Heshima wakuu,
Mimi ninatatizo la jino moja tu la mbele kupata ganzi ninapokunywa maji
ya baridi au ninapo vuta upepo. Please naomba mwenye ushauri hapa
jamvini anisaidie.
Asante!Pole sana!
Nashukuru kwa ushauri ndugu,ila pia kuna jino nimeziba nahisi pengine ni hayo material ndo yanaleta hivyo vitu,au wasi wasi wangu tu?Hospital inakuhusu na ufanye haraka
Hata mimi nasumbuliwa meno kufa ganzi, ya kwangu hayajatoboka wala kuoza.Nina tatizo kama lako na bado sijapona. Epuka kutumia nguvu wakati unapiga mswaki au epuka kupiga mswaki kwa muda mrefu. Wanagoogle wanasema ukiona umeanza kuhisi ganzi ktk meno ujue kuna layer ya juu kwenye meno umeiondoa, layer ya chini inayobaki ni very sensitive-ndo maana unapata ganzi. Hii sio suluhisho la tatizo, lakin itasaidia kuepuka matatizo zaidi.
Ukipata matibabu nifahamishe inbox.
Acha kutumia Whitedent, tumia Colgate utaponaHabari zenu wanajamvi,mnamo mwanzoni mwa mwaka jana nilianza kusumbuliwa na meno na hali ya kuwa na ukakasi kama mtu aliyekula ndizi mbichi au limao mdomoni,yaani kuna wakati nakuta kinywa ni kikavu hata nashindwa kuongea vizuri.Tena siwezi kukaa eneo lenye kelele nahisi meno yanakela kama mtu anaposugua kitu chenye kelele mfano wa bati kwenye sakafu.Naomba nisaidiwe ni nini hii jamani?
nipigie nkupe formula ya kutengeneza dawa ya kienyeji
Ni ipi hiyo dawa,iweke hapa isaidie wengi ndugu.Dah, pole sana bro.
Nayajua maumivu ya meno, pole tena. Maana yakianza kuuma, unaweza vua hata Nguo ukijua ni nzito.
Nilitibiwa kwa dawa ya kienyeji, dawa ya meno lkn ilipitia sikioni!!!! Siku 2 nilipona kabisa.
Nenda Hospital mapema upate Tiba