Tathmini ifanyike meza za bungeni.

Malata Junior

JF-Expert Member
Nov 29, 2011
3,102
2,538
Heshima mbele wakuu.
Tabia ya wabunge wa CCM kuunga mkono kila kitu hata kama hakuna tija na kuleta madhara kwa Taifa iangaliwe kwa hicho la tatu. Kibaya zaidi uungaji huo mkono wa kila kitu hata chenye madhara huambatana na kugonga meza kwa nguvu huku wakipiga mayowe kama wehu kitendo ambacho husababiaha uharibifu katika meza za binge. Utafiti umeonyesha viti ambavyo hukaliwa na wabunge wa CCM bungeni meza zake zimechakaa zaidi ya zile za wabunge wa upinzani kutokana na kugongwa kwa muda mrefu! Ili kuokoa fedha za walipa kodi zinazotumika Mara kwa Mara kutengeneza au kununua meza mpya tathmini ya uharifu huo wa meza za bunge unaofanywa na wabunge wa ccm ufanyike ikiwezekana kanuni za bunge zibadilishwe ili wabunge wawe wanapiga makofi badala ya kugonga meza.
 
Wapewe kengele na nondo za kupiga pale watakapoona inafaa,hali hiyo ikimkera spika ambae ni mstaarabu atawakataza

Pia wapewe madawati ambayo hawajizungushi wanapokaa bunheni watakumbuka kuwatetea wananchi wanyonge
 
Hahahaaaa, hiyo nayo ni kali duuu, pamoja na suala lameza, kweli wawakilishi wetu wanatakiwa kuwa makini na kile wanachokipitisha, ushabiki wa harakaharaka siyo mzuri, bali kama kuna jambo linahitaji muda, waombe muda mrefu wa kulijadili kwa kina sana
 
Ni vyema pia tungeanza na unafiki wa wabunge wa upinzani na tabia ya kupinga pinga tu, wao hawana jema ni kutukana na kejeli tu.
 
Huwezi kupeleka anayejua kusoma na kuandika tuu wakat kuna maslahi ya taifa...tuache ujuha ndio madhara yake
 
Naunga mkono hoja kwa 100% wapewe kengele zile kama za vipindi darasani au honi za magari.
 
Back
Top Bottom