Azizi Mussa
JF-Expert Member
- May 9, 2012
- 9,172
- 7,427
Kwa atakaye kuwa na swali lolote aniulize .safari hii nitamjibu hapa hapa na kwa uwazi kabisa.Kwa hali ilivyo kwa sasa, hii ndio itakuwa njia bora kabisa!
Ndugu zangu, kwanza nawasalimu sana!
Kwa kipindi sasa nimekuwa nikijaribu kusisitiza kuridhiana na kurudisha uhusiano mwema miongoni mwa wanachadema kwa kukwepa kueleza wazi wazi kile kinachotokea dhani ya chama nikiamini kwamba wahusika wangenielewa na kuchukua hatua za haraka kwa kuwa wanaelewa vizuri kile wanachokifanya. Kwa bahati mbaya ni kwamba inaonekana jitihada hizo zimekwama na bado baadhi ya viongozi wa chama wanaendelea kuzunguka huku na kule wakifitinisha wanachama wenzao na wananchi. Hali hii ya uchonganishi naona sasa imefikia hatua mbaya kiasi kwamba naona hamna haja ya kuendelea kufichaficha mambo!.
Kwa mfano, Kufuatia hotuba aliyoitoa Mchungaji Msigwa huko Arusha 04/12/2013, ilikuwa kwa kiwango kikubwa imejaa uchonganishi na uchochezi miongoni mwa wanachama kufikia kiasi cha msikilizaji mmoja ndugu Exaud Mamuya kusema " kutokana na speech ya Mh Msigwa, Zitto angetokea bahati mbaya angegombaniwa na kuraluliwa kama Simba aonavyo kitoweo." Katika mazingira haya naomba sasa niwe muwazi zaidi kidogo.
Ndugu wana CHADEMA wenzangu,
Tatizo la msingi kwa sasa ndani ya CHADEMA, ni "u-mwenyekiti".Hizi mbio tunazoziona mitaani kwa sasa, na kurushiwa maneno kwa ndugu Zitto,ni matokeo tu lakini suala la msingi ni "u-mwenyekiti "ndugu zangu.Tatizo la msingi ni Zitto kuonekana anaonesha dalili za kugombea uenyekiti na kuonekana ana ushawishi ndani na nje ya chama hivyo asipochafuliwa na kufitinishwa haraka, anaweza akashinda uenyekiti kweli.
Ndugu wana CHADEMA wenzangu,
Imeonekana kwamba kutokana na umaarufu wa Zitto kutokana na mambo aliyokifanyia Chama na taifa kwa ujumla ukichanganya na uwezo wake binafsi, si rahisi kwa mtu mmoja kumchafua na akachafuka bali hilo linaweza kufanyika kwa ufanisi kwa kuunda kundi kubwa na ikiwezekana kuishawishi kamati kuu kufanya mchezo huo wa hatari, wakufedhehesha, na kukatisha tamaa kabisa; mchezo ambao ni dhambi kumbwa sana.
Ndugu wana CHADEMA wenzangu,
Kitu kinachofanyika kwa sasa, licha ya kwamba ni dhambi na udhalimu mkuu, kinasababisha wananchi kugawanyika makundi makundi bila sababu ya msingi. Kadhalika kunasababisha wote tuonekane kama watu ambao tunalenga kupigania vyeo na maslahi tu na tusio kuwa na maono wala uadilifu wa kiuongozi hali hiyo hutufanya tuonekane tuko radhi hata kumtoa mtu muhanga kwa dhuluma ili tufikie lengo..Hali hiyo haiwezi kuwa na manufaa kwetu binafsi, kwa chama wala kwa taifa letu.
Ndugu wana CHADEMA wenzangu,
Hatuwezi kuwa vionzi bora wala hatuwezi kupewa madaraka ya kuongoza nchi hii kwa kufanyiana hila, uzushi, fitna majungu na kuchonganishana wenyewe kwa wenyewe.
Ndugu wana CHADEMA, wenzangu,
Wakati wote tumekuwa tukimlaumu na kumkemea Naibu Katibu mkuu wa CCM, ndugu Mwigulu Nchemba kwa kufanya siasa chafu za fitna na kugombanisha watu. Sasa na sisi tunafanya nini sasa? Tunafanya nini sasa?tunafanya nini ndugu zangu!
1.Nilijiapiza kujiepusha kwa uwezo na maarifa yangu yote kumdhulumu mtu yeyote kwa sababu yeyote na nikamuomba mungu anisaidie!.
2. Nilijiapiza kujiepusha kushirikiana na mtu yeyote kumuhujumu mtu yeyote kwa dhuluma na nikamuomba mungu anisaidie!.
3. Nilijiapiza kumkosoa mtu yeyote kwa njia ya hekma na busara na kumshauri ajirekebishe ikiwa anamdhulumu mwenzake kwa kutokujua au kwa makusudi na nikamuomba mungu anisaidie!.
Kwa sababu yeyote ile, sitakuwa tayari kuihalifu misingi yangu hii kwa sababu yeyote ile ,kwani kufanya kinyume na hapo, itakuwa ni kuchagua njia mbaya miongoni mwa njia mbaya kabisa !.
2. Mh. Lema, umemkosea Zitto na wewe unaelewa hilo, muombe radhi tusoonge mbele tafadhali!,
3. Kilewo, Umefanya jambo ambalo si jema sana kwa kusambaza waraka wa kumchafua Zitto bila kujua au kwa kujua, muombe radhi Zitto yaishe tujenge chama na nchi yetu!.
4. Mchungaji Msigwa! Wewe ni mchungaji, tumia busara za kichungaji muombe zitto msamaha! Wewe umemchafua na unaendelea kuuchafua zitto kwa makusudi na hali unajua. Ni bora ukaomba radhi yakaisha.! hauwezi kupungukiwa na kitu Msigwa!
5. Yericko Nyerere na wenzako wewe tumekuwa tukiungana mkono katika mambo mengi na wewe unalijua hilo, ila katika hili mimi nafsi yangu inakataa!.Tumia uaminifu wetu kumuomba Zitto radhi kwani wewe unajua umemfanyia nini!.Yericko naomba kwa hili tuwe waaminifu na busara itawale.Naamini mungu atakuongoza vyema.
Nawasihi sana wale mnaoendelea kuzunguka mitaani. Tafadhalini sana wekezeni nguvu zenu katika kushughulikia matatizo ya watu badala ya kuwachonganisha wanachama ikiwa kweli ninyi ni waadilifu, wenye nia njema na chama pamoja na nchi hii. Hatuwezi kuwa na mapenzi mema kwa jamii kwa kuchonganishana ,kufitinishana na kuchafuana!
Ni matumaini yangu kwamba jambo hili la kuendelea kuzunguka watu wakichafuana litakoma na atakayeliendeleza wananchi watamuelewa vyema!.
Ndugu zangu, kwanza nawasalimu sana!
Kwa kipindi sasa nimekuwa nikijaribu kusisitiza kuridhiana na kurudisha uhusiano mwema miongoni mwa wanachadema kwa kukwepa kueleza wazi wazi kile kinachotokea dhani ya chama nikiamini kwamba wahusika wangenielewa na kuchukua hatua za haraka kwa kuwa wanaelewa vizuri kile wanachokifanya. Kwa bahati mbaya ni kwamba inaonekana jitihada hizo zimekwama na bado baadhi ya viongozi wa chama wanaendelea kuzunguka huku na kule wakifitinisha wanachama wenzao na wananchi. Hali hii ya uchonganishi naona sasa imefikia hatua mbaya kiasi kwamba naona hamna haja ya kuendelea kufichaficha mambo!.
Kwa mfano, Kufuatia hotuba aliyoitoa Mchungaji Msigwa huko Arusha 04/12/2013, ilikuwa kwa kiwango kikubwa imejaa uchonganishi na uchochezi miongoni mwa wanachama kufikia kiasi cha msikilizaji mmoja ndugu Exaud Mamuya kusema " kutokana na speech ya Mh Msigwa, Zitto angetokea bahati mbaya angegombaniwa na kuraluliwa kama Simba aonavyo kitoweo." Katika mazingira haya naomba sasa niwe muwazi zaidi kidogo.
Ndugu wana CHADEMA wenzangu,
Tatizo la msingi kwa sasa ndani ya CHADEMA, ni "u-mwenyekiti".Hizi mbio tunazoziona mitaani kwa sasa, na kurushiwa maneno kwa ndugu Zitto,ni matokeo tu lakini suala la msingi ni "u-mwenyekiti "ndugu zangu.Tatizo la msingi ni Zitto kuonekana anaonesha dalili za kugombea uenyekiti na kuonekana ana ushawishi ndani na nje ya chama hivyo asipochafuliwa na kufitinishwa haraka, anaweza akashinda uenyekiti kweli.
Ndugu wana CHADEMA wenzangu,
Imeonekana kwamba kutokana na umaarufu wa Zitto kutokana na mambo aliyokifanyia Chama na taifa kwa ujumla ukichanganya na uwezo wake binafsi, si rahisi kwa mtu mmoja kumchafua na akachafuka bali hilo linaweza kufanyika kwa ufanisi kwa kuunda kundi kubwa na ikiwezekana kuishawishi kamati kuu kufanya mchezo huo wa hatari, wakufedhehesha, na kukatisha tamaa kabisa; mchezo ambao ni dhambi kumbwa sana.
Ndugu wana CHADEMA wenzangu,
Kitu kinachofanyika kwa sasa, licha ya kwamba ni dhambi na udhalimu mkuu, kinasababisha wananchi kugawanyika makundi makundi bila sababu ya msingi. Kadhalika kunasababisha wote tuonekane kama watu ambao tunalenga kupigania vyeo na maslahi tu na tusio kuwa na maono wala uadilifu wa kiuongozi hali hiyo hutufanya tuonekane tuko radhi hata kumtoa mtu muhanga kwa dhuluma ili tufikie lengo..Hali hiyo haiwezi kuwa na manufaa kwetu binafsi, kwa chama wala kwa taifa letu.
Ndugu wana CHADEMA wenzangu,
Hatuwezi kuwa vionzi bora wala hatuwezi kupewa madaraka ya kuongoza nchi hii kwa kufanyiana hila, uzushi, fitna majungu na kuchonganishana wenyewe kwa wenyewe.
Ndugu wana CHADEMA, wenzangu,
Wakati wote tumekuwa tukimlaumu na kumkemea Naibu Katibu mkuu wa CCM, ndugu Mwigulu Nchemba kwa kufanya siasa chafu za fitna na kugombanisha watu. Sasa na sisi tunafanya nini sasa? Tunafanya nini sasa?tunafanya nini ndugu zangu!
MSIMAMO WANGU.
Mimi tangu nilipopata akili, nilijiapiza na nikamuomba mungu anisaidie kwenye mambo kadhaa!.
1.Nilijiapiza kujiepusha kwa uwezo na maarifa yangu yote kumdhulumu mtu yeyote kwa sababu yeyote na nikamuomba mungu anisaidie!.
2. Nilijiapiza kujiepusha kushirikiana na mtu yeyote kumuhujumu mtu yeyote kwa dhuluma na nikamuomba mungu anisaidie!.
3. Nilijiapiza kumkosoa mtu yeyote kwa njia ya hekma na busara na kumshauri ajirekebishe ikiwa anamdhulumu mwenzake kwa kutokujua au kwa makusudi na nikamuomba mungu anisaidie!.
Kwa sababu yeyote ile, sitakuwa tayari kuihalifu misingi yangu hii kwa sababu yeyote ile ,kwani kufanya kinyume na hapo, itakuwa ni kuchagua njia mbaya miongoni mwa njia mbaya kabisa !.
KWA SASA KILICHOBAKIA NI HIKI;
1. Mh. Mbowe! Muombe radhi Mh.Zitto kwani wewe unajua umemfanyia nini na unaujua vizuri mkakati unaoendelea. Mwenyekiti muombe radhi mwenzako yaishe tujenge chama na taifa letu!
2. Mh. Lema, umemkosea Zitto na wewe unaelewa hilo, muombe radhi tusoonge mbele tafadhali!,
3. Kilewo, Umefanya jambo ambalo si jema sana kwa kusambaza waraka wa kumchafua Zitto bila kujua au kwa kujua, muombe radhi Zitto yaishe tujenge chama na nchi yetu!.
4. Mchungaji Msigwa! Wewe ni mchungaji, tumia busara za kichungaji muombe zitto msamaha! Wewe umemchafua na unaendelea kuuchafua zitto kwa makusudi na hali unajua. Ni bora ukaomba radhi yakaisha.! hauwezi kupungukiwa na kitu Msigwa!
5. Yericko Nyerere na wenzako wewe tumekuwa tukiungana mkono katika mambo mengi na wewe unalijua hilo, ila katika hili mimi nafsi yangu inakataa!.Tumia uaminifu wetu kumuomba Zitto radhi kwani wewe unajua umemfanyia nini!.Yericko naomba kwa hili tuwe waaminifu na busara itawale.Naamini mungu atakuongoza vyema.
Nawasihi sana wale mnaoendelea kuzunguka mitaani. Tafadhalini sana wekezeni nguvu zenu katika kushughulikia matatizo ya watu badala ya kuwachonganisha wanachama ikiwa kweli ninyi ni waadilifu, wenye nia njema na chama pamoja na nchi hii. Hatuwezi kuwa na mapenzi mema kwa jamii kwa kuchonganishana ,kufitinishana na kuchafuana!
Ni matumaini yangu kwamba jambo hili la kuendelea kuzunguka watu wakichafuana litakoma na atakayeliendeleza wananchi watamuelewa vyema!.