Tatizo la nchi hii wala sio Maprofesa na Wasomi wengine,tatizo liko hapa

Emmanuel J. Buyamba

JF-Expert Member
May 24, 2013
1,167
651
Tokea kuanza kusomwa hadharani ripoti mbalimbali za kamati za uchunguzi wa madini, kumeibuka tafsiri ya kwamba wasomi wetu hawalisaidii taifa. Kwa upande wangu huu mtazamo nauona hauko sawa.

Tatizo la nchi hii muda wote lipo kwenye mfumo mbovu unaolelewa na katiba mbovu ya nchi.

Leo kiongozi mwandamizi anaulizwa kwa nini ulisaini hizo nyaraka anajibu niliagizwa na bwana mkubwa ambae ndiyo aliyemteua. Na kwenye katiba huyo bwana mkubwa unakuta hahojiwi wala hashitakiwi mahakamani kabla na baada ya kustaafu.

Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya amefikia mahala akawaita majaji waliotengua ushindi wake kuwa ni "wakora" hali inayoonesha kuwa anachuki kali kifuani ila kwa kuwa mfumo ndiyo uliowapa majaji wale uhalali, amebaki kuugulia maumivu moyoni.

Kina professa Lipumba na wenzake nao wanafanya mambo ya hovyo leo hii kwenye chama walichofukuzwa kwa sababu tu ya mfumo mbaya wa baadhi ya vyombo vya serikali kujiingiza kwenye vyama vya siasa.

Hata hawa CCM ambao tunawaona hawafai ni kwa sababu ya system mbovu inayowapa "umungu mtu" fulani hivi wa kutenda wanavyojisikia.

Kwa hiyo ndugu zangu badala ya kuwashambulia wasomi wetu hebu hizo nguvu tuzielekeze kwenye kupigania mfumo bora wa kiuongozi.

Sote tuseme tunaitaka rasimu ya Jaji Warioba irejeshwe kwa wananchi,ijadiliwe na tupate katiba mpya!!
 
1504767341450.jpg
sasa ni kukimbiana tu. Hebu akeshea watulipe chetu mapema ili hao wengine wafuate
 
Ulivyotolea mfano wa kenya nimekuelewa sana. Nilimwona Uhuru alivyokuwa anaongea mpaka nikamshangaa. Ni kweli katiba yetu inatatizo. So far katiba ya Tanzania inampa raisi mamlaka makubwa. Kwa raisi wa ovyo hii katiba yetu ni mwiba. According to Magu katiba si kipaumbele chake hata wakati anaomba kura. Nafikiri anafanya hivyo kuendelea kuhold madaraka makubwa Kwa mabadiliko ya kiuchumi. Swali ni nani atakaye tusimamia katiba mpya ikapitishwa?
 
Hakuna namna uozo kama unaotokea Tanzania unaweza kuisha kwa watu kufikiri kuwa kuna "chama" au "mtu fulani" ndio chenye/mwenye uwezo wa kuweka mambo sawa. Hiyo ni nje kabisa ya kanuni kuu ya demokrasia. Kwanza, tujiulize ni kitu gani hasa kilisababisha binadamu hapo awali kufikia kuhitaji demokrasia katika mifumo yao ya uongozi na utawala? Ni kitu kilicho wazi kabisa kwamba, binadamu ana mapungufu na hawezi kutegemewa kutenda sahihi na haki wakati wowote. Mienendo na tabia za binadamu hazina "guarantee" yoyote. Kwa asili, binadamu wengi wakiaminiwa kupita kiasi na kukabidhiwa mamlaka yasiyo na ukomo, hujenga jeuri, dharau na kiburi kisichomithilika.

Jibu pekee ni kuweka demokrasia ya kweli inayowawezesha wananchi kuwajibisha vyama na viongozi wasipotimiza wajibu wao. Kuwafanya wawe na "hofu" ya "kauli ya umma" kama vile tunavyotakiwa kuwa na "hofu" ya Mungu. Hii kushabikia kutawaliwa na "messiah" na kundi la "mitume" wasiohojiwa hapa duniani ni ujinga uliopitiliza. Lazima tufikie mahali ambapo tunaenda kwenye chaguzi bila kuwa na uhakika wa chama kipi au mgombea yupi atashinda au kushindwa. Tatizo ni CCM? Wape guarantee hiyo hiyo CHADEMA/CUF/ACT kuwa madarakani bila kikomo kama hujaona uozo ukiendelea kama kawa.

Aidha, Rais hatakiwi kuwa na kauli ya mwisho kwenye maamuzi makuu ya kitaifa na katika teuzi/tengua za nafasi kwenye taasisi nyeti za dola. K.m. Marekani, Trump hawezi kumfukuza kazi (kumtumbua) hata mtendaji wa forodha bandarini kwa kuamuru tu akijisikia kuudhiwa. Hapa kwetu rais akisema, ndio mwisho wa yote; hahojiwi wala sheria haiuliziwi. Yakiharibika ndio anakimbilia kudai ushirikiano na uzalendo wa wote kurekebisha makosa yake. Katiba makini is the right starting point. Kenya ni mfano kiasi chake. Rais Kenyatta anatamani kufanya fujo lakini tayari amedhibitiwa na mfumo - hana janja zaidi ya kuanzisha machafuko.
 
Hakuna namna uozo kama unaotokea Tanzania unaweza kuisha kwa watu kufikiri kuwa kuna "chama" au "mtu fulani" ndio chenye/mwenye uwezo wa kuweka mambo sawa. Hiyo ni nje kabisa ya kanuni kuu ya demokrasia. Kwanza, tujiulize ni kitu gani hasa kilisababisha binadamu hapo awali kufikia kuhitaji demokrasia katika mifumo yao ya uongozi na utawala? Ni kitu kilicho wazi kabisa kwamba, binadamu ana mapungufu na hawezi kutegemewa kutenda sahihi na haki wakati wowote. Mienendo na tabia za binadamu hazina "guarantee" yoyote. Kwa asili, binadamu wengi wakiaminiwa kupita kiasi na kukabidhiwa mamlaka yasiyo na ukomo, hujenga jeuri, dharau na kiburi kisichomithilika.

Jibu pekee ni kuweka demokrasia ya kweli inayowawezesha wananchi kuwajibisha vyama na viongozi wasipotimiza wajibu wao. Kuwafanya wawe na "hofu" ya "kauli ya umma" kama vile tunavyotakiwa kuwa na "hofu" ya Mungu. Hii kushabikia kutawaliwa na "messiah" na kundi la "mitume" wasiohojiwa hapa duniani ni ujinga uliopitiliza. Lazima tufikie mahali ambapo tunaenda kwenye chaguzi bila kuwa na uhakika wa chama kipi au mgombea yupi atashinda au kushindwa. Tatizo ni CCM? Wape guarantee hiyo hiyo CHADEMA/CUF/ACT kuwa madarakani bila kikomo kama hujaona uozo ukiendelea kama kawa.

Aidha, Rais hatakiwi kuwa na kauli ya mwisho kwenye maamuzi makuu ya kitaifa na katika teuzi/tengua za nafasi kwenye taasisi nyeti za dola. K.m. Marekani, Trump hawezi kumfukuza kazi (kumtumbua) hata mtendaji wa forodha bandarini kwa kuamuru tu akijisikia kuudhiwa. Hapa kwetu rais akisema, ndio mwisho wa yote; hahojiwi wala sheria haiuliziwi. Yakiharibika ndio anakimbilia kudai ushirikiano na uzalendo wa wote kurekebisha makosa yake. Katiba makini is the right starting point. Kenya ni mfano kiasi chake. Rais Kenyatta anatamani kufanya fujo lakini tayari amedhibitiwa na mfumo - hana janja zaidi ya kuanzisha machafuko.
What you're saying is absolutely true but constitution itself doesn't guarantee the purification. All these depend on ourselves as humans, are we really smart enough to obey the rule of law? Look outside there what's going on the society! Mfano kijana alieteka watoto huko Arusha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
9 Reactions
Reply
Back
Top Bottom