platozoom
JF-Expert Member
- Jan 24, 2012
- 9,364
- 11,150
Niliwahi kuwa na jirani nikiwa mtoto aliyekuwa na huo ugonjwa. Watu walikuwa wanasema wenye huo ugonjwa kuwa hawafiki miaka 18...imani za mitaani hizo.
Huyu dada alikuwa mkubwa, akapata kazi. Ila alikufa baada ya kuolewa. Alafu alikuwa hata ukimuona unajua kuwa yuko weak. Inatia huruma sana. Kama unampenda mpe matumaini na mwambie kuwa unajua anaumwa and you dont care.
Tatizo naona na wewe umeshaanza kuwa na wasiwasi. Inataka upendo wa dhati kuwa na uhusiano na mtu mwenye ugonjwa kama huo. Ni moja ya magonjwa ambayo familia za Kiafrika zilikuwa zinachunguza kabla ya kuoa au kuolewa na koo fulani.
Nami namfahamu mmoja tukiwa wadogo kama 6yrs yeye alikuwa kama ana 15 lakini aliiishi ingawa alikuwa weak, na tatizo la wakati ule kunyanyapaliwa lakini akazoea maisha yakaendelea. Nyepesinyepesi zinasema alipokuwa amelala kitandani (chumba cha bibi yake) siku hiyo akiumwa mida ya saa 9 usiku bibi yake akamnyonga......asubuhi sisi tukiwa majirani aliwagongea wazazi wetu kwamba mjukuu wake kafariki.
Hii story alkuja kuitoa pia mjukuu wake mwingine ambaye alkuwa chumba cha pili na hakikuwa na dari na kwa maelezo yake anasema siku tatu kabla kulikuwa na kikao kati ya bibi yao na ma-bibi wenzie usiku kwamba na wao wanataka kuona huyo bibi anatimiza 'jukumu lake"........Hatukuweza kuamini sana lakini lilotushtua ni kwamba baada ya mazishi huyo mjukuu wake alitueleza alikataa katakata kulala kwenye ile nyumba na akaja kwetu nikalala naye chumba kimoja, na mara nyingi alikuwa akiweweseka sana.
It was so sad jamaa alikuwa mtu mzuri sana alkikufa at age of 24