Tathmini ya Mwaka mmoja: TANESCO ya Maharage Chande na January Makamba imefanikiwa kwenye jambo gani?

Leak

JF-Expert Member
Feb 22, 2012
52,187
42,013
Wasalaam wanajamvi!

Sasa ni zaidi ya mwaka mmoja tangu Mh Rais Samia achague mkurugenzi mkuu mpya wa TANESCO bwana Chande Maharage na baada ya hapo Waziri wa Nishati alivunja bodi ya tanesco na kuteua sura mpya ambayo alisema ni ya wataalam na wabobezi wanaojua biashara na ni weledi sana.

Waziri alikwenda mbali zaidi na kuweka wazi kuwa TANESCO ya sasa haitakuwa kama ile iliyopita kwani kwa sasa kila mtambo utafanyiwa matekebisho au matengenezo maana uko nyuma viongozi waliopita walizuia kufanyiwa matengenezo hivyo mitambo kulemewa kwa miaka mitano bila kufanyiwa marekebisho.

Mh Waziri na Mkurugenzi mkuu wa TANESCO walikwenda mbele zaidi na kusema wanakuja na tenesco ya kidijitali na inayojali wateja maana yake wateja watafungiwa umeme kwa haraka sana na umeme hautokatika katika kwani mitambo itafanyiwa matengenezo kila wakati.

Je, baada ya mwaka mmoja na zaidi ni kweli tuliyo ahidiwa na Makamba na Maharage yamefanikiwa?

Ni mchango wa wataalam wapya waliowekwa na Makamba kwenye bodi?

Ni mchango gani wa wafanya biashara walio wekwa kwenye bodi ya tanesco?

Tanesco ya January Makamaba na Maharage Chande imefanikiwa kwenye nini?
 
Wasalaam wanajamvi!

Sasa ni zaidi ya mwaka mmoja tangu Mh Rais Samia achague mkurugenzi mkuu mpya wa Tanesco bwana Chande Maharage na baada ya hapo Waziri wa Nishati alivunja bodi ya tanesco na kuteua sura mpya ambayo alisema ni ya wataalam na wabobezi wanaojua biashara na ni weledi sana.
Hakuna chochote cha maana zaidi ya kuongeza maumivu. Watu kwa sasa wanaona ni bora wajichange kununua umeme wa solar kuliko kuomba wa Tanesco...
 
Ajirini wachina katika shirika la Tanesco katika ngazi za juu na wataalamu wa kutosha katika shirika. Alafu njoo hapa baada ya miaka 20+ uje uone mahali Tanesco itafika Afrika na duniani kiujumla.

state-grid-corporation-of-china-logo-business-electrical-grid-png-favpng-7Gg7DNgRQigcHXUmZG85J...jpg
Screenshot_20220914-103430.jpg
Globo_Top10Empresas_p11.jpg
 
Hakuna kitu, ukiona mtu mzima mpaka anasema watu waende wamuue tu ujue kashindwa. Makamba ni bright ila kosa lake ni kumdharau na kumdhihaki Dkt Magufuli.

Aiseeeer
 
Baada ya umeme kukatika masaa matatu tena bila taarifa ndio nakutana na hii.

1.Gharama za kuunganisha umeme zimepaa
2.Gharama za unit zimepaa.
3.Tozo ya jengo kwenye umeme, kilio kwa wengi.
4.Mfumo umekodishwa kwa mabilioni ya pesa.
5.Umeme kukatika katika kumezidi tena bila taarifa rasmi.
6.Project ya hydroelectric pale imekwama.
 
Wasalaam wanajamvi!

Sasa ni zaidi ya mwaka mmoja tangu Mh Rais Samia achague mkurugenzi mkuu mpya wa TANESCO bwana Chande Maharage na baada ya hapo Waziri wa Nishati alivunja bodi ya tanesco na kuteua sura mpya ambayo alisema ni ya wataalam na wabobezi wanaojua biashara na ni weledi sana.

Waziri alikwenda mbali zaidi na kuweka wazi kuwa TANESCO ya sasa haitakuwa kama ile iliyopita kwani kwa sasa kila mtambo utafanyiwa matekebisho au matengenezo maana uko nyuma viongozi waliopita walizuia kufanyiwa matengenezo hivyo mitambo kulemewa kwa miaka mitano bila kufanyiwa marekebisho.

Mh Waziri na Mkurugenzi mkuu wa TANESCO walikwenda mbele zaidi na kusema wanakuja na tenesco ya kidijitali na inayojali wateja maana yake wateja watafungiwa umeme kwa haraka sana na umeme hautokatika katika kwani mitambo itafanyiwa matengenezo kila wakati.

Je, baada ya mwaka mmoja na zaidi ni kweli tuliyo ahidiwa na Makamba na Maharage yamefanikiwa?

Ni mchango wa wataalam wapya waliowekwa na Makamba kwenye bodi?

Ni mchango gani wa wafanya biashara walio wekwa kwenye bodi ya tanesco?

Tanesco ya January Makamaba na Maharage Chande imefanikiwa kwenye nini?
Hayo ni majizi yamewekwa kimkakati,mbaya zaidi mkuu wa nchi kazingwa ,haoni lolote
 
Back
Top Bottom