Pretty R.
JF-Expert Member
- Apr 14, 2012
- 200
- 31
Habari zenu madokta wa jf? Mm nina tatizo la ngozi ambalo linanifanya nikose hamu ya kuishi kwa sababu kila dokta ninayemwendea ananiambia tatizo lake, mwingine ananiambia allerg ya sulphur, mwingine naungua na mionzi ya jua na wengine wananiambia allerg ya vipodozi na sijawahi kutumia cream. Tatizo hili lilinianza nikiwa form six uso ukaanza kuwa mweusi na baadaye ukasambaa mpaka kwenye mikono na shingoni ila sehemu zingine zipo kawaida. Ni mwaka wa 3 sasa nahangaika kwenda hospital bila matokeo yoyote mazuri. I'm frustrated kama kuna mtu anaweza kunisaidia humu jf anisaidie jamani nateseka sn. Asanteni nasubiri michango yenu.