Tanzia: Thomas Mashali afariki dunia baada ya kushambuliwa na watu wasiojulikana

Jamaa alikuwa na territory ya ukweli aisee.
M'babe m'babe mmoja mtata sana,alikuwa amewapangia hesabu mateja na ilikuwa haipungui hata sent na ikipungua alioenda kukabidhi alikuwa anachezea vikombe anapukutishwa za mfukoni kisha anafukuzwa kituoni hasimami hadi kwa utashi wa jamaa amruhusu tena na akimkuta kasimama bila idhini yake anamvunja mbavu...walikuwa wakimuogopa hakuna mfano.
 
Mashali alikuwa jambazi, tena wamechelewa kumuua ameumiza watu wengi sana....REST IN HELL MASHALI....NATUMAINI SASA HIVI YUKO JEHANAM ANACHOMWA MOTO KWA MATENDO YAKE.
Duhh, huyu bwana kumbe alikuwa hatari sana. Nasikia aliacha shule akiwa darasa la nne baada ya kumpiga mwalimu na kufukuzwa shule ndipo akajiunga na ndondi
 
Enyi watu mtu anapokumbwa na umauti sio wakati wake kusema myasemayo kwa kuona unatumis jina la uongo kwenye jf.wewe huenda unanunua malaya,huenda ni mlevi,hutoi sadaka,hufanyi ibada,unawakela jirani zako.zote ni dhambi mbele ya Mungu.usitingwe na dunia kujiona huru sana fahamu Mungu anasema nini baada ya mtu kukumbwa na umauti.mashali kuchomwa motoni au kuingia peponi Mungu anajua
Hakuna kitu kibaya kama unafki.Hivi huyu "Mungu"tunayemuomba kila mtu anapofariki eti "alazwe pema peponi hata kama mtu tulikuwa tubamjua maovu yake!Acheni unafki eti marehemu hazungumzwi vibaya.Mwacheni Mungu amlaze muhusika mahali anapoona panafaa,tusimfundishe cha kufanya.Ova!
 
jamaa mbona alikuwa mtu poa sana dah pole sana kwa familia yake, jamaa mara ya mwisho kumuona ilikuwa alipokuja Moro kupambana na cheka..Mungu amlaze mahali pema inshallah.
Acha unafiki hajawah kuwa poa...watafute wauza mitumba wa big brother,wakaz wa tandale,madalali wa soko la tandale,malaya wa lambo bar..nk..watakuambia...R.I.P
 
Mashali alikuwa m2 poa sana mm nilikuwa nakutana nae sana maeneo ya Meridian M'nyamala na kama humjui ilikuwa sio rahisi kuja km ni boxer hakuwa na ubabe jinsi watu wanavyoelezea
Acha uongo...waulize watu wa big brother,tandale,urafik,...jamaa alikuwa anadhulumu hata chips mayai...waulize boda boda wa manzese..watakuambia...ila unyama aliofanyiwa haukubalik..
 
MASHALI ALIKUWA MTU MBAYA.....
Mtetee tu kwa sababu ulikuwa unakutana naye hapo

PROMOTA WAKE ameiambia Clouds360 kwamba MASHALI akilewa huwa "MBABE" jana alipgiwa cm na rafk yake kwenda kimara,baada ya kufika huko wakawa wanakula MVINYO,baada ya kulewa wakaznguanana na mtu mwingn,MASHALI akamtandika[NGUMI KALI] huyo jamaa baada ya kupewa kichapo akaanza kupiga kelele za mwiz,,,Wakatokea wananchi wenye hasira na silaha wakamchakaza[bila kujua kama ni Mashali] baadhi ya watu wakasema sio mwizi huyu ni mashali raia wakamuacha lakini alikua tayar ashaumia sana na kumwaga damu nyingi...BODABODA wa hapo kimara wakamchukua na kumpeleka hospital then wakaanza kutoa taarifa kwa WANAOMJUA.
 
Duhh, huyu bwana kumbe alikuwa hatari sana. Nasikia aliacha shule akiwa darasa la nne baada ya kumpiga mwalimu na kufukuzwa shule ndipo akajiunga na ndondi
Unaamini kirahisi hivyo mtu hana ushahidi na wewe unakubali unaweza kuta huyu ndo kamuua huyo mahali tuepuke kuamini mambo km haya kirahisirahisi... One mtu mmoja amesema uwongo kuhusu miss tz juz mpaka leo Kuna sintofahamu
 
Acha unafiki hajawah kuwa poa...watafute wauza mitumba wa big brother,wakaz wa tandale,madalali wa soko la tandale,malaya wa lambo bar..nk..watakuambia...R.I.P
Sasa Unafk wake ni upi nyie mliokuwa mnamfahamu halafu mkafumbia macho mpaka sahizi amerudi mavumbini ndo wanaa au kwavile hawezi kujitetea tena?
 
Alishawahi kufungwa miaka 2.
Alishaponea chupuchupu mburahati

Ukikutana naye night Kali lazima ule ngumi nzito na kuachia vitu vyako ,alikuwa mkabaji mzr na mbabe wa kijinga

Ujanja ukiwa mwingi madhara yke ndio hayo
Tena wale jamaa wa mburahat wangemuua...walimpa kichapo heavy mpaka alinyoa rasta...kifup alikuwa kavu...ila wahusika wasakwe tuu
 
Unaamini kirahisi hivyo mtu hana ushahidi na wewe unakubali unaweza kuta huyu ndo kamuua huyo mahali tuepuke kuamini mambo km haya kirahisirahisi... One mtu mmoja amesema uwongo kuhusu miss tz juz mpaka leo Kuna sintofahamu
Ndivyo mzee wake alivyoongea na ndio sababu ya kutokuelewana kati ya baba na mtoto kwa kipindi kirefu
 
Back
Top Bottom