Nachukua nafasi hii kueneza habari hii. Jamani nakuombeni tuipigie debe sana hasa mshikaji nakuomba Freeman Mbowe yapeleke mapendekezo haya Bungeni.
Nina imani kubwa kwamba tatizo la mafuta hasa nchi zetu za kiafrika ni tatizo la kujitakia! Kwa nini nasema hivi?
Kwanza kabisa ikiwa leo hao wataalamu wanaamini kwamba pombe inayotokana na mazao yetu (ethanol) inaweza kabisa kuendesha magari na mashine zote zinazotegemea petrol na diesel. Tunapozungumzioa swala la pombe nadhani sisi waafrika tuko mbele sana kwani hii ni jadi yetu toka Nabii Nuhu, sasa tunashindwa kutumia ujuzi na elimu tuliyojaaliwa bila kwenda darasani isipokuwa tunasubiri mzungu avumbue ndipo nasi tuanze kuiga! Huu ni upotofu wa viongozi wetu wasiokuwa wabunifu na wasiotakia kheri nchi yetu zaidi ya maslahi yao na utumwa wa mawazo. Brazil ambao walikuwa wakitegemea mafuta toka nje kwa asilimia 70, leo hii wamekaribia kabisa kujitegemea kwa matumizi ya ethanol... Sii jambo gumu ama laa ajabu!.. Who knows, labda Gongo linaweza kutuondoa ktk umaskini kuliko hiyo dhahabu.
Tazama tovuti hii ifuatayo na utaona hakuna kitu tunachoshindwa sisi kukifanya tena tukiweka na wasomi wetu ndio kabisaaa!
http://www.ethanolstill.com/
Nina imani kubwa kwamba tatizo la mafuta hasa nchi zetu za kiafrika ni tatizo la kujitakia! Kwa nini nasema hivi?
Kwanza kabisa ikiwa leo hao wataalamu wanaamini kwamba pombe inayotokana na mazao yetu (ethanol) inaweza kabisa kuendesha magari na mashine zote zinazotegemea petrol na diesel. Tunapozungumzioa swala la pombe nadhani sisi waafrika tuko mbele sana kwani hii ni jadi yetu toka Nabii Nuhu, sasa tunashindwa kutumia ujuzi na elimu tuliyojaaliwa bila kwenda darasani isipokuwa tunasubiri mzungu avumbue ndipo nasi tuanze kuiga! Huu ni upotofu wa viongozi wetu wasiokuwa wabunifu na wasiotakia kheri nchi yetu zaidi ya maslahi yao na utumwa wa mawazo. Brazil ambao walikuwa wakitegemea mafuta toka nje kwa asilimia 70, leo hii wamekaribia kabisa kujitegemea kwa matumizi ya ethanol... Sii jambo gumu ama laa ajabu!.. Who knows, labda Gongo linaweza kutuondoa ktk umaskini kuliko hiyo dhahabu.
Tazama tovuti hii ifuatayo na utaona hakuna kitu tunachoshindwa sisi kukifanya tena tukiweka na wasomi wetu ndio kabisaaa!
http://www.ethanolstill.com/