Tatizo la kushindwa kutambua, kuficha madhaifu ya Mpenzi wako. Nini hatima yake!?

Mwifwa

JF-Expert Member
Apr 3, 2017
46,876
122,112
Jambo la muhimu katika kuchagua mpenzi wako ama awe katika mahusiano au mwezi wako wa ndoa ni lazima/muhimu mkajuana na kutambuana tabia zenu na hatimae kuridhiana na kuingia kwenye mahusiano.

Mnaweza kudumu katika mahusiano kwa muda fulani lengo likiwa ni kuzoeana na kutambuana hizo sifa ambazo kila mmoja anataka mwezi wake awe nazo hasa mwenendo kitabia.

Kumeibuka na mtindo wa kuonesha tabia kwa mpenzi wako ambazo sio tabia halisi ulizo nazo lengo au nia yako ikiwa ni kumvutia huyo mpenzi wako ili aendelee kuwa nawe ilihali hizo tabia sio halisi.

Wengine wanaweza kuwa wawazi na kuonesha tabia zao halisi lakini ikawa ni vigumu wao kutambua madhaifu ya kila mmoja akidhani hana madhaifu.

Siku wakiingia kwenye ndoa ghafla tabia ambazo kila mmoja alikuwa nazo na wakaaminiana kipindi cha mahusianao zinaanza kuonekana zikitoweka na kuibuka tabia zingine mpya ambazo ni kikwazo katika ndoa.

Nini kifanyike kwa wapenzi wakiwa kwenye mahusiano wakitarajia baadae wawe wana ndoa ili kuonesha tabia ambazo ni za kweli wakati wa mahusiano na wakiwa kwenye ndoa, na pia ni mbinu gani itumike kutambua madhaifu ya mpenzi wako pale unaposhindwa kuyatambua na wakati akijaribu kuyaficha hayo madhaifu yake.
 
Mwenyez Mungu atusaidie tu tufanye chaguo sahihi maana hapana aisee unaweza kujiona ww umekamilika ukamuacha mwenzako kumbe ww ndo hujakamilika
Sijui Kwann binaadam hatujikubali,cjui kwann tunapenda uongo wa kupindukia

Sidhani kama kuna aliye ingia kwenye ndoa bila misukosuko lkn uvumilivu unaanzia hapo tunashindwa kuvumiliana tunashindwa kukubali kwamba hakuna mkamilifu,tunashindwa kuwa wakweli mh aisee
Nitakuwa mkweli always hata mtu akiniacha fine ila nafsi yangu ipo huru cjamdanganya kitu nitaumia tu labda amenipotezea mda lkn sio kwasababu ya ukweli wangu NO

Be You banaa kama mtu hakukubali jinsi ulivyo bac
 
Uchumba uwe na muda mrefu kiasi. Sio wa miezi miwili mitatu kisha ndoa. Uchumba wa muda mfupi sana una muda mdogo sana wa kufahamiana kwa undani hasa ktk kipindi hiki cha ubusy wa kusaka tonge mnakuwa mnakutana mara mojamoja kitu ambacho ni rahisi kuficha madhaifu.
 
Uchumba uwe na muda mrefu kiasi. Sio wa miezi miwili mitatu kisha ndoa. Uchumba wa muda mfupi sana una muda mdogo sana wa kufahamiana kwa undani hasa ktk kipindi hiki cha ubusy wa kusaka tonge mnakuwa mnakutana mara mojamoja kitu ambacho ni rahisi kuficha madhaifu.
Uko sahihi mkuu
 
Mke mwema na mume mwema hutoka kwa bwana kwa akili zetu hatuwezi
Sawa, lakini juhudi inahitajika katika kumpata huyo mwenzi mwema ambapo vigezo mbalimbali vinazingatiwa.

Sasa changamoto ni kuwa na vitu vinavyokwamisha hilo suala la kutafuta huo mwenzi wako.
Sasa ni namna gani tunaweza kuvikwepa au kujiepusha kabisa na hivi vikwazo ili kuweza kufanikiwa vizuri katika hili jambo
 
Mwenyez Mungu atusaidie tu tufanye chaguo sahihi maana hapana aisee unaweza kujiona ww umekamilika ukamuacha mwenzako kumbe ww ndo hujakamilika
Sijui Kwann binaadam hatujikubali,cjui kwann tunapenda uongo wa kupindukia

Sidhani kama kuna aliye ingia kwenye ndoa bila misukosuko lkn uvumilivu unaanzia hapo tunashindwa kuvumiliana tunashindwa kukubali kwamba hakuna mkamilifu,tunashindwa kuwa wakweli mh aisee
Nitakuwa mkweli always hata mtu akiniacha fine ila nafsi yangu ipo huru cjamdanganya kitu nitaumia tu labda amenipotezea mda lkn sio kwasababu ya ukweli wangu NO

Be You banaa kama mtu hakukubali jinsi ulivyo bac
Njoo nikuokolee muda wako
 
Igiza vitu vyote lakini sio tabia, siku zote changamoto kwenye ndoa huanza pale kunapokuwa na gap kubwa la Tabia kipindi mpo kwenye mahusiano na Maisha halisi ya Ndoa.., hivyo ni bora rangi zenu halisi mzioneshe kipindi cha mahusiano ili muwekane sawa huko huko hatimae maisha ya ndoa changamoto zitakuwa za kawaida tu!!!
 
Tabia ya mtu haijifichi kamwe... Ukijagundua too late mvumiliane tu hamna mkamilifu ila tunatofautiana viwango tuu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom