Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,266
- 33,039
TANGAZO LA MSIBA:
Jumuiya ya Watanzania Roma pamoja na Jumuiya ya Watanzania Italia zinasikitisha kutangaza kifo
cha Ndugu Abdulli Abuu(HATIBU CLEAN HEART) kilichotokea tarehe 08-12-2013 mjini Rome
kwenye Casa di Cura (HOSPICE S. ANTONIO DA PADOVA) baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Kutokana na msiba huu ambao sisi sote kama watanzania unatugusa, tunaombwa tujumuike kwa
pamoja tuweze kuangalia mpango mzima wa msiba huu! Mjini Rome tumeamua kuwa na kikao siku
ya Jumanne tarehe 17 Disemba saa kumi na moja kamili, maeneo ya Termini kwenye restaurant ya
Wahindi iliyopo kwenye Mtaa wa Via Principe Amedeo. Na kwa wakazi wa NAPOLI na mkoa mzima
wa CAMPANIA kutakuwa na mkutano siku ya jumamosi tarehe 14/12/2013 PENITAMARE kwa dada
MARY kuanzia saa kumi Jioni. Tunaombwa tujumuike kwa wingi. Mwenyezi Mungu amlaze
marehemu Abdulli Abuu mahali pema peponi amina.
MAWASILIANO:
ROMA: 3391597134 KATIBU
NAPOLI: 389 8583370 KATIBU