Tathmini: Kuzuia shughuli za kisiasa mpaka 2020 haiwezekani

MAHANJU

JF-Expert Member
Aug 26, 2014
5,244
7,966
Katiba ya jamhuri ya Muungano wa Tanzania inavipa vyama vyote vya siasa nchini kufanya shughuli za kisiasa ikiwa ni pamoja na kufungua matawi maeneo mbali mbali, kukagua uhai wa chama, kuwashawishi wananchi ili kupata uungwaji mkono.

Vyama vya siasa pia vina haki ya kikatiba kutoa elimu kuhusu utekelezaji wa sera mbali mbali unaofanywa na serikali, vyama vya siasa vinavyo wajibu hata wa kutoa elimu ya uraia, vyama vya siasa vinavyo wajibu wa kotoa elimu ya katiba kwa wananchi.

Kabla ya kufikia uchaguzi mwingine ni lazima chama cha siasa kihakikishe kua kinajiandaa kwa kutafuta wapiga kura katika maeneo mbali mbali ya nchi ili itakapofika muda wa kampeni basi itakua ni rahisi kuwafikia wafuasi wake.Kuna idadi ya wanachama ambao chama kinatakiwa kua nao ili kukidhi matakwa ya kisheria kua na sifa ya kua chama cha siasa.

Ikumbukwe kua kila chama kina misingi yake kuanzia ngazi za chini, katika ile misingi hua kuna wasimamizi wake ambao ndio viongozi wasimamizi wa ustawi wa chama husika. Lazima viongozi wa kitaifa wapate muda wa kupitia katika misingi ya vyama vyao ili kuendelea kuwajengea uwezo wasimamizi wa misingi hiyo. Kwahiyo muda wa kufanya siasa hauna kikomo wala muda maalum, ni nafasi tu ya chama chenyewe kulingana na uwezo wake.

Kazi nyingine ya vyama vya siasa kwa sababu katiba inaruhusu kuunda serikali kivuli kwa chama chenye wabunge wengi baada ya chama tawala, ni lazima viikosoe serikali iliyoko madarakani pale panapohitaji kukosolewa. Mataifa yote yenye mfumo wa vyama ni kawaida sana kwa upinzani kuikosoa serikali.

Isichukuliwe kama kukosolewa serikali na upinzani ni kukwamisha maendeleo! Sijawahi kusikia kwa taifa la Marekani limekwama kimaendeleo sababu tu kwamba vyama vya upinzani vilikua vikifanya mikutano. Nchi za wenzetu siasa inafanyika na maendeleo ni makubwa sana tu.Suala ni kuangalia ni wapi tulijikwa na kurekebisha kasoro zilizopo lakini sio kuzuia vyama vya upinzani kufanya siasa.

Hivyo basi, ni jambo jema sana kuviachia vyama vya kisiasa kuendelea na majukumu yake ya kisiasa kwa sababu chama chenyewe ndio siasa, na huu ndio mzizi wa kujenga mshikamano na umoja wa watu katika taifa linalotaka kuendelea.Hii ndio inayoitwa demokrasia ya vyama vingi.Haya yote yanawezekana Kama vuguvugu la vyama vingi silingekuepo ndani ya taifa letu.

Nchi yoyote duniani ambayo haijatulia kisiasa(Political instability) vyanzo vyake kwa kiasi kikubwa hutokana na ukosefu wa demokrasia na hapo ndipo vikundi vyenye nia ovu hapata nafasi ya kupenya na kusababisha vurugu.
 
Wewe umeongea hayo ukizingatia Katiba ya nchi ambayo viongozi wa nchi waliapa kuilinda, lakini jiulize swali moja tu dogo, hivi anapotokea Mkuu wa nchi na kutangaza hadharani kuwa mikutano yoyote ya kisiasa na shughuli nyingine za kisiasa zisitishwe hadi mwaka 2020.

Hivi kiongozi wa aina hiyo ni kweli ameamua kuilinda Katiba yetu kama alivyokula kiapo au ameamua kuisigina?

Mwalimu Nyerere enzi za uhai wake aliwahi kusema kuwa Rais wa nchi ndiye mtu anayestahili kuwa mstari wa mbele kuilinda Katiba.

Anapotokea Rais ambaye hataki kuilinda Katiba tuliyo nayo alitamka waziwazi Mwalimu kuwa Rais wa namna hiyo hatufai.....
 
Kwa trend ninayoiona inayokwenda nayo serikali ya awamu ya 5 naona hakuna kazi itakayokuwa ngumu kama ya Uas...kari.

Kwa kuwa ethics za Usoja ni kupokea amri toka 'juu' na kuzitekeleza, bila 'kutafakari' na kujiridhisha kuwa amri hiyo uliyopokea ni halali au laa.....
 
1466901125053.jpg
 
Kuzuia kufanya siasa ni masihara na upuuzi maana hata yeye anafanya mchakato wa uenyekiti wa CCM (siasa) na ni mwakani tu chama kitafanya uchaguzi kwa mwaka mzima. 2019 ni uchaguzi S/mitaa.
 
JPM anaminya demokrasia anachotaka ni kusifiwa tu. Kweli atasifiwa kwa mema na busara lakini akiboronga lazima aambiwe tu, mzee (baba j) hapa umekunya
 
Wewe umeongea hayo ukizingatia Katiba ya nchi ambayo viongozi wa nchi waliapa kuilinda, lakini jiulize swali moja tu dogo, hivi anapotokea Mkuu wa nchi na kutangaza hadharani kuwa mikutano yoyote ya kisiasa na shughuli nyingine za kisiasa zisitishwe hadi mwaka 2020.

Hivi kiongozi wa aina ni kweli ameamua kuilinda Katiba yetu kama alivyokula kiapo au ameamua kuisigina?

Mwalimu Nyerere enzi za uhai wake aliwahi kusema kuwa Rais wa nchi ndiye mtu anayestahili kuwa mstari wa mbele kuilinda Katiba.

Anapotokea Rais ambaye hataki kuilinda Katiba tuliyo nayo alitamka waziwazi Mwalimu kuwa Rais wa namna hiyo hatufai.....
Kwa maoni yangu binafsi nafikiri kabla ya maamuzi ungefanyika utafiti kujua kama shughuli za kisiasa kwa mujibu wa katiba zinaathiri maendeleo, kuliko kuacha baadhi ya askari wetu kuapa kula sahani moja na vyama vya siasa.
 
Kwa trend ninayoiona inayokwenda nayo serikali ya awamu ya 5 naona hakuna kazi itakayokuwa ngumu kama ya Uas...kari.

Kwa kuwa ethics za Usoja ni kupokea amri toka 'juu' na kuzitekeleza, bila 'kutafakari' na kujiridhisha kuwa amri hiyo uliyopokea ni halali au laa.....
Kuna makundi ambayo hua hayana nia njema na nchi yetu yanapoona hakuna utulivu hutumia nafasi hiyo kujipenyeza.
 
Sheria namba 11 (1) (a) ya vyama vya siasa inavipa vyama haki ya kufanya mikutano ya KISIASA ili KUJINADI na KUTAFUTA WANACHAMA wapya.
Bila kuwa na Wanachama wapya vyama haviwezi Kukua.

Pili kuna vyama havina mbunge hata mmoja na wala havijulikani, leo kuviambia visubiri Five Years ndo vifanye Siasa ni Sawa na Kumwambia mwanafunzi asubiri NECTA ndo asome, Hili haliwezekani!

Pia kuna hoja eti watu wafanye Siasa ktk majimbo yao, Kuna vyama havina Mbunge hata mmoja, Je wao wakafanyie wapi Siasa?

Kuna vyama vina Mbunge mmoja, je mnataka vyama hivyo vikafanye siasa katika jimbo hilohilo moja?, Vitakua lini?, Tukifanya hivi hamuoni kuwa vyama vitakuwa vya kikanda?

All in all Katiba imetoa Freedom of Assembly ili mradi hauvunji sheria. Tamko la kufanya Siasa after 5 years halina msingi katika kifungu chochote cha sheria na hivyo inabaki kuwa Opinion.
 
JPM anaminya demokrasia anachotaka ni kusifiwa tu. Kweli atasifiwa kwa mema na busara lakini akiboronga lazima aambiwe tu, mzee (baba j) hapa umekunya
Kibaya zaidi wakati Magu anawapiga STOP vyama vya siasa vya upinzani visifanye mikutano yoyote ya kisiasa wala hata mikutano yao ya ndani hadi mwaka 2020, wao CCM wanaendelea Kufanya siasa kwa mwendokasi.

Taifa tumetangaziwa kuwa mwezi ujao CCM watakuwa na mkutano wao Mkuu.

Sasa kama Polisi nao hawatapiga STOP mkutano huo kutokana na maelekezo aliyoyatoa Mkuu wa nchi, hapo ndipo tutakapoona double standard ya hali ya juu ya utendaji kazi wa Jeshi letu la Polisi.

Kama Jeshi hilo lilidiriki hata kutumia magari ya washawasha kuzuia hata sherehe za Mahafali za wanachuo wa Chaso mikoani Dodoma, Kilimanjaro na Morogoro ambapo ni mikutano ya ndani, iweje Jeshi hilo hilo lipate 'kigugumizi :cha kuzuia mkutano Mkuu wa CCM wa mwezi ujao?!
 
Hivi na ruzuku za kila mwezi kwa vyama vya siasa, bado zitaendelea kutolewa, au nazo zimesitishwa hadi 2020?
 
Anapenda sana sifa, ameanza kudharau katiba iliyomuweka hapo alipo, anatumia kigezo cha kuwatumikia wananchi kukanyaga katiba
 
Hivi na ruzuku za kila mwezi kwa vyama vya siasa, bado zitaendelea kutolewa, au nazo zimesitishwa hadi 2020?
Malengo makubwa ya ruzuku ni kujiimarisha chama. Sijui kwa sasa zitakua na kazi gani.
 
Kibaya zaidi wakati Magu anawapiga STOP vyama vya siasa vya upinzani visifanye mikutano yoyote ya kisiasa wala hata mikutano yao ya ndani hadi mwaka 2020, wao CCM wanaendelea Kufanya siasa kwa mwendokasi.

Taifa tumetangaziwa kuwa mwezi ujao CCM watakuwa na mkutano wao Mkuu.

Sasa kama Polisi nao hawatapiga STOP mkutano huo kutokana na maelekezo aliyoyatoa Mkuu wa nchi, hapo ndipo tutakapoona double standard ya hali ya juu ya utendaji kazi wa Jeshi letu la Polisi.

Kama Jeshi hilo lilidiriki hata kutumia magari ya washawasha kuzuia hata sherehe za Mahafali za wanachuo wa Chaso mikoani Dodoma, Kilimanjaro na Morogoro ambapo ni mikutano ya ndani, iweje Jeshi hilo hilo lipate 'kigugumizi :cha kuzuia mkutano Mkuu wa CCM wa mwezi ujao?!
CCM wanao uwezo wa kufanya siasa kwa gia ya kukagua utekelezaji wa ilani ya Chama. Pia wakuu wa wilaya na mikoa wote kazi zao kubwa hua ni kufanya siasa kama mawakala wa chama wanao mwakilisha mkuu wa nchi.
 
Sheria namba 11 (1) (a) ya vyama vya siasa inavipa vyama haki ya kufanya mikutano ya KISIASA ili KUJINADI na KUTAFUTA WANACHAMA wapya.
Bila kuwa na Wanachama wapya vyama haviwezi Kukua.

Pili kuna vyama havina mbunge hata mmoja na wala havijulikani, leo kuviambia visubiri Five Years ndo vifanye Siasa ni Sawa na Kumwambia mwanafunzi asubiri NECTA ndo asome, Hili haliwezekani!

Pia kuna hoja eti watu wafanye Siasa ktk majimbo yao, Kuna vyama havina Mbunge hata mmoja, Je wao wakafanyie wapi Siasa?

Kuna vyama vina Mbunge mmoja, je mnataka vyama hivyo vikafanye siasa katika jimbo hilohilo moja?, Vitakua lini?, Tukifanya hivi hamuoni kuwa vyama vitakuwa vya kikanda?

All in all Katiba imetoa Freedom of Assembly ili mradi hauvunji sheria. Tamko la kufanya Siasa after 5 years halina msingi katika kifungu chochote cha sheria na hivyo inabaki kuwa Opinion.
Mkuu hili suala ni gumu sana, halihitaji hasira. Ni busara pekee ndio zinazotosha.
 
Mbona jana Rais kashukuru wananchi kwa kuacha kazi zao na kwenda ktk mkutatano wake wa kisiasa pale Kinondoni. Wanasiasa waliitwa pale kusalimia wananchi, wasio kuwepo walilaumiwa kwa kutofika sasa unawezaje kuzuia au kusimamisha siasa wakati ni shuguli za kila siku?

Siasa ni Pana hakuna anayeweza kuizuia, inaanzia ktk mtu binafsi, familia na kuendelea.

Lakini pia utekelezaji wa shughuli zote za kiserikali na mipango mbali mbali inahusisha siasa. Labda tatizo liwe kujua nini maana ya SIASA?
 
lakini kumbuken hivi; wkt anaepkea fmu pl Dom alisema at ANaenda KUJARiBU baHAtI yaKE; hii inamaanisha kuwa hakuwa tayar kuwatumikia wanch! na likuw ni zali lake 2! so natabir AnGK LKe sOOn!
 
Back
Top Bottom