Tatizo la infection katika damu

Mtu Mmoja

JF-Expert Member
Mar 18, 2010
593
64
wakuu,

hapa JF Dr kunana uzi huu:

https://www.jamiiforums.com/jf-doctor/210330-tonses.html

Dr Nguruvi3 alikuwa amemjinu mtoa mada kama nilivyoquote hapo chini:

Ni uvimbe katika Tonsils za kwenye koo na husababishwa na virus au bacteria. Unatibika kwa dawa kutegemeana na aina ya mdudu hasa wale bacteria. Moja ya bacteria maarufu wanaitwa streptococcal. Inapotokea ugonjwa kujirudia basi mgonjwa hufanyiwa operesheni ndogo inaitwa tonsillectomy, yaani wanaondoa tonsil. Hii inazuia kujirudia rudia ambako kunaweza kuleta complications. Wadudu kama strept wanaweza kusababaisha kitu kinaitwa peritosillar absess(Quinsy) na kuweza kusababisha mambo kama
infection katika damu(septicaemia), au sehemu nyingine kama figo na moyo.Ingawa complication hutokea nadra lakini huwezi jua hiyo nadra itatokea wapi. Ikimtokea mtu wako sio nadra ni madhara kamili.
Ningekushauri uwaone wataalam(ENT) ukiwaeleza kujirudia rudia kwa hali hiyo na kama zipo kumbu kumbu wapelekea ili wabaini ukubwa wa tatizo.

Dhana hii ya vitu baridi imeenea sana, hakuna mahali kwenye medical iterature imeelezwa. Haina ukweli. Ni Bacteria au virus. Kama ni virus huwa 'self limiting' kwasababu hakuna dawa ya kutibu virus.
Mara nyingi huwa ni bacteria ambao wanatibika kwa dawa za kawaida kabisa. Tatizo ni pale kunapokuwa na usugu na kujirudia rudia. Kinachotokea hapo ni kuwa hao bacteria wanaweza kupata access kwa kwenda sehemu nyingine na huko wakasababisha madhara makubwa zaidi. Hiyo ndiyo inaitwa complication. Kwa medical terminology, complication ni matokeo ya tatizo fulani. Kwa mfano bacteria wakitoka kwenye tonsils nakuingia katika damuhalafu kutua katika figo na kusababisha 'Glomerulonephritis', basi maradhi ya figo ni complication ya untreated tonsilitis.

sasa mheshimiwa Dr. Nguruvi 3 na wengine

naomba kujua zaidi hapo kwenye
red.

Nina mtoto wa miaka mitatu sasa na amekuwa akipata joto la mara kwa mara miguuni na kichwani kwa kama mwezi mmoja sasa. daktari kasema ana infection kwenye damu na kifua. amempa sindano za powersif na antibiotics.

1. ni namna gani nyingine ambazo huenda hiyo infection kwenye damu ilimuingia mwanangu (kumbuka hajawahi kuwa na tatizo la tonsils maishani mwake). na je,

2. nini kifanyike kuzuia maambuklizi kama hayo kwa siku za usoni? na mwisho, je,

3. hayo matibabu aliyopewa ni sahihi kwa tatizo lake au niendelee kutafuta utaalam zaidi??

asanteni sana wakuu


heri ya mwaka mpya 2012!
 
wakuu,

hapa JF Dr kunana uzi huu:

https://www.jamiiforums.com/jf-doctor/210330-tonses.html

Dr Nguruvi3 alikuwa amemjinu mtoa mada kama nilivyoquote hapo chini:





sasa mheshimiwa Dr. Nguruvi 3 na wengine

naomba kujua zaidi hapo kwenye
red.

nina mtoto wa miaka mitatu sasa na amekuwa akipata joto la mara kwa mara miguuni na kichwani kwa kama mwezi mmoja sasa. daktari kasema ana infection kwenye damu na kifua. amempa sindano za powersif na antibiotics.

1. ni namna gani nyingine ambazo huenda hiyo infection kwenye damu ilimuingia mwanangu (kumbuka hajawahi kuwa na tatizo la tonsils maishani mwake). na je,

2. nini kifanyike kuzuia maambuklizi kama hayo kwa siku za usoni? na mwisho, je,

3. hayo matibabu aliyopewa ni sahihi kwa tatizo lake au niendelee kutafuta utaalam zaidi??

asanteni sana wajibu


heri ya mwaka mpya 2012!

Habari,
Nitapenda kulijibu hili kwaajili ya uelewa.
Kwa kawaida huwa tunatumia maneno kwa kuyapatia tafsiri. Lakini wakati mwingine tafsiri hiyo inaweza isibebe ujumbe sawasawa na ilivyotumika katika lugha ya kwanza.

Mfano: huwa tunatumia neno mchafuko wa damu/ infection kwenye damu kwa kulinganisha au kumaanisha Septicaemia.
Hii si sawa kwani maana ya Septicaemia ni uwepo wa maambukizi kwenye mfumo wa mwili/kiungo au tishu. Uwepo wa maambukizi husika huamsha mfumo wa kinga wa mwili na mwili hutoa kemikali na vichocheo vya kupambana na adui/bacteria. Matokeo yake mtu hujisikia kuumwa na kuonyesha dalili husika. Muunganiko wa dalili pamoja na kupima askari wa mwili ndiyo huleta jibu kuwa mgonjwa ana Septicaemia LAKINI maambuki yaweza kuwa yapo kwenye koo/tonsils, kifua/mapafu, njia ya chakula nk. Damu hutumika kubeba tu hao askari waliozalisha na mwili ili kuwapeleka sehemu ya mapigano.

Neno maambukizi kwenye damu ni sawa na neno Bacteremia ambayo ni kuwa umeweza kufanya kipimo na kugundua kuwa kwenye DAMU kuna bakteria. Mara nyingi ni kwa kuotesha damu maabara.

Kumbuka mwanzoni maambukizi yalikuwa kwenye tishu au nyama za mwili na sasa hii ni kwenye damu.

Na hapa hali huwa ni mbaya zaidi kwani wadudu huweza kusafirishwa kutoka sehemu moja ya mwili kwenda sehemu nyingine kupitia damu kitu ambacho si rahisi/kawaida kwa Septicaemia.

Ahsante.
 
Nimepima kipimo Cha full blood picture doctor kasema sina infection kwenye damu sasa inamaana afya ipo vizuri au
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom