Mtini
JF-Expert Member
- Apr 28, 2011
- 1,486
- 2,332
By Malisa GJ,
Katika mkutano mkuu wa CCM wa July 23 uliomchagua Magufuli kuwa Mwenyekiti Mpya niliobserve yafuatayo;
1. Jina "Magufuli" lilitajwa mara 108
2. Neno "Ilani ya Chama" lilitajwa mara 76
3. Neno "Tanzania" lilitajwa mara 31
4. Jina "Kinana" lilitajwa mara 16
5. Jina "Kikwete" lilitajwa mara 23
5. Jina "Nappe" lilitajwa mara 7
6. Jina "Lowassa" lilitajwa mara 504
7. Kati ya wazungumzaji wote waliopewa nafasi ya kuzungumza hakuna hata mmoja ambaye hakumtaja Lowassa.
8. Lowassa alitajwa mara 4 zaidi ya Rais Magufuli ndani ya mkutano huo (yani 504 Lowassa gawanya 108 JPM).
9. Lowassa alitajwa mara 23 zaidi ya Kikwete ndani ya mkutano huo (yani Lowassa 504 gawanya 23 JK)
10. Lowassa alitajwa mara 37 zaidi ya Kinana kwenye mkutano huo (yani Lowassa 504 gawanya 16 Kinana).
#NILICHOJIFUNZA:
1. Lowassa aliye nje ya CCM ana nguvu mara 4 zaidi ndani ya CCM kuliko Mwenyekiti wa sasa wa CCM Ndugu JPM. Ana nguvu mara 23 ndani ya CCM kuliko Mwenyekiti mstaafu wa CCM Ndugu JK. Pia ana nguvu mara 37 ndani ya CCM kuliko Katibu mkuu wa CCM Ndugu Kinana. Hesabu hii CCM wanaweza kushindwa kuielewa maana niliwahi kusema "wanapenda namba lakini hawajui hesabu"
2. Lowassa bado ni agenda kuu ndani ya CCM. CCM bado inaishi na kivuli cha Lowassa na kinawatesa. CCM inamhofia Lowassa, inamuogopa, inashtuka ikimsikia. Ndio maana inamuwaza siku zote. Hakuwepo kwenye mkutano wao lakini ametajwa kuliko mtu yoyote aliyekuwepo kwenye Mkutano huo. Ametajwa kuliko mwenyekiti wa chama, ametajwa kuliko mwenyekiti mstaafu, ametajwa kuliko Katibu Mkuu. Hii ni hofu ya wazi.!
3. Nimegundua Lowassa ni bora maradufu kuliko kiongozi yoyote ndani ya CCM. Kitendo cha kila kiongozi wa CCM kumtaja kinadhihirisha ubora huo. Hata katika mpira, mtangazaji humtaja mchezaji mwenye mpira, sio yule anayezubaa. Mchezaji anayetajwa zaidi ndiye anayemiliki mpira zaidi. Kwa sasa Lowassa ndiye anayemiliki mpira wa siasa za nchi hii. CCM wanajua, Tanzania inajua na dunia inajua.
4. CCM ina kila sababu ya kumhofia Lowassa kwa sababu wajumbe wale walioimba "wana imani nae", ndio haohao waliomchagua Magufuli kuwa Mwenyekiti wao, bila kutoa "remix" kwamba wana imani na mtu gani mwingine. Kwahiyo Lowassa anabaki kuwa bora ndani na nje ya CCM. Kinana anajua, Nappe anajua na dunia inajua.!
Alamsiki,
Malisa G.J
Katika mkutano mkuu wa CCM wa July 23 uliomchagua Magufuli kuwa Mwenyekiti Mpya niliobserve yafuatayo;
1. Jina "Magufuli" lilitajwa mara 108
2. Neno "Ilani ya Chama" lilitajwa mara 76
3. Neno "Tanzania" lilitajwa mara 31
4. Jina "Kinana" lilitajwa mara 16
5. Jina "Kikwete" lilitajwa mara 23
5. Jina "Nappe" lilitajwa mara 7
6. Jina "Lowassa" lilitajwa mara 504
7. Kati ya wazungumzaji wote waliopewa nafasi ya kuzungumza hakuna hata mmoja ambaye hakumtaja Lowassa.
8. Lowassa alitajwa mara 4 zaidi ya Rais Magufuli ndani ya mkutano huo (yani 504 Lowassa gawanya 108 JPM).
9. Lowassa alitajwa mara 23 zaidi ya Kikwete ndani ya mkutano huo (yani Lowassa 504 gawanya 23 JK)
10. Lowassa alitajwa mara 37 zaidi ya Kinana kwenye mkutano huo (yani Lowassa 504 gawanya 16 Kinana).
#NILICHOJIFUNZA:
1. Lowassa aliye nje ya CCM ana nguvu mara 4 zaidi ndani ya CCM kuliko Mwenyekiti wa sasa wa CCM Ndugu JPM. Ana nguvu mara 23 ndani ya CCM kuliko Mwenyekiti mstaafu wa CCM Ndugu JK. Pia ana nguvu mara 37 ndani ya CCM kuliko Katibu mkuu wa CCM Ndugu Kinana. Hesabu hii CCM wanaweza kushindwa kuielewa maana niliwahi kusema "wanapenda namba lakini hawajui hesabu"
2. Lowassa bado ni agenda kuu ndani ya CCM. CCM bado inaishi na kivuli cha Lowassa na kinawatesa. CCM inamhofia Lowassa, inamuogopa, inashtuka ikimsikia. Ndio maana inamuwaza siku zote. Hakuwepo kwenye mkutano wao lakini ametajwa kuliko mtu yoyote aliyekuwepo kwenye Mkutano huo. Ametajwa kuliko mwenyekiti wa chama, ametajwa kuliko mwenyekiti mstaafu, ametajwa kuliko Katibu Mkuu. Hii ni hofu ya wazi.!
3. Nimegundua Lowassa ni bora maradufu kuliko kiongozi yoyote ndani ya CCM. Kitendo cha kila kiongozi wa CCM kumtaja kinadhihirisha ubora huo. Hata katika mpira, mtangazaji humtaja mchezaji mwenye mpira, sio yule anayezubaa. Mchezaji anayetajwa zaidi ndiye anayemiliki mpira zaidi. Kwa sasa Lowassa ndiye anayemiliki mpira wa siasa za nchi hii. CCM wanajua, Tanzania inajua na dunia inajua.
4. CCM ina kila sababu ya kumhofia Lowassa kwa sababu wajumbe wale walioimba "wana imani nae", ndio haohao waliomchagua Magufuli kuwa Mwenyekiti wao, bila kutoa "remix" kwamba wana imani na mtu gani mwingine. Kwahiyo Lowassa anabaki kuwa bora ndani na nje ya CCM. Kinana anajua, Nappe anajua na dunia inajua.!
Alamsiki,
Malisa G.J