Tatizo la mimba kwa wanafunzi Tanzania nini kifanyike?

kindikwili

JF-Expert Member
Oct 5, 2016
1,862
2,871
Habari za asubuhi wadau!

Leo nilikuwa nasikiliza radio nikiwa kwenye daladala kwa kweli takwimu za wanafunzi wanaopata mimba ni kubwa sana. Huko mkoani Mwanza hali inaonekana ni mbaya zaidi. Kwa kweli takwimu inawezekana ni kubwa zaidi kwa sababu maeneo mengine ya nchi haya mambo hayaripotiwi hata polisi maana mambo humalizwa nyumbani. Lakini pia huenda kuna mimba zinanyofolewa zikiwa hazijaonekana kwa wengine. Lakini hata kwa takwimu hizi ambazo serikali inazo bado hali si nzuri.

Sababu ziko nyingi sana za hawa wanafunzi kupata mimba na tukisema tuzitaje tunaweza kutaja sababu lukuki , kwa hiyo hapa natamani tungejadili namna gani tunaweza kumaliza tatizo hili. Wadau karibu sana tutoe mchango wetu ni kivipi tunaweza kuondokana na hii tabia ya dada zetu , wadogo zetu na shangazi zetu na mama zetu wadogo kupewa ujauzito wangali wadogo na kukatishwa haki yao ya kupata elimu.
 
Kwa upande wako wewe unashauri serikali ifanye nini ili iondoe au ipunguze hiyo kadhia ya wanafunzi kupewa mimba?
 
Wanafunzi wote wa kike wachomwe sindano maalumu ya kuchelewesha balehe kwa miaka 10 mbele. Yani mtoto wa kike abelehe akiwa na umri wa miaka 20. Namuomba mkuu wa nchi asimamie hili jambo kama alivyopambana kusimamia Tanzania ya viwanda. Utawala wake huu amefanya mambo makubwa sana hawezi kushindwa na hili.
 
Haya mambo yanachangiwa kwa kiasi kikubwa na jamii yenyewe. Unakuta binti mwanafunzi amepewa mimba na familia zinaamua kuyamaliza bila kuyafikisha kwenye vyombo vya sheria au wakati mwengine suala linafika hadi mahakamani lakini familia ya mhanga (binti) wanakataa kutoa ushirikiano kwa Serikali kwa aidha kumtorosha binti au kumrubuni asitoe ushahidi kwa ushawishi wa familia au mtuhumiwa mwenyewe. Kigezo kinachotumika kwa hizo familia ni je, kama baba wa mtoto atafungwa, mtoto atalelewa na nani ikiwemi huduka muhimu. So familia hujikuta zikiyamaliza haya mambo nyumbani na ndio chanzo cha visa hivi kutoisha maana watuhumiwa wanajua watayamaliza tu
 
Wa

Wanaume badilikeni acheni kutembea na wanafunzi. Solution ndio hiyo hakuna nyingine.
Hili tatizo halitaisha milele.
Wanataka wenyewe. Wakati mwingine wanaomba hela tunawapa,lift tunawapakia,mwisho wanaomba pen...zi tunawakatalia,wanaanza kulia tunawahurumia tunawapa.
 
"Nakuomba nereaaa usitoe mimba yangu wee
Mungu akileta mtoto analeta na sahani take
Muache nitamlea usitoe mimba yangu
Mungu akileta mtoto analeta sahani take" --

Basi acheni watoto waje
 
  • Thanks
Reactions: tbl
Mimba ni miongoni mwa uchumi wa viwanda kama utakumbuka raisi wetu alisisitiza kufyatua watoto Kwa kwenda mbele
 
Tatizo wanafunzi wenyewe ndo unakuta wanautaka utamuu, mwisho wa siku utamu inakuwa shibe

Halafu wengine hawajui kabisaaaa kitu kinachoitwa condomu
 
Wanataka wenyewe. Wakati mwingine wanaomba hela tunawapa,lift tunawapakia,mwisho wanaomba pen...zi tunawakatalia,wanaanza kulia tunawahurumia tunawapa.
Ni kweli. Ndo hivyo hatuwezi kubadili tabia za binadamu. Hapa tunadiscuss kupoteza muda
 
Serikali kuna sehemu inakosea hasa kwenye upande wa hukumu kugusa wanaume peke yao,ni muda sasa serikali nayo kuwaangalia hawa wanawake.

Kama nao wanawake wangekuwa kwenye sehemu ya hukumu hata kidogo nao wangeogopa zaidi,ila kwakuwa wanajua hukumu ipo kwa wanaume tu so wao hawajali sana
 
Habari za asubuhi wadau!

Leo nilikuwa nasikiliza radio nikiwa kwenye daladala kwa kweli takwimu za wanafunzi wanaopata mimba ni kubwa sana. Huko mkoani Mwanza hali inaonekana ni mbaya zaidi. Kwa kweli takwimu inawezekana ni kubwa zaidi kwa sababu maeneo mengine ya nchi haya mambo hayaripotiwi hata polisi maana mambo humalizwa nyumbani. Lakini pia huenda kuna mimba zinanyofolewa zikiwa hazijaonekana kwa wengine. Lakini hata kwa takwimu hizi ambazo serikali inazo bado hali si nzuri.

Sababu ziko nyingi sana za hawa wanafunzi kupata mimba na tukisema tuzitaje tunaweza kutaja sababu lukuki , kwa hiyo hapa natamani tungejadili namna gani tunaweza kumaliza tatizo hili. Wadau karibu sana tutoe mchango wetu ni kivipi tunaweza kuondokana na hii tabia ya dada zetu , wadogo zetu na shangazi zetu na mama zetu wadogo kupewa ujauzito wangali wadogo na kukatishwa haki yao ya kupata elimu.
Cha kufanya ni sisi wanaume tuache kutongoza watoto wa shule.
 
Umaskini ndio zao kubwa la mimba kwa mabinti, sio kwamba wanapenda, ila wanalazimishwa na uduni wa maisha, ukitaka kuamini hili angalia familia zote zenye vipato vizuri, mtoto anapata huduma zote, kwenye zile familia maskini mahitaji anayokosa mtoto ndio anatimiziwa na mabazazi kwa kurubuniwa mwisho wa siku mimba juu.
Hili tatizo kamwe halitaisha kama vipato vya familia maskini visipoimarika.
Jiulize tu kama wanasiasa na usomi wao wanafika bei/ wananunulika kale kabinti kanatoka familia maskini kanashindwaje kuhadaliwa na visenti.
 
Sheria katika suala la hisia za ngono bado nitatizo.
Tatizo ni chanzo cha malezi nyumbani na changamoto ya utandawazi .
 
Back
Top Bottom