Nani anataka kukumbushwa misafara yenu na Rais Mkapa kwenda Geneva kutoa mada kuhusu ajira za utotoni???...Wakati huo tulikuwa Geneva, Uswisi kuhudhuria mkutano wa ... kuwasilisha mada kuhusu ajira mbaya za utotoni (worse forms of child labour).
... akiwa na wajumbe wote kutoka Tanzania.
...Nakumbuka Bwana Naftali Nsemwa, aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa PPF alikwenda....
...na viongozi waandamizi wa Serikali akiwemo Balozi Ali Mchumo
...Mkurugenzi Mkuu wa NSSF nae amehudhuria mkutano huo.
...Balozi Joshua Opanga ambaye alikuwa Mkuu wa Itifaki ...
Hao watoto wanaoajiriwa wako Geneva ???
Halafu NSSF na PPF ni mifuko ya ajira za watu wazima, sasa hizo mada za watoto zinawahusu nini kama sio kwenda kutumbua kodi za jasho la masikini??
Halafu umesema aliyeitwa kusoma mada ni Rais Mkapa. Nyinyi msururu wa vigogo wengine mlienda kumshikia maiki ?????
Rais Magufuli muda huu amesimamisha gari Kibiti akitoka kumzika Mkapa, ameamuru wanananchi eneo la Soko Kuu Kibiti kutumia choo cha nyumbani kwa DC na Mkurugenzi wa Wilaya kwa siku saba wakati wilaya inajenga choo.
Wewe unatueleza habari ya ulikutana na Rais kwa mara ya kwanza Geneva, mkiwa mmeambatana na viongozi kibao ambao walitakiwa kuwa bongo wanajenga vyoo, visima na kuzibua mitaro! Hatutaki kusikia ya Geneva.
Obviously mnakumbuka Mkapa (Kikwete pia) kwa sababu ndio walikuwa wanalea uozo na wizi huo
Usitutibue please, kwa kutukumbusha shenanigans za serikali zenu zile. You should be in jail right now, for all the swindles and scandals you occasioned at NSSF