Tathimini yangu Gamba CCM ni CCM yenyewe kulivua gamba bila kuivunja CCM ni usanii

Jan 16, 2007
721
176
Tumekemea ufisadi na rushwa ndani ya CCM,Tumeonyesha maovu,ufisadi,rushwa na madudu kibao ndani ya CCM.Walitubeza na kukanusha kwa muda mrefu baadae wakaibuka na kauli mbiu "Kujivua gamba"Tukawabana kuitekeleza kauli hiyo ya kisanii kujivua gamba siku tisini............sasa mwaka unakaribia hakuna lilifanyika.Tunachoshuhudia hivi sasa ni kauli na minyukano katika majukwaa na vyombo vya habari wakipigana vijembe katika makundi yaliyomo ndani ya CCM yakilituhumu kundi lingine kua Magamba na ufisadi na wanakili ya kua kuna magamba na ufisadi uliokithiri ndani chama tawala CCM,wanakili kwamba viongozi wanatoa hongo na kutumia pesa kupata nafasi za uongozi!Na viongozi haohao kutoka chama tawala wanakua viongozi katika serikali tutegemee nini.Tathimini yangu Gamba CCM ni CCM yenyewe kulivua gamba bila kuivunja CCM ni usanii.
 
Ndugu yangu kwa kawaida nyoka akijivua gamba anakuwa na sumu kali kuliko mwanzo, kwa maana hiyo tusitarajie lolote la maana toka ccm baada ya kujivua gamba zaidi sana wataishia kubadilisha mbinu za kuiba. BILA KATIBA MPYA HATA WAKIJIVUA MENO BADO WATAIBA TU.
 
Back
Top Bottom