Mabibi na mabwana ni ukweli usiopingika kuwa kesho yetu iliyo bora zaidi inategemea sana uwepo wa katiba mpya. Kwa hali tuliyofikia kunahitajika zaidi mustakabala mpya wa utangamano. Ni wazi kuwa hayupo mmoja ambaye kwa dhati yake asiyekwazika kabisa kwa lolote na katiba iliyopo labda tu, kwa kutokujua au kuwa mnufaika wa moja kwa moja na mapungufu ya katiba hii tuliyo nayo sasa.
Si Mataga, si CCM, si CUF, si ACT, si Chadema nk. Ni chama gani kwa dhati yao wanaishabikia katiba hii kuwa ndiyo mustakabala bora kabisa tunayoistahili?
Si manguli wa siasa wakiwamo kina Bashiru, kina Pole pole, Warioba, Butiku, nk wote hao wangependa uwepo wa katiba nyingine. Wala si hii ambayo ni wazi kuwa wengine katika hawa bila ya kutarajia kwa katiba hii, wamejikuta wakivunjika mioyo ghafla na kweli kweli. Hawakujua kuwa walistahili katiba mpya mapema, lakini sasa wanajua. Jambo la kheri tu.
Kundi pekee linaloishabikia katiba iliyopo kwa dhati (kuacha mambumbu) ni dogo sana na hili ni lile tu linalonufaika madarakani moja kwa moja kibinafsi kutokana na katiba iliyopo. Hawa wala si wengi kuvihimili vishindo vya watakao mabadiliko.
Kizingiti pekee kilichopo kuifikia azma hii inayotakikana na wengi ni kukosekana kwa umoja. Ni vipi Mataga wa CCM na CCM yenyewe iweze kushirikiana na vyama vingine kama Chadema kudai katiba mpya? Hilo haliwezekani japo wote Chadema na CCM wakiwamo Mataga wanaihitaji mno katiba mpya yenye kuwapa wote uhakika zaidi wa kesho.
CCM kushirikiana na wengine kwenye hili, ni rahisi zaidi kwa Ngamia kupita kwenye tundu la sindano. Ni wazi kuwa wajinga ndiyo waliwao na ndiyo iliyo hali halisi!
Kupatikana kwa katiba mpya itakayo wanufaisha wote wakiwamo Chadema, kwa msimamo wa CCM ni bora isipatikane tu. Ya kuwa ni heri hali iliyopo iendelee kuliko kwa namna yoyote kuja pia kuwanufaisha Chadema. Ndivyo ilivyo hasa kwa kuzingatia kuwa pamoja na mapungufu yaliyopo, bado pia CCM ndiye aliye mnufaika zaidi.
Anayebakia kwenye harakati hizi za kupata katiba mpya na ya haki, ni Chadema na wachache wengine lakini si CCM. Kwa hali hii upatikanaji wa katiba mpya si rahisi sana, lakini si kuwa eti haiwezekani.
Kunahitajika kujizatiti vilivyo. Kutambua nini kinahitajika, kuwatambua washirika, kuwatambua maadui na kutambua nini cha kufanya kuhusu wote hao na lini.
Hakuna harakati zisizokuwa kuwa na wahanga. Ni muhimu kutambua viwango vyote vya uhanga unaoweza kutokea kutokana na jitihada za namna hii na kuona namna ya kuzi assimilate, accommodate au kuzifidia.
Kwamba litakayemkuta akale tu na wakwao, hiyo si katika zama hizi na kwa niaba na maslahi ya wote!
Hadi hapa tulipo leo, uzoefu uliopo unatosha sana.
Kutegemea kuwa pana mnufaika mmoja mahali kwa utashi wake tu atakuja siku moja akatupa katiba muafaka isiyokuwa na mapendeleo yoyote, haiwezi kuwa option.
Hali kadhalika kutegemea kuwa kwa kudra ya mwenyezi Mungu, siku moja mambo yatabadilika yenyewe ghafla na kuwa sawa, hilo pia haliwezi kuwa option.
Kulielewa tatizo kwa mapana, marefu na kimo chake ni mwanzo mwema wa kulitafutia suluhu ya kudumu.
Si Mataga, si CCM, si CUF, si ACT, si Chadema nk. Ni chama gani kwa dhati yao wanaishabikia katiba hii kuwa ndiyo mustakabala bora kabisa tunayoistahili?
Si manguli wa siasa wakiwamo kina Bashiru, kina Pole pole, Warioba, Butiku, nk wote hao wangependa uwepo wa katiba nyingine. Wala si hii ambayo ni wazi kuwa wengine katika hawa bila ya kutarajia kwa katiba hii, wamejikuta wakivunjika mioyo ghafla na kweli kweli. Hawakujua kuwa walistahili katiba mpya mapema, lakini sasa wanajua. Jambo la kheri tu.
Kundi pekee linaloishabikia katiba iliyopo kwa dhati (kuacha mambumbu) ni dogo sana na hili ni lile tu linalonufaika madarakani moja kwa moja kibinafsi kutokana na katiba iliyopo. Hawa wala si wengi kuvihimili vishindo vya watakao mabadiliko.
Kizingiti pekee kilichopo kuifikia azma hii inayotakikana na wengi ni kukosekana kwa umoja. Ni vipi Mataga wa CCM na CCM yenyewe iweze kushirikiana na vyama vingine kama Chadema kudai katiba mpya? Hilo haliwezekani japo wote Chadema na CCM wakiwamo Mataga wanaihitaji mno katiba mpya yenye kuwapa wote uhakika zaidi wa kesho.
CCM kushirikiana na wengine kwenye hili, ni rahisi zaidi kwa Ngamia kupita kwenye tundu la sindano. Ni wazi kuwa wajinga ndiyo waliwao na ndiyo iliyo hali halisi!
Kupatikana kwa katiba mpya itakayo wanufaisha wote wakiwamo Chadema, kwa msimamo wa CCM ni bora isipatikane tu. Ya kuwa ni heri hali iliyopo iendelee kuliko kwa namna yoyote kuja pia kuwanufaisha Chadema. Ndivyo ilivyo hasa kwa kuzingatia kuwa pamoja na mapungufu yaliyopo, bado pia CCM ndiye aliye mnufaika zaidi.
Anayebakia kwenye harakati hizi za kupata katiba mpya na ya haki, ni Chadema na wachache wengine lakini si CCM. Kwa hali hii upatikanaji wa katiba mpya si rahisi sana, lakini si kuwa eti haiwezekani.
Kunahitajika kujizatiti vilivyo. Kutambua nini kinahitajika, kuwatambua washirika, kuwatambua maadui na kutambua nini cha kufanya kuhusu wote hao na lini.
Hakuna harakati zisizokuwa kuwa na wahanga. Ni muhimu kutambua viwango vyote vya uhanga unaoweza kutokea kutokana na jitihada za namna hii na kuona namna ya kuzi assimilate, accommodate au kuzifidia.
Kwamba litakayemkuta akale tu na wakwao, hiyo si katika zama hizi na kwa niaba na maslahi ya wote!
Hadi hapa tulipo leo, uzoefu uliopo unatosha sana.
Kutegemea kuwa pana mnufaika mmoja mahali kwa utashi wake tu atakuja siku moja akatupa katiba muafaka isiyokuwa na mapendeleo yoyote, haiwezi kuwa option.
Hali kadhalika kutegemea kuwa kwa kudra ya mwenyezi Mungu, siku moja mambo yatabadilika yenyewe ghafla na kuwa sawa, hilo pia haliwezi kuwa option.
Kulielewa tatizo kwa mapana, marefu na kimo chake ni mwanzo mwema wa kulitafutia suluhu ya kudumu.