Elli
Platinum Member
- Mar 17, 2008
- 55,484
- 86,000
Wadau,
Ni almost miezi Tisa tangu Tanzania ifanye uchaguzi wa serikali za mitaa. Kama mtakumbuka, uchaguzi huu uligubikwa na kila aina ya hila na vituko.
Matukio kabla ya Uchaguzi
Miongoni mwa matukio ya makubwa ilikua ni pamoja na kuenguliwa kwa Wagombea wa upinzani kwa kigezo cha kukosea kujaza form, almost 90% ya Wapinzani waliondolewa kwa kigezo hicho!
Matukio ya rushwa na figisu za hapa na pale, rejea tukio la yule Mama (kiongozi wa CCM aliyerekodiwa akieleza jinsi walivyomfitini mgombea mwingine akajisahau kuwa huyo anayemweleza ndio huyo mhusika aliyeenguliwa)
Rushwa pia ilitamalaki sana sana, matukio haya yalitawala kimya kimya na kwa waziwazi. Si kesi.
Tukio kubwa zaidi ilikua ni hotuba ya H.E Freeman Mbowe kuwa Wapinzani wajitoe, ilikua ni tamko fupi sana lakini kilikua na impact kubwa sana maana inasadikika kuwa hadi Viongozi wa Serikali pia hawakupiga kura.
Hali hii iliwalazimu Serikali kutoa Waraka wa "kuwataka" waajiriwa kwenda kupiga kura na ukweli ni kwamba hawakwenda!
Matukio ni mengi mtanisaidia, turudi sasa kwenye tathmini ambayo ni fupi sana na iko kwenye mfumo wa swali kama ifuatavyo.
Kumekua na "mitazamo" kuwa Wapinzani na siasa zao za "kupinga kila kitu" ndio zinakwamisha Maendeleo. Sasa majibu yenu hapa ndio yatatoa tathmini halisi.
Je, miezi Tisa baada ya Uchaguzi ambapo Serikali walijitangazia Ushindi wa 99% Kuna Maendeleo gani yanefanyika?
Kuna mabadiliko yoyote mazuri tunaweza kujivunia kwa kua Serikali zote (Sm) zinaongozwa na CCM? Mifumo ya uendeshaji mambo kwenye serikali za mitaa umeimairika? Kero za Wanachi zimeshughulikiwa?
Je, ni kweli Upinzani ndio tatizo au ni mfumo ndio mbovu?
Karibuni kwa hoja nzito, huu mjadala sio kwa Watoto, wasaka tonge, vibaraka, au wasiojitambua
Ni almost miezi Tisa tangu Tanzania ifanye uchaguzi wa serikali za mitaa. Kama mtakumbuka, uchaguzi huu uligubikwa na kila aina ya hila na vituko.
Matukio kabla ya Uchaguzi
Miongoni mwa matukio ya makubwa ilikua ni pamoja na kuenguliwa kwa Wagombea wa upinzani kwa kigezo cha kukosea kujaza form, almost 90% ya Wapinzani waliondolewa kwa kigezo hicho!
Matukio ya rushwa na figisu za hapa na pale, rejea tukio la yule Mama (kiongozi wa CCM aliyerekodiwa akieleza jinsi walivyomfitini mgombea mwingine akajisahau kuwa huyo anayemweleza ndio huyo mhusika aliyeenguliwa)
Rushwa pia ilitamalaki sana sana, matukio haya yalitawala kimya kimya na kwa waziwazi. Si kesi.
Tukio kubwa zaidi ilikua ni hotuba ya H.E Freeman Mbowe kuwa Wapinzani wajitoe, ilikua ni tamko fupi sana lakini kilikua na impact kubwa sana maana inasadikika kuwa hadi Viongozi wa Serikali pia hawakupiga kura.
Hali hii iliwalazimu Serikali kutoa Waraka wa "kuwataka" waajiriwa kwenda kupiga kura na ukweli ni kwamba hawakwenda!
Matukio ni mengi mtanisaidia, turudi sasa kwenye tathmini ambayo ni fupi sana na iko kwenye mfumo wa swali kama ifuatavyo.
Kumekua na "mitazamo" kuwa Wapinzani na siasa zao za "kupinga kila kitu" ndio zinakwamisha Maendeleo. Sasa majibu yenu hapa ndio yatatoa tathmini halisi.
Je, miezi Tisa baada ya Uchaguzi ambapo Serikali walijitangazia Ushindi wa 99% Kuna Maendeleo gani yanefanyika?
Kuna mabadiliko yoyote mazuri tunaweza kujivunia kwa kua Serikali zote (Sm) zinaongozwa na CCM? Mifumo ya uendeshaji mambo kwenye serikali za mitaa umeimairika? Kero za Wanachi zimeshughulikiwa?
Je, ni kweli Upinzani ndio tatizo au ni mfumo ndio mbovu?
Karibuni kwa hoja nzito, huu mjadala sio kwa Watoto, wasaka tonge, vibaraka, au wasiojitambua