Fumadilu Kalimanzila
JF-Expert Member
- Dec 10, 2016
- 1,651
- 5,126
Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli mimi najua wewe ni jembe kwelikweli na hutaki mchezo katika masuala ya kazi.
Nakuomba Mkuu najua nafasi hizi Mungu ndiye hupanga.
Angalia tena wakati unamwapisha Ndugu Martin Shigela kuwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga, pamoja na Shigela kuwa na Masters ya sheria (LLM) alishindwa kabisa kusoma kiapo. Ni mtendaji mzuri na anachapa kazi kwelikweli!
Mwingine aliyewahi kubabaika sana mbele yako ni Eng. Stella Manyanya wakati akiapa kuwa Naibu Waziri .
Mkuu nakuomba ebu tumia hekima yako Mungu aliyokujalia pamoja na vyombo vyako katika jambo hili.
Kama ulivyosita kutia saini kunyonga wale wafungwa basi ebu sita tena katika maamuzi yako kuhusu Mhe. Francis Ndulane.
Mimi binafsi simjui huyu ndugu Francis Ndulane ila imeniuma sana pale nilipojaribu kuvaa viatu vyake!
Sina ninaloweza kumsaidia zaidi ya kuandika hapa kwenye huu ukurasa basi.
Najua Mwenyezi Mungu hufanya kazi kwa namna ya ajabu pengine huu ujumbe waweza kukufikia. Ahsante.
Nakuomba Mkuu najua nafasi hizi Mungu ndiye hupanga.
Angalia tena wakati unamwapisha Ndugu Martin Shigela kuwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga, pamoja na Shigela kuwa na Masters ya sheria (LLM) alishindwa kabisa kusoma kiapo. Ni mtendaji mzuri na anachapa kazi kwelikweli!
Mwingine aliyewahi kubabaika sana mbele yako ni Eng. Stella Manyanya wakati akiapa kuwa Naibu Waziri .
Mkuu nakuomba ebu tumia hekima yako Mungu aliyokujalia pamoja na vyombo vyako katika jambo hili.
Kama ulivyosita kutia saini kunyonga wale wafungwa basi ebu sita tena katika maamuzi yako kuhusu Mhe. Francis Ndulane.
Mimi binafsi simjui huyu ndugu Francis Ndulane ila imeniuma sana pale nilipojaribu kuvaa viatu vyake!
Sina ninaloweza kumsaidia zaidi ya kuandika hapa kwenye huu ukurasa basi.
Najua Mwenyezi Mungu hufanya kazi kwa namna ya ajabu pengine huu ujumbe waweza kukufikia. Ahsante.