TARURA, ni wakati sasa mkajikita kurekebisha kwa kiwango cha lami barabara za mitaani Dar es salaam

N'yadikwa

JF-Expert Member
Aug 10, 2014
6,825
9,532
Nawakumbusha tu TARURA wakati serikali mpya ikiingia madarakani ni muhimu sasa barabara za mitaani katika jiji la kibiashara la Dar es salaam zikajengwa kwa kiwango cha lami. kusema kweli ni aibu kwamba barabara nyingi za mitaani hata katika maeneo yaliyopangiliwa kama vile Mbezi Beach, Mbweni,Bunju Beach,Makongo, Tegeta Masaiti Nakadhalika zina mashimo ya kiwango cha mahandaki. Ili wananchi wa Dar es salaam wajenge imani kwa serikali hii iliyoingia madarakani. Aidha barabara zote hata kwa maeneo yasiyopangiliwa zijengwe kwa kiwango hicho cha lami.

Ujenzi wa barabara hizi utasaidia pia kudhibiti mafuriko ya mara kwa mara Dar es Salaam kwa kuwa utaambatana na mifereji inayotoa maji mengi yanayokusanyika kutoka kwenye bati na kuelekea kwenye mkondo wake.

Sambamba na hilo TAMISEMI tafakarini kwa kushirikiana na Wizara ya Miundombinu njia ya kuondoa kero ya mafuriko Dar es salaam hasa pale Jangwani ambapo barabara hufungwa kwa mvua ya mm kidogo tu.
 
Hela watatoa wapiiii?
Serikali inazo pesa au humsikii Mheshimiwa Magufuli akisisitiza kwamba Sisi ni matajiri na fedha tunazo. Tanzania hatuna tatizo la fedha hata kidogo kwa vitu vidogo kama hivi.

Faini za barabarani peke yake zinaweza kujenga barabara za mitaa kwenye miji yetu mikuu bila kutegemea wafadhili. Vijana wanaomiliki magari na kuvunja sheria ni wengi mno siku hizi.

Aidha Halmashauri zinaweza kutenga fedha kwa ajili hii kwa sababu lami za huku mitaani naamini hazitakuwa za kiwango cha mainroad kwa hiyo gharama itakuwa chini.

TUNAWEZA
 
...'Hamashauri kutenga fedha'...
huo ulikuwa ni mfumo wa kizamani ulioruhusu 'upigaji'na ulaji wa kufuru.

Sasa hivi halmashauri hawatengi fedha bali wanatengewa na kupewa miongozo jinsi ya kuzitumia maana wanazokusanya hawana mamlaka nazo tena ya kuzitumia.

Enzi halmashauri zinajiendesha, uliona zikileta maendeleo?
Labda kwa uchache sana.
 
...'Hamashauri kutenga fedha'...
huo ulikuwa ni mfumo wa kizamani ulioruhusu 'upigaji'na ulaji wa kufuru.

Sasa hivi halmashauri hawatengi fedha bali wanatengewa na kupewa miongozo jinsi ya kuzitumia maana wanazokusanya hawana mamlaka nazo tena ya kuzitumia.

Enzi halmashauri zinajiendesha, uliona zikileta maendeleo?
Labda kwa uchache sana.
Nadhani angalau sasa serikali kuu wanaweza kuutendea kazi ushauri huu...barabara za mitaani Dar es Salaam zinatia huruma hakyanan
 
TARURA ki ujenzi aidha hawajajielewa bado au ndio kazi ni ngumu kwao.
Makandarasi wanaojielewa hawacukui kazi za TARURA.
Rates za kazi ni ndogo mno, ati wanaziita value for money- misemo ya wanasiasa!
Gharama za kazi haiwezi kuvuta wakandarasi wanaolia kodi.
Heri TARURA wafanye hizo kazi kwa mtindo wa Fosi Akaunti!!
 
Nadhani angalau sasa serikali kuu wanaweza kuutendea kazi ushauri huu...barabara za mitaani Dar es Salaam zinatia huruma hakyanan

Barabara za mitaan hazifai hata kidogo, sio lazima lami, angalau zishindiliwe tu vizuri na kuzijengea mifereji ya maana. Sasa barabara nyingi hasa kimara ni udongo mtupu, mvua ikinyesha kidogo hazipitiki!
Ila cha ajabu hakuna hata anayejali, mimi kuna muda huwa nawaza sisi watu weusi tuna matatizo makubwa sana vichwani.
 
Tatizo mnataka maendeleo ya haraka, maendeleo hayana haraka.
... wale wapinzani waliokuwa wanapinga maendeleo Bungeni sasa hawapo tena; ni lazima tupate maendeleo kwa speed ya mwanga maana CCM imebaki peke yake sasa. Hope by 2025 lazima nchi iwe kama Dubai.
 
Barabara za mitaan hazifai hata kidogo, sio lazima lami, angalau zishindiliwe tu vizuri na kuzijengea mifereji ya maana. Sasa barabara nyingi hasa kimara ni udongo mtupu, mvua ikinyesha kidogo hazipitiki!
Ila cha ajabu hakuna hata anayejali, mimi kuna muda huwa nawaza sisi watu weusi tuna matatizo makubwa sana vichwani.
Kwa kweli mkuu.
 
TARURA ki ujenzi aidha hawajajielewa bado au ndio kazi ni ngumu kwao.
Makandarasi wanaojielewa hawacukui kazi za TARURA.
Rates za kazi ni ndogo mno, ati wanaziita value for money- misemo ya wanasiasa!
Gharama za kazi haiwezi kuvuta wakandarasi wanaolia kodi.
Heri TARURA wafanye hizo kazi kwa mtindo wa Fosi Akaunti!!
Mkuu kuuliza sio ujinga. Hivi force account inafanyaje kazi na ikoje hasa uhalali wake kisheria nk
 
Unatukumbusha wewe ni nani
Wewe ni mbunge mteule.
Watu wanalipwa kwa hii kazi unayofanya
Mimi ni mwananchi wa kawaida tu ninaeipenda nchi yangu. Katiba inaniruhusu kushiriki ujenzi wa Taifa, hivyo natoa maoni kuwakumbusha watekelezaji kupitia kodi ninayolipa kila siku. Una swali jingine mkuu!?
 
Back
Top Bottom