Tarime: Askari Polisi adaiwa kumuua raia kwa kumfyatulia risasi

Nyakijooga

Senior Member
Dec 9, 2018
121
202
Askari namba H.4489 PC Kululetela wa kituo cha Polis Sirari Mkoa wa Kipolisi Tarime Rorya anadaiwa kushikiriwa na Jeshi la Polisi kwa kusababisha kifo cha mtu mmoja aliyetambulika kwa jina la Ng’ondi Marwa Masiaga (22) kutokana na kumfyatulia risasi kwa uzembe na kupekea majeraha yaliyopelekea kutokwa damu nyingi.

Taarifa ya Jeshi la Polisi kutoka Mkoa wa kipolisi Tarime Rorya inaeleza kuwa Askari huyo kwa uzembe wake mwenyewe na bila uhalali wowote alimfyatulia risasi raia huyo asiyekuwa na hatia na kumjeruhi kwenye paja lake la mguu wa kulia.

Madhura huyo imeelezwa kuwa alikimbizwa katika hospitali ya Tarime ambapo alifariki Dunia wakati akipatiwa matibabu. Ambapo imeelezwa kuwa uchunguzi wa awali umebai kuwa alifariki kutokana na kutoka damu nyingi.

Kufuatia tukio hilo imeripotiwa kuwa askari huyo anashikiriwa na upelelezi wa tukio hilo unaendelea na kuwa utakamirishwa mapema, huku taarifa hiyo iliyotolewa Machi 31, 2023 inaeleza kuwa mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Tarime ukisubiri uchunguzi wa kitabibu.
IMG-20230401-WA0000.jpg


Sent from my Infinix X665 using JamiiForums mobile app
 
Askari anamfyatulia raia bila sababu? Kuna mambo mawili aidha wanajuana hapo kabla ambapo walishapishana au askari ana matatizo ya afya ya akili.

Mental health is a real problem nowbdays. Tuwe makini na hawa ashika mitutu sio wote ni wazima
 
Tukifanya kama walichokifanya Geita tutaonekana wakorofi,,
anyway Rip Ng'odi umekufa ukingali mdogo sana,, Hasira yangu juu ya mapolisi haitakuja kuisha mpaka nije niwafanyie kitu cha kihistoria hawa mbwa ndipo nami nife kwa amani,, ipo siku
 
Askari namba H.4489 PC Kululetela wa kituo cha Polis Sirari Mkoa wa Kipolisi Tarime Rorya anadaiwa kushikiriwa na Jeshi la Polisi kwa kusababisha kifo cha mtu mmoja aliyetambulika kwa jina la Ng’ondi Marwa Masiaga (22) kutokana na kumfyatulia risasi kwa uzembe na kupekea majeraha yaliyopelekea kutokwa damu nyingi.

Taarifa ya Jeshi la Polisi kutoka Mkoa wa kipolisi Tarime Rorya inaeleza kuwa Askari huyo kwa uzembe wake mwenyewe na bila uhalali wowote alimfyatulia risasi raia huyo asiyekuwa na hatia na kumjeruhi kwenye paja lake la mguu wa kulia.

Madhura huyo imeelezwa kuwa alikimbizwa katika hospitali ya Tarime ambapo alifariki Dunia wakati akipatiwa matibabu. Ambapo imeelezwa kuwa uchunguzi wa awali umebai kuwa alifariki kutokana na kutoka damu nyingi.

Kufuatia tukio hilo imeripotiwa kuwa askari huyo anashikiriwa na upelelezi wa tukio hilo unaendelea na kuwa utakamirishwa mapema, huku taarifa hiyo iliyotolewa Machi 31, 2023 inaeleza kuwa mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Tarime ukisubiri uchunguzi wa kitabibu.View attachment 2572755

Sent from my Infinix X665 using JamiiForums mobile app
Kule Chato ilitokea nn? Kituo kidogo cha polisi mganza,hii tarifa aijatimia chanzo nn?
 
Huyu baada ya miaka 2 atahamishiwa kituo cha mbali anaendelea na kazi yake
 
Ila jaman hawa walinzi wetu siku hizi wamekuaje?? Mbna wanatesa na kuua raia bila sababu za msingi? Tatizo nn?

Wanakera mnooo.
 
Back
Top Bottom