Tathmini: Matokeo ya Uchaguzi wa Udiwani uliofanyika Februari 9, 2014

Hivi kweli mkuu unaamini ccm wanaweza kushiriki uchaguzi bila ujanja wowote?Hivi uingie kwenye mtihani ambao majibu unatunza mwenyewe na kusahihisha unasahihisha wewe na matokeo unatangaza wewe, halafu ujipe F.Inawezekana?
Mkuu naamini hoja yako. Na pia nimeona mojawapo ya marungu ambayo ccm inafaidika nayo kwa sasa ni Daftari la wapiga kura kutoboreshwa. Ninaamini kuna vijana wengi sana waliokuwa na umri kati ya miaka 15-17 wakati wa uandikishwaji wa mara ya mwisho ambao leo wangeweza kupiga kura lakini hawana nafasi hiyo. Ni kweli watajazana kwenye mikutano ya chadema na hata kushangilia kwa hamasa lakini wakati wa kutumia sanduku la kura kutimiza haki yao nafasi hiyo hawana. Daftari la wapiga kura sio Rungu pekee lakini ni mojawapo ya mengi ambayo CCM wanayo. Kibinafsi nimechoka na utawala wa CCM na ninatamani mabadiliko.
 
Itanichukua miaka kuamini watanzania wanawapigia kura CCM....

CCM ni chama dola ina mbinu nyingi sana za kulazimisha ushindi....

Wanatengeneza mazingira ya kuonyesha wao wanapigiwa kura kumbe laa!

Kwamfano huko Arusha- Sombetini siamini kabisa hizo kura walizopata.

CCM wanahakikisha morale ta wapiga kura haipandi hata siku moja hivyo wapo tayari kwa lolote ilimradi isionekane kwa vitendo upinzani unakua...Hiki kinawahakikishia wao wanaendelea kumanipulate kura. Naamini siku CCM wakishindwa ku manipulate kura kwa njia zake zote watakuwatayari kuilinda dola yao kwa ncha ya upanga....kwa wengi wao wenye nguvu hawajui maisha nengine zaidi ua kuitumia dola kupata kila wanachokihitaji!
Una haki na imani yako hata kama inakupotosha.ukweli unabaki palepale.CCM ina watu wengi wanayoiunga mkono.sio watu wa kelele nyingi.hivi kweli uliamini watu waliokuja kuangalia chopa wangewapigia kura.elew mwendo ni huu huu 2015
 
Pokea LIKE mkuu.Chadema someni na mfanyie kazi maoni ya ndugu Mayenga
Kulikuwa na bwana mmoja aliyepewa jiwe kubwa sana ambalo aliambiwa akiliponda likapasuka vipande vipande,atapata dhahabu.Bwana huyu baada ya kuponda jiwe lile mara miamoja,alikata tamaa,akaghafirika na kutupa nyundo chini na kuondoka.Mwingine aliyekuja aliponda nyundo moja tu na jiwe lile likapasuka vipande vipande,hatua moja au mpondo mmoja ulimkosesha yule bwana dhahabu.

Ni kwamba,katika hatua yoyote ya maisha,hatuna budi kujua changamoto na matatizo ni njia ya kuelekea kwenye neema.Hakika mwisho wa kitu,kiwe kizuri au kibaya hauji upesi.Kazi ambayo imeshafanywa na Chadema ni kubwa.Wenye kukata tamaa na kile wanachoona kimefanyika au na matokeo yaliyotangazwa,ni watu wabaya sana.Si watu wema,hawajui uchungu wa mapambano.Wengi wetu tunafanya maamuzi nyuma ya keyboards zetu,na kamwe hatuna uthubutu wa kujua kiwango cha mapambano.

Uchaguzi huu ukipimwa kwa mizania ya kisayansi,ni ukweli usiopingika kuwa Chadema ndio washindi and CCM stand loosers!! Bilioni moja ukiondoa shilingi moja si bilioni tena,tutaiita bilioni moja kasoro,Shilingi mbili ukiongeza Sh moja,pesa hiyo inakuwa imeongezeka.Katika hili CCM wakati wanatafakari kuzipoteza kata zao,CDM hawatafakari maumivu wanatafakari kwanini hawakuongeza zaidi.Haya ni mambo mawili tofauti.

Katika uhalisia wa mambo unavyokwenda,haya si matokeo ya chama chochote kujitapa,ni kujitafakari na kuchukua hatua.Niliwahi kuandika hapa jamvini,kuwa bila ya chadema kufanya decentralization,hali itaendelea kuwa hivi hivi.Nakumbuka huko kwetu kuna kijiji ambacho hata gari hawajawahi kuliona na mpaka sasa wanajua rais ni nyerere.Lakini mfumo wa uongozi ulio katika kijiji kile umejikita mizizi sana.Haiwezekani CDM mtake kila kijiji na matawi yote yamjue Dr.Slaa na Mbowe.Hebu vifanye vijiji,matawi na mashina yawe na imani na uongozi wa mahali pale.Wape uwezo hawa viongozi wa chini,wanyweshe majina ya bendera kama CCM walivyofanya.Nina babu yangu mpaka leo ukimwambia kwanini unaipenda CCM hana zaidi ya kusema kuwa ni kwa sababu ilileta uhuru.Hakuna cha ziada walichonacho watu juu ya ccm,haiwezekani mindset ya watu ikabadilika kwa chopa inayotua kwa masaa kadhaa,lazima mabadiliko yafanywe.

CDM punguzeni centralization,decentralize the party na nguvu ya umma inayohubiriwa ionekane.

Ni hayo tu!
 
Tunasikitika na ni haki yetu kufanya hivyo.CHADEMA LAZIMA WAJITOFAUTISHE NA CCM KIMATENDO.NGUVU ZOTE HIYO HAIJAKIPATIA CHAMA KATA YA ZIADA HATA MOJA?HADI KITETO AMBAKO RAIA WANAUANA KWA SABABU YA CCM?Maana yake hamna watu makini wa chama kwenye grassroot au nn? Hangover?
Habari wakuu,

Naomba wana-CHADEMA msiumize vichwa kuhusu huu ushindi wa CCM.Msidhani CCM inakubalika au inapendwa sana na wananchi.

Watanzania wataipenda CCM kwa vipi wakati kila siku wanalia na maisha magumu,ufisadi,mishahara midogo,bei za umeme,shida za maji,huduma mbovu za afya,ubovu wa miundo mbinu,migogoro ya wakulima na wafugaji,unyanyasaji wa polisi n.k

Wanachofanya watanzania kwa sasa ni kuchagua "mwenye chongo katika jamii ya vipofu awaongoze njia".Ndio maana watu wengi leo hii hawapigi kura kwani wamekata tamaa kabisa.Wasiopiga kura wengi wao ni wana CCM wanaona hakuna tena maana ya kuchagua viongozi.

Wapinzani kwa sasa mnachotakiwa ni kuonyesha kwa vitendo tofauti yenu na CCM.

Wapinzani,all you need to do is to walk the walk.

Mnapinga posho huku mnazichukua,mnapinga mashangingi wakati kiongozi wa kambi ya upinzani anatumia shangingi,mnaambiwa muungane hamtaki,vita ya madaraka katika vyama vya siasa hakuishii,boresheni na kujali viongozi na ofisi katika ngazi za chini hamtaki n.k

Wapinzani,wananchi bado wamewaweka katila "probation".

NB:Ingawa CCM ni wabovu,watanzania wengi wana hofu ya kufanya "majaribio" katika uongonzi wa nchi na hivyo wanaona ni bora "mwenye chongo katika jamii ya vipofu"
 
Hii inaitwa KO yaani raundi ya kwanza tu,leteni hekaya zenu,hadithi zenu mwisho mmeangukia pua,na 2015 ndio mwisho wa baadhi ya member kuwa hapa jukwaani kwa aibu
 
Chadema ni genge la wahuni haliwezi kuimarika.... Dr mwenyewe alishasema genge haliko imara.
 
una maana sasa ni mwaka 2014 + 20 maana yake walau 2034 ndio watakuwa tayari? mbowe anaenda 60 maana yake atakuwa anaenda 80 vongozi wengine sijui.
 
Mwlm nyerere hakuleta uhuru kwa siku 1 wenzenu wakishangilia kwa kuona wameshinda ninyi fanyeni kazi pangeni mikakati madhubuti, nyerere wakati mwingine ilionekana kama anashindwa na wakoloni, nawakoloni walikua wakijipongeza, wakati nyerere alikua akipanga mikakati na kikosikazi chake na mwisho wa siku wakoloni walishindwa, wito wangu kwa viongozi ni kujipanga na kuzidisha mikakati madhubuti,kuboresha kanda zote kupeleka vitendea kazi kila kanda kupanga timu imara kila kanda na kujenga chama na kukieneza kwa nguvu kubwa, kuwa tibu wananchi na ugonjwa wa kutokupiga kura,yaani kutoa elim ya uraia, na kujipanga kwa uchaguzi wa serikali za mitaa na uchanguzi mkuu,nashauri kiundwa kikosi kazi ambacho kitapita kanda zote 10 na kujenga chama kwa muda uhu mchache ulio baki, hakuna kulala mpaka kieleweke, kuwekeza nguvu kwenye mkakati wa chadema ndio msingi, hakuna ushindi kwa maandalizi hafifu nilazima chama kijizatiti kweli kweli kuelekea 2015,kushurutisha tume ya uchaguzi iboreshe daftari la wapiga kura na kudai tume huru ya uchaguzi,mwisho na wapongeza ccm kwa matokeo ya jana,iyo ndio demokrasia, naomba kuwasilisha,asatnteni,
 
Chadema walidhani kwa umaarufu walioupata wanaweza kuwatupa wowote wasioendana na mawazo ya mbowe. Haya ni malipo ya dhambi ya kusaliti michango ya wengine na kuwatwisha madhambi yasiyo yao mara wasaliti mara vile. Bilion na helkpta zote kumbe ilikuwa ni political tour tu. Mfa maji haishi kutapa tapa wasisingizie daftrari kuboreshwa kwa sababu kata walizoshinda daftari halikuboreshwa na vilevile hata ambao wangeandikishwa wasingezid hawa walioandikishwa possibly haizid 10% ya waliondikishwa na sababu kubwa zaid wanahitaji uwezo wa kushawishi hata katika hawa waliopo ili washinde through hawa. Kwani wana uhakika gani kama wapya wangeandikishwa ndo wangeipigia chadema kama waliopo wameshindwa? Ni aibu matumiz ya mbwembwe aafu unaambulia kata hizo tu aafu bado unaota kuchukua nchi. Ni kweli matatizo ndani ya ccm yamezd ila chadema wanahitaji kujipanga upya kwa mwendo wataimba tunachakachuliwa milele. Matokeo ya akili ndogo kutawala akili kubwa
 
Wasubr sana chama siasa kikiwa taasis ya watu hata siku hakiwezi kushika dola. Kama chama wamekihodhi na kufanya cha familia na sehemu ya kuchumia hela na kupatia mahawara kwa kuwaonga viti maalumu, wakipewa nchi si watajimilikisha mpaka magenge ya watu?
 
Baada ya matokeo yote kutangazwa,kata 27 kati ya hizo ccm imeshinda kata 23,chadema 3,nccr mageuzi 1 ni ishara tosha kuwa chadema bado ni chama kichanga kinakuwa na imefika hatuwa kipo dormant hakikui tena,na inaonesha ccm wakiwabana watendaji serikalini wataongza miaka mingi kama kile chama tawala cha
africa kusini au cha zimbabwe.,ccm inatakiwa iwabane watedaji wazembe wataongoza miongo mingi sana.....
 
BAO LA kisigino!!Kuna matatizo 7 ambayo CHADEMA bado hawayafahamu:

1. Hawajui priority ya matatizo ya watanzania

2. M4C imekuwa na propaganda zaidi kuliko kuwa na idiolojia ya kudumu juu ya kile kinacholenga kutatua matatizo ya watanzania. Hivyo imekipaka matope zaidi chama kuliko kukijenga, kwani watanzania wanaona kama mchezo wa kuigiza. Na ndio maana Zitto hakushabikia wala kushiriki katika M4C.

3. CHADEMA wanadhani watanzania ni WAJINGA/MAJINGA ya kudanganya danganya tu. Hili ni kosa kubwa.

4. Ukabila na Udini

5. Kutoelewa DEMOKRASIA. (Hili ni tatizo kubwa sana, halitatuliwa leo wala kesho). Kwa maana hiyo kuwapendekeza wagombea wasionamvuta kwa wananchi. Hii ni pamoja na uchaguzi wa ndani ya chama na nje(udiwani/ubunge) hata uwakilishi mbali mbali.

6. Mgao wa Ruzuku.

7. Kudhani kuwa Fujo, mapigano, vurugu ndio siasa zinazohitajika Tanzania. Wakati mwingine wakisema hadharani kuwa watanzania ni WAOGA.

Na kwa hayo, ndio sababu kubwa ya wananchi kutojitokeza katika kupiga kura. Kwani walikuwa na imani sana na CHADEMA, na imewafikisha pabaya na wala hawanahaja na CCM. Hawa wamechagua kususia uchaguzi.

! Matokeo haya ni taswira tosha juu ya uchaguzi mkuu 2015. Awe Slaa, Mbowe , pindi wataposhindwa wasizingizie kuwa wamepigwa bao, bali hiyo ndio itakuwa hali halisi. Tena mgombea wa urais wa CHADEMA akipata 10% ashukuru Mungu
 
Baada ya matokeo yote kutangazwa,kata 27 kati ya hizo ccm imeshinda kata 23,chadema 3,nccr mageuzi 1 ni ishara tosha kuwa chadema bado ni chama kichanga kinakuwa na imefika hatuwa kipo dormant hakikui tena,na inaonesha ccm wakiwabana watendaji serikalini wataongza miaka mingi kama kile chama tawala cha
africa kusini au cha zimbabwe.,ccm inatakiwa iwabane watedaji wazembe wataongoza miongo mingi sana.....

CCM haina uwezo wa kuwabana watendaji Wazembe.Mtu anayelipwa Mshahara chini ya Tshs.200,000/=kwa Mwezi sawa na Dola 15 atawezaje kufanya kazi kwa ufanisi kama sio kugeuza Ofisi ya Serikali kuwa Sehemu ya Kupigia Dili zake.
 
Back
Top Bottom