Muokota Makopo
Member
- Jan 9, 2020
- 54
- 95
Mwandishi Nguli wa Kazi za Fasihi ya Kiswahili Prof. Euphrase Kezilahabi amefariki dunia. Tutamkumbuka Kezilahabi kwa kazi zake kama Rosa Mistika, Uwanja wa Fujo, Kaptula la Marx, Nagona na Mzingile! Alitetea Mashairi ya Kisasa!
Hakika, Jabali limeanguka! Tumeondokewa pakubwa.
Pumzika kwa amani Euphrase Vincent Mfunzi Bagaza Tilibuzya Kezilahabi😭😭
Soma; Kaptula la Marx: Unafahamu kwanini kitabu hiki kilipigwa marufuku? Waandishi wetu na Siasa zetu
====
1. Kaptula la Marx: Unafahamu kwanini kitabu hiki kilipigwa marufuku? Waandishi wetu na Siasa zetu
Hakika, Jabali limeanguka! Tumeondokewa pakubwa.
Pumzika kwa amani Euphrase Vincent Mfunzi Bagaza Tilibuzya Kezilahabi😭😭
Soma; Kaptula la Marx: Unafahamu kwanini kitabu hiki kilipigwa marufuku? Waandishi wetu na Siasa zetu
Huyu E. Kezihalabi ni nani?
Euphrase Kezilahabi alizaliwa 13 Aprili 1944 huko Namagondo kisiwani Ukerewe kilichopo ndani ya Ziwa Viktoria. Babake Vincent Tilibuzya alikuwa msimamizi wa kijiji na Euphrase alikuwa na ndugu 10 yaani wavulana 5 na wasichana 5. Alisoma shule ya msingi ya Nakasayenge halafu tangu 1957 Seminari ya kikatoliki ya Nyegezi aliyomaliza mwaka 1966.
1967 alijiandiskisha kwenye Chuo Kikuu cha Dar es Salaam akasoma ualimu na fasihi hadi digrii ya B.A. katika mwaka 1970. Mwaka uleule 1970 akawa mwalimu wa shule ya sekondari Mzumbe (Morogoro) halafu kwenye shule ya sekondari ya Mkwawa (Iringa).
1971 alirudi chuoni Dar es Salaam akawa mhadhiri msaidizi wa chuo alipoandika pia tasinifu ya M.A. kuhusu riwaya za Shaaban Robert, tangu 1974 mhadhiri kamili na 1978 mhadhiri mwandamizi. Akaendelea na masomo ya Ph.D. huko Marekani kwenye Chuo Kikuu cha Wisconsin Madison alipotoa tasinifu yake mwaka 1985 kuhusu "African Philosophy and the Problem of Literary Interpretation". Sasa (mwaka 2012) ni profesa wa lugha za Kiafrika kwenye Chuo Kikuu cha Botswana.
Uandishi wake fikirishi uliowahi mletea shida sana kisiasa
kwa wale wenzangu ambao wamekuwa na utamaduni wa kujisomea bila shaka napotaja jina la Euprase Kezihalabi si geni masikioni mwao. Ukiacha ambao walisoma vitabu vyake wakiwa shule kwenye fasihi. binasfi nilianza kusoma vitabu vyake nikiwa nyumbani nikisoma kama burudani kabla ya kuja kufaham baadaye kile kilichokuwa kimeandikwa na athari zake. Nilisoma vitabu kama Rosa Mistika, Kichwa maji ,Dunia Uwanja wa Fujo,Gamba la Nyoka na Kaptula la Marx.
Vitabu hivi vitatu vilikuwa na ukakasi mwingi sana kufikia hatua viwili kati yake kufungiwa au kuzuiwa kuuzwa. Rosa Mistika na Kaptula la Max.
Zaidi Soma:1. Kaptula la Marx: Unafahamu kwanini kitabu hiki kilipigwa marufuku? Waandishi wetu na Siasa zetu