Wadau, heri ya mwezi mpya huu, nina swali ambalo linahitaji msaada wenu.
Kwa nini kuna baadhi ya watu midomo inatoa harufu mbaya!?
Hata Kama akipiga mswaki baada ya muda harufu hiyo hurudi.
Unakuta mtu meno ni meupe na masafi ila mdomo unanuka, shida ni nini?
Na dawa yake ni nini?
Karibuni wadau, shukrani sana.
*******
Ushauri
Sio kila kinachotoa harufu mdomoni kinahusiana na usafi wa kutokupiga mswaki, ukishafahamu hilo ndio utajua kwamba mwanadamu yoyote duniani lazima atoe harufu kinywani kwake. Kuna wengine wana matatizo ya kiafya tumboni pia.
Hili jambo ni gumu mno kulielezea, na ndio maana hata Dunia ya kwanza uuzaji wa Chewing gum, Spray za mdomoni zina soko sana, wewe ushangai mpaka wakina Obama wanatafuna Chewing gum, kunuka mdomo ni hasili ya mwanadamu aliepukiki hata, unaweza ukahisi unuki mwenzako akakusikia unanuka na unaweza kujihisi unanuka mdomo mtu mwengine asikusikie.
Kunywa maji mengi, na jaribu kila wakati mdomo wako uwe unachecheza kwa vitu vya ubuge ubuge,Kunywa maji kila mara na kutokuacha mabaki ya chakula kinywani usaidia pia kupunguza hali ya harufu.
Pia soma: Ongezeko la watu kunuka mdomo
Kunuka mdomo kumesababisha niachwe na mpenzi, tafadhali nisaidieni
Habari wana jamvi huyu mwanamke toka nimempata hataki nimpige kiss, denda na hata tukiongea huwa anaziba pua. Sasa jana tumekosana ndo kanambia domo langu linatoa harufu kama choo, nikaishwa mpaka pozi nikakumbuka matukio yote nikiwa na wadau nikiongea tu wanaziba pua. Dah huu mdomo huu mbona...
www.jamiiforums.com