mr yamoto
JF-Expert Member
- Oct 2, 2016
- 923
- 1,393
Tarehe na mwezi kama wa leo mwaka 2017, Mbunge wa Singida Mashariki na Mwanasheria mkuu wa ChademaTz Mh. Tundu Lissu alipigwa risasi mchana kweupe mkoani Dodoma Akiwa katika majukumu yake ya kibunge.
Leo imetimia miaka 2 tangu shambulizi lililokusudia kumwua Mbunge mwenzetu Tundu Lissu. Tunamshukuru sana Mungu kwa uwezo wake na maajabu yake ambayo yamemweka hai mwenzetu na sasa amepona na kuweza kushiriki nasi katika mapambano ya kuhami na kukomaza demokrasia yetu
Siku ya Tarehe 7/9/2017 ilianza kama siku nyengine tu kwa Wabunge na Watanzania. Rais Magufuli alikuwa Ikulu akizungumzia sarakasi za makanikia, Tundu akiwa Bungeni akitimiza majukumu yake kwa kujadili Azimio la Malawi-Tanzania ( Mto Songwe). Ilipofika saa 7/8 mchana mzizimo
Serikali na vyombo vyake vya dola mtajiondoa kwenye lawama za shambulizi la AIBU la Lissu wetu pale tu mtakapotumia utaalam na weledi wenu wote kuwabaini na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria washenzi wale waliotekeleza shambulio lile. Mmetuambia mara kadhaa uwezo huo mnao.
Tukijidai kusahau shambulizi lile la kipumbavu kwa Tundu Lissu, ipo siku litajirudia ila hatujui ni lini na kwa nani. JINAI ina tabia ya kuendelea kuwepo isipokemewa, watenda jinai wasipobainika na sheria kuchukua mkondo wake.
.
Leo imetimia miaka 2 tangu shambulizi lililokusudia kumwua Mbunge mwenzetu Tundu Lissu. Tunamshukuru sana Mungu kwa uwezo wake na maajabu yake ambayo yamemweka hai mwenzetu na sasa amepona na kuweza kushiriki nasi katika mapambano ya kuhami na kukomaza demokrasia yetu
Siku ya Tarehe 7/9/2017 ilianza kama siku nyengine tu kwa Wabunge na Watanzania. Rais Magufuli alikuwa Ikulu akizungumzia sarakasi za makanikia, Tundu akiwa Bungeni akitimiza majukumu yake kwa kujadili Azimio la Malawi-Tanzania ( Mto Songwe). Ilipofika saa 7/8 mchana mzizimo
Serikali na vyombo vyake vya dola mtajiondoa kwenye lawama za shambulizi la AIBU la Lissu wetu pale tu mtakapotumia utaalam na weledi wenu wote kuwabaini na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria washenzi wale waliotekeleza shambulio lile. Mmetuambia mara kadhaa uwezo huo mnao.
Tukijidai kusahau shambulizi lile la kipumbavu kwa Tundu Lissu, ipo siku litajirudia ila hatujui ni lini na kwa nani. JINAI ina tabia ya kuendelea kuwepo isipokemewa, watenda jinai wasipobainika na sheria kuchukua mkondo wake.
.