Tatizo la elimu ya Tanzania sio kukariri bali ni ugumu wa lugha inayotumika bila kuwekewa msingi mzuri katika lugha hiyo

Habari wanaJF,

Kuhusiana na suala la elimu bora Tanzania, mimi nadhani tulio wengi tumefikia mahali tunafikiri kufundishwa kwa kiswahili kutaboresha elimu yetu.

Sijue nyie wenzangu, ila mimi nilishangilia nilipopata D kiswahili form four national exam. Pointi hapa ni kwamba kiswahili chetu cha kila siku mitaani na majumbani sio kama nilichokiona ndani ya mtihani wa form four. Yaani kwa kweli hicho kiswahili kingetumika ndani ya mtihani wa Physics (Fizikia?) ningepata changamoto ya kuchanganua lugha afu kuchanganua somo, nahisi ningetumia mda mrefu zaidi.

Maoni yangu,
1. Kiswahili fasaha unachokutana nacho ndani ya elimu za juu, wengi hatukijui vizuri - hata tuliokulia Dar na kanda zote za pwani ... sasa sembuse wa mikoani? Tukitaka kiswahili kiwe lugha ya kufundishia, itabidi tutie mkazo katika kufundisha kiswahili fasaha na kipana kuanzia shule za awali, na espesheli kukazia yale maneno ya kisayansi, kifundi, kimahesabu, nk kwa sababu ni maneno ambayo hatutumii sana katika maongezi ya kila leo. La sivyo kama hatujui kiswahili fasaha, tutarudi kukariri mashuleni hata kama lugha ya kufundishia ni kiswahili.

2. Hizi nchi nyingi tunazozisifia kuwa na elimu bora zina tabia ya kurutubisha elimu. Mtoto anasomewa vitabu, wengine kabla hata hawajaongea vizuri. Mtoto akiwa shuleni, wazazi wanasaidia na maswala ya shule - homework nk. Leo hii siwezi amini kuna wazazi (kati ya wazazi wawili) ambao hawana elimu ya kumfundisha ama kumsaidia na maswala ya shule mtoto wa awali ama darasa la kwanza. Basi tulio wengi hatuwazii ama tuna uvivu wa kumtayarisha mtoto kimasomo kuanzia nyumbani kabla hawajaanza shule.

3. Tuzingatie fani ya ualimu kuwa ni ya muhimu sana kiasi kwamba hata uchaguzi wa watakaosomea ualimu uwe wa msingi. Tunategemea nini serikali inapopeleka waliofeli sekondari kwenda kusomea ualimu na uaskari? Hatuwezi pata walimu wenye uwezo mzuri kwa mfumo huu. Naamini wako wengi tu wenye ubongo na uwezo wakitaka kuwa waalimu lakini mshahara hauwavutii kabisa. Ni mda serikali na uongozi wa elimu nchini kuzingatia nani anachaguliwa kuwa mwalimu na nini wampe mwalimu awe na motisha mzuri wa kufundisha.

4. Mwanafunzi bora ni yule anaejiamini. Kujiamini kunakuja na malisho ya ubongo wa mtoto. Kwa mfano tabia potofu za kumuaminisha mtoto wazungu wana akili kuliko sisi - zinamfanya mtoto asijiamini na asishindane na wazungu kwa mfano huu.

5. Tutambue na kuzingatia kwamba kutojua kitu sio ujinga ila ni kutokuwa na elimu kuhusiana na kitu hicho. Ina maana ukijielimisha utakijua hicho kitu vizuri hata kuliko yule aliekucheka mwanzoni. Epuka sana sana kutumia hivi vipimo vya kizungu wanaviita IQ TEST kupima watoto wetu. Natambua mzungu alitumia hizi test kujipandisha...
Hebu fikiri staili zao za hizi test... ni kama kumuuliza mtoto wa kijijini alama ya 'pundamilia' barabarani ina maana gani, afu asipojua unamwandika ni mjinga.
 
Hiv unajua kuna watu ni wazur kwenye hayo masomo chemia na physics lakin somo la english linawasumbua sana wanaishia kupata 20% kuzungumza hata dk 1 hawez
Mkuu, mazoezi ni kila kitu. Yaan najifunza leo shuleni 'how are you' afu sina mtu wa kuongea nae kila siku anikosoe hata matamshi... sitaweza shindana na anaefanya mazoezi ya lugha hio kila siku. Shule za 'english medium' zimedhihirisha hilo.
 
Ebu sema " define physics" kwa kiswahili
Tuanzie hapo kwanza

Sent using Jamii Forums mobile app
changanua fizikia...

Mara nyingine najiuliza mbona kama vile katika kutaka kiswahili kikue tumekazana kutafsiri hata majina? Kwani nikijibu 'changanua physics' ntakuwa siongei kiswahili?

Ni kawaida sana kwa jamii (lugha) kuazima maneno ya vile vitu ambavyo havikuwa asili ya jamii (lugha). Kiswahili kimeazima na kuongeza kwenye kiswahili maneno kama 'leso', 'pesa' kwa mfumo huo
 
Kuhusu lugha ya kiswahili hatuna shida, kwa upande mwingine lugha la kiingereza ni janga kubwa sana na ukizingatia ndio lugha ya kimataifa na mfano mzuri madam akitoka Tanzania huko aendako lugha anayotumia ni kiingereza na sio cha kubabaisha anaongea kile kiingereza chenye hadhi ya kimataifa, jambo la msingi twende na wakati lugha ya kufundishia kuanzia chekechea hadi chuo kikuu iwe ni kiingereza na kwa upande wa kiswahili liwe somo tu hapo hata jeuri ya kwenda kutembelea hapo kwa m7 achana na South au USA na ukaenda kuongea mambo ya maana itakuwepo, wageni wanapata shida sana kuwasiliana na sisi wenyeji hasa wawekezaji lugha hakuna kabisa mpaka anakuongelesha kwa ishara kama bubu.

Mkuu, lengo kuu la elimu ya taifa lolote ni kuwapa watu wake walio wengi weledi na nyenzo za kukabiliana na changamoto za kila siku katika mazingira yao, na sio kuwawezesha kusafiri kwenda ughaibuni.

Tafiti zinaonesha kwamba, mtu anapata maarifa na weledi zaidi anapojifunza kwa lugha anayoielewa vizuri.

Hapa kwetu, tungetumia Kiswahili kufundishia masomo yote, na Kiingereza kifundishwe kama somo tu (lugha ya kimataifa). La msingi ni kuwa na walimu wazuri wa kufundisha lugha hiyo.

Nchi nyingi zaidi duniani zinafundisha Kiingereza kama somo tu, lakini zinafundisha masomo mengine kwa lugha zao, na wanaongea Kiingereza cha kutosha kuwasiliana na dunia. Nchi kama China, Norway, Ufaransa, Ujerumani, Poland, Ukraine Latvia, Urusi, Israel, Uarabuni n.k. zote hizo Kiingereza kinafundishwa kama lugha tu, lakini hakitumiki kufundishia masomo mengine. Kwa maana nyingine, katika nchi nyingi, Kiingereza hakitumiki kama nyenzo ya kutolea weledi na maarifa ya msingi kwa watu wao.

Kwakiasi kikubwa ni nchi za Afrika ndio zinakumbatia lugha za wakoloni (Waingereza, Wafaransa, Wabeligiji n.k.) katika kufundisha, kujifunza, na kupima ubora wa elimu. Na haya ni moja ya madhara ya ukoloni.
 
Waliosoma English medium schools shida hiyo haipo

Wasoma English Medium lugha ya kujifunzia sio tatizo Pelekeni watoto english medium schools acheni ubahili
 
Kwani kiswahili ni lugha yetu?

Maana kuna watu wajinga wachache wanaodhani ni rahisi kujifunza physics au biology kwa kiswahili kuliko kutumia kiingereza.

Ninapinga sana hii dhana ya kujifunza masomo kwa kiswahili kwani shule ya msingi tunajifunza sayansi hii kwa kiswahili lakini hadi ilinipa shida sana kuelewa misamiati ya ajabu ajabu niliyoyakuta kwenye masomo ya sayansi ambayo haitumiki kabisa kwenye maisha ya kawaida.Mfano neno kama dutu,tungamo,ujazo nene,mshitarizi,na ujinga mwigine mwingi mno.


Kama maneno hakuna popote unapoyatumia kwenye maisha ya kawaida hata kama ni kiswahili,lazima yawe magumu tu.

Tofauti na kiingereza misamiati mingi ya sayansi inaweza kutumika pia kwenye maisha ya kawaida mfano neno dense.."density"
Television kuna neno vision hapo linaeleweka vizuri..sasa kisawhili unasema luninga?!! au neno kishikwambi?!!
Acha niishie hapa,nina hasira sana na hawa wasomi wa kiswahili maana wanatuvuruga sana
Mkuu, lengo kuu la elimu ya taifa lolote ni kuwapa watu wake walio wengi weledi na nyenzo za kukabiliana na changamoto za kila siku katika mazingira yao, na sio kuwawezesha kusafiri kwenda ughaibuni.

Tafiti zinaonesha kwamba, mtu anapata maarifa na weledi zaidi anapojifunza kwa lugha anayoielewa vizuri.

Hapa kwetu, tungetumia Kiswahili kufundishia masomo yote, na Kiingereza kifundishwe kama somo tu (lugha ya kimataifa). La msingi ni kuwa na walimu wazuri wa kufundisha lugha hiyo.

Nchi nyingi zaidi duniani zinafundisha Kiingereza kama somo tu, lakini zinafundisha masomo mengine kwa lugha zao, na wanaongea Kiingereza cha kutosha kuwasiliana na dunia. Nchi kama China, Norway, Ufaransa, Ujerumani, Poland, Ukraine Latvia, Urusi, Israel, Uarabuni n.k. zote hizo Kiingereza kinafundishwa kama lugha tu, lakini hakitumiki kufundishia masomo mengine. Kwa maana nyingine, katika nchi nyingi, Kiingereza hakitumiki kama nyenzo ya kutolea weledi na maarifa ya msingi kwa watu wao.

Kwakiasi kikubwa ni nchi za Afrika ndio zinakumbatia lugha za wakoloni (Waingereza, Wafaransa, Wabeligiji n.k.) katika kufundisha, kujifunza, na kupima ubora wa elimu. Na haya ni moja ya madhara ya ukoloni.
 
Kwani kiswahili ni lugha yetu?

Maana kuna watu wajinga wachache wanaodhani ni rahisi kujifunza physics au biology kwa kiswahili kuliko kutumia kiingereza.

Ninapinga sana hii dhana ya kujifunza masomo kwa kiswahili kwani shule ya msingi tunajifunza sayansi hii kwa kiswahili lakini hadi ilinipa shida sana kuelewa misamiati ya ajabu ajabu niliyoyakuta kwenye masomo ya sayansi ambayo haitumiki kabisa kwenye maisha ya kawaida.Mfano neno kama dutu,tungamo,ujazo nene,mshitarizi,na ujinga mwigine mwingi mno.


Kama maneno hakuna popote unapoyatumia kwenye maisha ya kawaida hata kama ni kiswahili,lazima yawe magumu tu.

Tofauti na kiingereza misamiati mingi ya sayansi inaweza kutumika pia kwenye maisha ya kawaida mfano neno dense.."density"
Television kuna neno vision hapo linaeleweka vizuri..sasa kisawhili unasema luninga?!! au neno kishikwambi?!!
Acha niishie hapa,nina hasira sana na hawa wasomi wa kiswahili maana wanatuvuruga sana

Mkuu, hakuna haja ya kuita watu wengine 'wajinga' wala kuwa na 'hasira sana', unajiumiza bure. Wewe jenga hoja yako tu utaeleweka na utajibiwa kwa hoja
 
Kwani kiswahili ni lugha yetu?

Maana kuna watu wajinga wachache wanaodhani ni rahisi kujifunza physics au biology kwa kiswahili kuliko kutumia kiingereza.

Ninapinga sana hii dhana ya kujifunza masomo kwa kiswahili kwani shule ya msingi tunajifunza sayansi hii kwa kiswahili lakini hadi ilinipa shida sana kuelewa misamiati ya ajabu ajabu niliyoyakuta kwenye masomo ya sayansi ambayo haitumiki kabisa kwenye maisha ya kawaida.Mfano neno kama dutu,tungamo,ujazo nene,mshitarizi,na ujinga mwigine mwingi mno.


Kama maneno hakuna popote unapoyatumia kwenye maisha ya kawaida hata kama ni kiswahili,lazima yawe magumu tu.

Tofauti na kiingereza misamiati mingi ya sayansi inaweza kutumika pia kwenye maisha ya kawaida mfano neno dense.."density"
Television kuna neno vision hapo linaeleweka vizuri..sasa kisawhili unasema luninga?!! au neno kishikwambi?!!
Acha niishie hapa,nina hasira sana na hawa wasomi wa kiswahili maana wanatuvuruga sana
Kwani kiswahili ni lugha yetu?

Maana kuna watu wajinga wachache wanaodhani ni rahisi kujifunza physics au biology kwa kiswahili kuliko kutumia kiingereza.

Ninapinga sana hii dhana ya kujifunza masomo kwa kiswahili kwani shule ya msingi tunajifunza sayansi hii kwa kiswahili lakini hadi ilinipa shida sana kuelewa misamiati ya ajabu ajabu niliyoyakuta kwenye masomo ya sayansi ambayo haitumiki kabisa kwenye maisha ya kawaida.Mfano neno kama dutu,tungamo,ujazo nene,mshitarizi,na ujinga mwigine mwingi mno.


Kama maneno hakuna popote unapoyatumia kwenye maisha ya kawaida hata kama ni kiswahili,lazima yawe magumu tu.

Tofauti na kiingereza misamiati mingi ya sayansi inaweza kutumika pia kwenye maisha ya kawaida mfano neno dense.."density"
Television kuna neno vision hapo linaeleweka vizuri..sasa kisawhili unasema luninga?!! au neno kishikwambi?!!
Acha niishie hapa,nina hasira sana na hawa wasomi wa kiswahili maana wanatuvuruga sana

1). Lugha zote zinakua kwa kutengeneza na kutumia misamiati mipya. Na misamiati 'inakufa' isipotumiwa. Mfano: neno 'barakoa' lilikuwepo kwenye kamusi ya Kiswahili, lakini halikujulikana hadi lilipoanza kutumiwa kufuatia UVIKO-19. Kwa sasa, hata mtoto mdogo, mijini na vijijini, wanajua barakoa. Lakini sio neno la Kiingereza ni la Kiswahili.

2). Lugha zote zinakopa na kutohoa misamiati toka Lugha nyingine. Hilo neno uliloandika 'bilojia' ama 'biology' kwa Kiingereza, limekopwa toka Kilatini au Kigiriki. Halina asili ya Kiingereza. Hilo ni neno moja kati ya mengine mengi sana. Masomo mengine ya Sayansi (fizikia, kemia n.k. pia yana misamiati lukuki iliyokopwa toka lugha zingine kwenda Kiingereza). Kwa taarifa yako tu, nimesoma Sayansi hadi chuo kikuu, kwa hiyo ninaelewa ninachokizungumza.

3). Kuelewa misamiati ni sehemu ndogo tu ya elimu na kuelimika. Elimu bora ni ile inayomuwezesha mtu kukabiliana na changamoto zilizoko kwenye mazingira yake, ikiwa ni pamoja na kuwa mbunifu, jasiri, uzalendo, kuelewa haki zake, kujali haki za wengine, kudhibiti hisia zake n.k. Haya yote na mengine mengi yanapatikana zaidi kama mtu huyo atajifunza kwa lugha "anayoielewa vizuri". Tatiti zipo, ukitaka ni PM email yako nitakutumia.

4). Kwamba Kiswahili 'sio lugha yetu', hilo linahitaji mjadala mwingine. Lakini, Kiswahili ndiyo lugha inayozungumzwa na kueleweka kwa Watanzania walio wengi (kama sio wote). Kiswahili kinafaa kutumika kama lugha ya kufundishia kwa elimu ya Taifa (elimu ya wengi). Kiingereza kifundishwe kama somo, na kikifundishwa vizuri watu watakizungumza bila shida.

5). Elimu yetu ina inakabiliwa changamoto nyingi za ubora. Lakini hii ya lugha ya kufundishia ni moja ya changamoto kubwa sana.
 
Lugha kweli ni tatizo lakini binafsi nalipa uzito wa 30% na hizo 70 zilizobaki ni mfumo wetu ambao unaamini katika uwezo wa kuNAKILI yaani kwakizungu tuite COPY AND PASTE na si uelewa wa mwanafunzi katika masomo.
ole wako uulizwe what is haematology? halafu utoe maelezo yako binafsi jua umekwenda na maji.

ole wako uulizwe factors affecting industries in Tanzania halafu usahau point ya low capital na ile ya poor infrastructure jua hujajibu kitu bado.

na wale wa hisabati ole wako uandike 2x + 2 wakati marking scheme inasema 2(x + 1) ndugu yangu huna chako

kwahyo utagundua walimu na wanafunzi wote washaharibiwa na mfumo na hakuna nayewaza nje ya box na wewe ukijitia umewaza nje ya box ukajaribu kutwist akilo yako kidogo basi ndo mfumo ushakutema hivyo.

NB:jamani msiniulize tufanyaje maana hata mimi sielewi
 
Mkuu, lengo kuu la elimu ya taifa lolote ni kuwapa watu wake walio wengi weledi na nyenzo za kukabiliana na changamoto za kila siku katika mazingira yao, na sio kuwawezesha kusafiri kwenda ughaibuni.

Tafiti zinaonesha kwamba, mtu anapata maarifa na weledi zaidi anapojifunza kwa lugha anayoielewa vizuri.

Hapa kwetu, tungetumia Kiswahili kufundishia masomo yote, na Kiingereza kifundishwe kama somo tu (lugha ya kimataifa). La msingi ni kuwa na walimu wazuri wa kufundisha lugha hiyo.

Nchi nyingi zaidi duniani zinafundisha Kiingereza kama somo tu, lakini zinafundisha masomo mengine kwa lugha zao, na wanaongea Kiingereza cha kutosha kuwasiliana na dunia. Nchi kama China, Norway, Ufaransa, Ujerumani, Poland, Ukraine Latvia, Urusi, Israel, Uarabuni n.k. zote hizo Kiingereza kinafundishwa kama lugha tu, lakini hakitumiki kufundishia masomo mengine. Kwa maana nyingine, katika nchi nyingi, Kiingereza hakitumiki kama nyenzo ya kutolea weledi na maarifa ya msingi kwa watu wao.

Kwakiasi kikubwa ni nchi za Afrika ndio zinakumbatia lugha za wakoloni (Waingereza, Wafaransa, Wabeligiji n.k.) katika kufundisha, kujifunza, na kupima ubora wa elimu. Na haya ni moja ya madhara ya ukoloni.
Hello mkuu, ni kweli unaelewa zaidi unapojifunza ukitumia lugha unayoielewa vizuri. Niruke mbele kidogo - ulipoongelea ukoloni, mimi nadhani umegonga ikulu. Tulirithi mifumo ya kikoloni (tena ukoloni wa kirumi) katika mambo mengi pamoja na elimu. Naamini tulirithi elimu ya kikoloni kwa sababu ya umaskini (kwa mfano tulikuwa hatuna vyuo vya kutoshana, lazima kusoma kule nchini kwa wakoloni), ila mbeleni naamini tumeshikilia mifumo hii sababu ya ukoloni mamboleo (yaani cheti cha VETA zetu ni duni kuliko cha VETA zao.)

Nchi ulizoorodhesha kuwa zinatumia lugha zao... je tumewafikia katika uchumi wa elimu na uwekezaji wa nyenzo nzuri za elimu?
 
Hello mkuu, ni kweli unaelewa zaidi unapojifunza ukitumia lugha unayoielewa vizuri. Niruke mbele kidogo - ulipoongelea ukoloni, mimi nadhani umegonga ikulu. Tulirithi mifumo ya kikoloni (tena ukoloni wa kirumi) katika mambo mengi pamoja na elimu. Naamini tulirithi elimu ya kikoloni kwa sababu ya umaskini (kwa mfano tulikuwa hatuna vyuo vya kutoshana, lazima kusoma kule nchini kwa wakoloni), ila mbeleni naamini tumeshikilia mifumo hii sababu ya ukoloni mamboleo (yaani cheti cha VETA zetu ni duni kuliko cha VETA zao.)

Nchi ulizoorodhesha kuwa zinatumia lugha zao... je tumewafikia katika uchumi wa elimu na uwekezaji wa nyenzo nzuri za elimu?

Hizo nchi zimefika hapo zilipo kiuchumi kutokana na ubora wa elimu yao. Na kuna uhusiano mkubwa kati ya elimu bora na lugha inayotumika kufundishia. Miongoni mwa sababu za Afrika kubaki masikini ni elimu isiyokidhi mahitaji ya watu wake kijamii na kiuchumi. Elimu yetu sio bora. Na kwa Tanzania, suala la lugha ya kufundishia linaathiri ubora wa elimu yetu kwa kiwango kikubwa.
 
1). Lugha zote zinakua kwa kutengeneza na kutumia misamiati mipya. Na misamiati 'inakufa' isipotumiwa. Mfano: neno 'barakoa' lilikuwepo kwenye kamusi ya Kiswahili, lakini halikujulikana hadi lilipoanza kutumiwa kufuatia UVIKO-19. Kwa sasa, hata mtoto mdogo, mijini na vijijini, wanajua barakoa. Lakini sio neno la Kiingereza ni la Kiswahili.

2). Lugha zote zinakopa na kutohoa misamiati toka Lugha nyingine. Hilo neno uliloandika 'bilojia' ama 'biology' kwa Kiingereza, limekopwa toka Kilatini au Kigiriki. Halina asili ya Kiingereza. Hilo ni neno moja kati ya mengine mengi sana. Masomo mengine ya Sayansi (fizikia, kemia n.k. pia yana misamiati lukuki iliyokopwa toka lugha zingine kwenda Kiingereza). Kwa taarifa yako tu, nimesoma Sayansi hadi chuo kikuu, kwa hiyo ninaelewa ninachokizungumza.

3). Kuelewa misamiati ni sehemu ndogo tu ya elimu na kuelimika. Elimu bora ni ile inayomuwezesha mtu kukabiliana na changamoto zilizoko kwenye mazingira yake, ikiwa ni pamoja na kuwa mbunifu, jasiri, uzalendo, kuelewa haki zake, kujali haki za wengine, kudhibiti hisia zake n.k. Haya yote na mengine mengi yanapatikana zaidi kama mtu huyo atajifunza kwa lugha "anayoielewa vizuri". Tatiti zipo, ukitaka ni PM email yako nitakutumia.

4). Kwamba Kiswahili 'sio lugha yetu', hilo linahitaji mjadala mwingine. Lakini, Kiswahili ndiyo lugha inayozungumzwa na kueleweka kwa Watanzania walio wengi (kama sio wote). Kiswahili kinafaa kutumika kama lugha ya kufundishia kwa elimu ya Taifa (elimu ya wengi). Kiingereza kifundishwe kama somo, na kikifundishwa vizuri watu watakizungumza bila shida.

5). Elimu yetu ina inakabiliwa changamoto nyingi za ubora. Lakini hii ya lugha ya kufundishia ni moja ya changamoto kubwa sana.
Vipengele vyote ulivyoorodhesha ni ukweli. Huu ukweli ni kama sarafu, una nyuso mbili, kwa mfano:

Kipengele namba 1 - upande wa pili ni kwamba sikujua neno barakoa tulikuwa nalo siku nyingi, ni kama elimu ya nadharia bila vitendo hujui barakoa ni nini na unaivaaje... du nje ya mada, hivi kwa nini tulikuwa na neno barakoa ndani ya kamusi yetu toka zamani? ilitumikaje? ... labda vumbi letu

Kipengele namba 2 - Ni kweli. Na sababu kubwa ni kwamba vilikuwa ni vitu ama vitendo vigeni kwa hiyo havikuwa na neno la kiasili. Sasa najiuliza kwa nini leo kuna mkazo wa neno la kiswahili kwa kila kitu?

Kipengele namba 3 - Naipenda sana misamiati na elimu yake ni nzuri sana pale inapotumiwa mara nyingi ndani ya jamii (shuleni, mitaani, majumba ya dini, vyombo vya habari, wasanii, nk). Ukoloni mamboleo umesababisha umefanya misamiati iwe mapambo ya ukutani, na anaeipenda kuitwa boya.

Kipengele namba 4 - hapa ulikuwa unamjibu mwenzetu... ndio kiswahili ni lugha yetu. Na ntaongezea, kama wewe ni mbantu, kiswahili kina maneno mengi ya kabila lako. Ni lugha yako. Pia tafakari utumwa ulivosababisha lugha mpya za watu weusi kuibuka, kwa mfano Patois kule Jamaica - hii ni lugha ya mtu mweusi hata kama ni mchanganyiko wa kibantu na kiingereza ama kifaransa.

Kipengele namba 5 - sipingi ila tumewekeza nguvu nyingi sana kichwani na kwa miaka mingi kwamba kiswahili ndio sababu ya elimu kuwa duni ama kufeli HADI tumepuuzia kwa muda mrefu kwamba elimu pia inahitaji nyenzo bora na wafundishaji bora. Tumefika mahali tunakubali waliofeli form IV ndo waje kuwa walimu halafu tunalalamika kwa nini elimu ni duni. Kiswahili kimekuwa kisingizio kikubwa kwamba tunashindwa kutambua mbona watoto hawa hawa wakienda english medium ama shule za wenye "vipaji" wanafanya vizuri? Mbona wazazi wetu (vizazi vya kabla ya uhuru na baada ya uhuru) walitoka vijijini hawajui hata kiswahili wakafanya vizuri hadi Makerere ama Cambridge? Mbona babu alieishia la nne ana elimu kubwa kuliko wa leo alieishia la saba? ... Japo ni bora kufundishia kiswahili, sio kinachoangusha elimu yetu leo.


* Swali kwa wenzangu wote wanaJF - Je ni lazima tukitumia kiswahili kufundisha, tutafute neno la kiswahili la Bunsen Burner? Tulio wengi tuliona rahisi kuiita television - televisheni kuliko 'luninga'. Kulikuwa na sababu gani ya kutafuta neno luninga wakati hatujaunda televisheni? Yaani hata Covid tumetafuta neno la kiswahili, kwa nini? kwani ni yetu kuimiliki? Kwangu mimi, kuhusu vitu vilivyoundwa... jina linaanza na muundaji, wengine tunaiga ila tunabadili matamshi na maandishi kuendana na lugha zetu na herufi zake. Ukichunguza dunia yetu, vitu muhimu maishani kwa kila mtu kama maji na mama havina maneno tofauti sana ndani ya lugha nyingi tu. Leo hii nikiwa natayarisha simu janja mpya nakimbilia menu ya kiingereza manake menu ya kiswahili maneno mapya kwangu kibao. Nikitafakari kama hili lingekuwa darasa, ningepoteza mda na labda kufeli sababu ya kujifunza hiki kiswahili kipya. Huu mwenendo wa kutafuta neno la kiswahili kwa kila jipya linaongeza ugumu wa kiswahili na litaangusha lengo la kiswahili kuwa lugha rahisi ya kufundishia elimu.
 
Hizo nchi zimefika hapo zilipo kiuchumi kutokana na ubora wa elimu yao. Na kuna uhusiano mkubwa kati ya elimu bora na lugha inayotumika kufundishia. Miongoni mwa sababu za Afrika kubaki masikini ni elimu isiyokidhi mahitaji ya watu wake kijamii na kiuchumi. Elimu yetu sio bora. Na kwa Tanzania, suala la lugha ya kufundishia linaathiri ubora wa elimu yetu kwa kiwango kikubwa.
Ukitaka kufanikisha kitu, inatakiwa uwe na msimamo na usiyumbe. Ukifanya hivo, hata ukifeli, patajulikana ulifeli wapi. Tuchambue msimamo wetu - kwa nini tuliamua shule ya msingi kiswahili, ya sekondari kiingereza? tungeamua moja mfumo mzima. Wakenya waliamua lugha moja mfumo mzima. Sio kila familia Kenya wanabonga kimombo nyumbani, wanaongea kiswahili. Tulifundishwa kuwaona ni vibaraka kwa hilo swala, ila leo hii elimu yao inatuzidi kiwango na wanaongea kiswahili zaidi kuliko zamani... Pia Uganda, Zaire na watuzungukao.

Nchi kama China, India, Singapore, na nyingi nyingenezo hususani barani Asia, zilikuwemo kwenye orodha ya nchi maskini duniani mwaka 1961. Ziliwahi tawaliwa na mkoloni. Walifanya nini kufikia kiwango cha leo? Naamini...

1. Walijitambua - Pamoja na ukoloni kuwepo, walisisitiza mila na desturi zao na wakazipandisha hadhi na matumizi baada ya ukoloni. Mojawapo ya mila na desturi ni ile ya kusisitiza elimu (umuhimu na adabu) na wazazi kujitoa mhanga mtoto asome amzidi. Tulikuwa na mila hizi... niaje siku hizi? Siku hizi tunatungiwa sheria za kusisitiza kumpeleka mtoto shule pamoja na kusogezewa mashule kila kata. Nini tofauti na kina babu na babu waliotembea kwa miguu siku mbili kwenda shule?

2. Uzalendo - umpende mmasai ama usimpende, mpe sifa yake kuwa mzalendo na kutomeza ukoloni mamboleo. Hili limemfanya adumishe na kuendeleze vizuri elimu yake ya kijadi. Pale alipoongeza vyombo ama elimu nje ya jadi ilikuwa kuboresha yake sio kuibomoa. Kwa hiyo leo hii atakufungia dawa zake kwenye plastiki badala ya jani la mgomba. Ataisaga dawa zake ni kimashine, nk. La msingi, Dawa hajabadili. Sisi tulio wengi tumemeza ukoloni mamboleo, hadi watoto wakisomea chini ya mwembe hatuwakazii wala kuwasaidia kimasomo (tuition nk) kuliko yule aliepo shule za maghorofa za kulipia... Kiundani, tumejitayarisha na kuwatayarisha watoto kufeli sababu wanasomea chini ya mwembe

* Chunguza mchina, mhindi (hata wa bongo), na myahudi... Mila, desturi, dini zimewaunganisha na wamezitumia kutopokea wala kumeza ukoloni mambolea na tabia zake na kusisitiza elimu, uzalendo na mafanikio ya elimu... hata wakibezwa kiasi gani. Angalia kila kizazi wana wasomi wangapi ndani ya jamii zao.
 
umeongea vitu vyote vya kweli. nachukia sana elimu ya kukariri na sio kuelewa. lugha ni tatizo kubwa sana na ningekuwa Rais ningesababisha kuanzia kindergarten hadi unviersity tutumie kiingereza. na tukifanya hivyo sio kwamba kiswahili kitakufa hapana. mbona sisi wengine tulizaliwa vijijini kiswahili tumekuja kukijua baadaye tulipoingia shule, tumeishi mjini miaka mingiiii hadi tumechoka na huku mjini hatuongei lugha zetu za kabila, ila hadi leo, niko fluent kwenye lugha yangu ya kabila kuliko hata kiswahili.

bahati mbaya hata kubadilisha mitaala kwamba kitumike kiswahili hadi university tuachane na kiingereza, bado hatuna material za kutosha kufundishia, vitu vyote vya elimu tunaimport toka kwa wenzetu ndio tufundishie watoto wetu. ni muda wa kuamua tu kwamba tutumie english through out, na hatutapoteza kitu. nakaribisha maprofesa wa kiswahili wa udsm waje hapa najua lazima watoe povu.
Acheni uongo!! shule zooote zipo hapa nchini! kifaransa kijermani, kiinglish chenu hicho! kama weye ni kilaza ni kilaza tu usitafute sababu!! wooote tumesoma shule hizo hizo za kayumba !! lkn tuko juuu!! kwani English media hkn failure??

English course zipo tele kama maji!...siuende kasome hata sasa zipo!! Elimu haina mwisho ukifail usi singizie sirikali!! Naomba wahusika mkazie hapo hapo Kiswahili lazima yajue haya majitu!! na ukishindwa kwenu!...hata uingereza kuna failure mbaya!

MNaanzaga ivo ivo!!! mara mtataka Kiitaliano, mara kirusi jinga kabisa nyie!!...warusi mbona wameendelea wantikisa Dunia? Putin kiingereza hajui kabisaa,........wachina je? wajapani??

acheni ujinga someni vya kwenu mnatamani vya wengine hovyo tu!!....kwanza wazungu wenyewe wanajifunza kiswahili!..tatizo humu wanaingia watu wote hata wale mbumbu kabisaaa!!......

Division zero nyie!!!!..... hamna maana kabisa! mnataka kila kitu!
 
Back
Top Bottom