Nimefuatilia kwa umakini kuhusu kampeni zinazoendelea hadi sasa. Kimsingi CCM inaongoza kwa mikakati na mbinu bora zaidi kuliko vyama vingine vya Chadema,ACT nk na hivyo kuwa na nafasi nzuri ya kushinda asilimia 80+ Hii ni kutokana na sababu zifuatazo:
1. CCM imeweza kuwatumia makada wake kikamilifu walosambaa nchi nzima wakifanya kampeni kwa mpigo wakati wapinzani wamemwachia mgombea uraisi pekee kwa sasa.kwa mfano tumeona huko zanzibar juzi makada wengine wa Chadema hawakuwepo kabisa inaonekana wamejikita kwenye majimbo yao wakipigania uhai wao.
2. CCM wamaonekana kuwa wako makini - serious-kupambana kwelikweli kwa nguvu zote bila kupuuza chochote mbele yao na wakijibu hoja za wapinzani na hapohapo wakifafanua sera zao wakati wapinzani wanatumia muda mchache kuelezea sera zao na hususani kuelezea kwa kina udhaifu wa sera za chama tawala na madhara yake kiuchumi na ustawi wa jamii kwa kipindi cha muda mfupi na mrefu badala yake wanatoa hoja nyepesi.
3.CCM wanatumia saikolojia ya kujaza watu kwenye mikutano ili kujenga mob sychology kuonyesha kukubalika kwao kwa wananchi ili baadaye tarehe 28.9.2020 wapigiwe kura kwa imani kuwa hiki ndicho chama kinachokubalika na wengi na kwa kuchagizwa na propoganda sahihi
4.Wana uwezo kifedha na logistiki vitu ambavyo vimewarahisishia zaidi kuyafikia maeneo yote muhimu ya wilayani majimboni na vijijini.
5.Mikoa yenye kura nyingi ya kanda ya ziwa mgombea wao ameitumia vizuri fursa ya kujitangaza pamoja na wagombea ubunge na madiwani kwenye mikutano ya kampeni.Aidha ameweza kufukia mashimo ya waliachwa kwenye kura za maoni.
6.CCM inajitahidi kutoacha pengo au mwanya kwa wapinzani sasa hivi kusini kuna JK na Mama SAmia na kaskazini Waziri Mkuu wakati wapinzani hawaonekani kusambaa nchi nzima nguvu kubwa kila mmoja kwenye jimbo lake. Kutoka na uhaba wa fedha wameshindwa kusambaza nguvu kazi zao kusaidia majimboni.
7.Mgombea uraisi anaeleweka kwa lugha nyepesi kwa wananchi na anazungumzia maendeleo yanayoonekana. Hii inamwongezea hali ya kuaminika zaidi akipewa madaraka. Mbinu ya kutumia vikundi visivyoonekana,wanamuziki na coverage ya media siyo ya kupuuza hata kidogo inasaidia sana kwa CCM
8. Kampeni ya kitanda kwa kitanda na uwepo wa matawi na mashina kwa chama cha CCM inawabeba sana kufikia ushindi. Hivyo wamekuwa na malengo ya muda mrefu ya kutafuta ushindi mengine siwezi kuyasma hapa kwa sababu za kimkakati na malengo ya muda mfupi yote yanabebana interchangebly.
8.Kwa ujumla vyama vya upinzani kwa kipindi hiki cha mwanzo vinaonekana kupoteana. Ni kama wanasindikiza tu au kukamilisha matakwa ya kikatiba bila kuwa na mwelekeo thabiti. Niseme CCM anashinda mapema tu bahati nzuri Mgombea uraisi wa Chadema amekiri leo mbele ya waandishi wa habari kuwa kazi ni nzito na kuwa wana changamoto ya fedha. Hii ni dalili ya kukubali kushindwa vinginevyo wabadilishe mbinu za mchezo na waanze pia kushawishi vyombo vya habari kuwatangaza badala ya mitandao ya kijamiii pekee. Kwa msingi huo wapinzani mkishindwa msilalamikie Tume ya uchaguzi kuwa uchaguzi haukuwa huru na haki hali ndiyo hiyo inajieleza yenyewe.
1. CCM imeweza kuwatumia makada wake kikamilifu walosambaa nchi nzima wakifanya kampeni kwa mpigo wakati wapinzani wamemwachia mgombea uraisi pekee kwa sasa.kwa mfano tumeona huko zanzibar juzi makada wengine wa Chadema hawakuwepo kabisa inaonekana wamejikita kwenye majimbo yao wakipigania uhai wao.
2. CCM wamaonekana kuwa wako makini - serious-kupambana kwelikweli kwa nguvu zote bila kupuuza chochote mbele yao na wakijibu hoja za wapinzani na hapohapo wakifafanua sera zao wakati wapinzani wanatumia muda mchache kuelezea sera zao na hususani kuelezea kwa kina udhaifu wa sera za chama tawala na madhara yake kiuchumi na ustawi wa jamii kwa kipindi cha muda mfupi na mrefu badala yake wanatoa hoja nyepesi.
3.CCM wanatumia saikolojia ya kujaza watu kwenye mikutano ili kujenga mob sychology kuonyesha kukubalika kwao kwa wananchi ili baadaye tarehe 28.9.2020 wapigiwe kura kwa imani kuwa hiki ndicho chama kinachokubalika na wengi na kwa kuchagizwa na propoganda sahihi
4.Wana uwezo kifedha na logistiki vitu ambavyo vimewarahisishia zaidi kuyafikia maeneo yote muhimu ya wilayani majimboni na vijijini.
5.Mikoa yenye kura nyingi ya kanda ya ziwa mgombea wao ameitumia vizuri fursa ya kujitangaza pamoja na wagombea ubunge na madiwani kwenye mikutano ya kampeni.Aidha ameweza kufukia mashimo ya waliachwa kwenye kura za maoni.
6.CCM inajitahidi kutoacha pengo au mwanya kwa wapinzani sasa hivi kusini kuna JK na Mama SAmia na kaskazini Waziri Mkuu wakati wapinzani hawaonekani kusambaa nchi nzima nguvu kubwa kila mmoja kwenye jimbo lake. Kutoka na uhaba wa fedha wameshindwa kusambaza nguvu kazi zao kusaidia majimboni.
7.Mgombea uraisi anaeleweka kwa lugha nyepesi kwa wananchi na anazungumzia maendeleo yanayoonekana. Hii inamwongezea hali ya kuaminika zaidi akipewa madaraka. Mbinu ya kutumia vikundi visivyoonekana,wanamuziki na coverage ya media siyo ya kupuuza hata kidogo inasaidia sana kwa CCM
8. Kampeni ya kitanda kwa kitanda na uwepo wa matawi na mashina kwa chama cha CCM inawabeba sana kufikia ushindi. Hivyo wamekuwa na malengo ya muda mrefu ya kutafuta ushindi mengine siwezi kuyasma hapa kwa sababu za kimkakati na malengo ya muda mfupi yote yanabebana interchangebly.
8.Kwa ujumla vyama vya upinzani kwa kipindi hiki cha mwanzo vinaonekana kupoteana. Ni kama wanasindikiza tu au kukamilisha matakwa ya kikatiba bila kuwa na mwelekeo thabiti. Niseme CCM anashinda mapema tu bahati nzuri Mgombea uraisi wa Chadema amekiri leo mbele ya waandishi wa habari kuwa kazi ni nzito na kuwa wana changamoto ya fedha. Hii ni dalili ya kukubali kushindwa vinginevyo wabadilishe mbinu za mchezo na waanze pia kushawishi vyombo vya habari kuwatangaza badala ya mitandao ya kijamiii pekee. Kwa msingi huo wapinzani mkishindwa msilalamikie Tume ya uchaguzi kuwa uchaguzi haukuwa huru na haki hali ndiyo hiyo inajieleza yenyewe.