lakini baadaye tena hujiunga na sisi kulalamikia wale wale waliotuminisha kwamba ni Bora na ni watu wema!
Tatizo la Tanzania ni CCM na Tatizo la CCM ni CCM yenyewe!!