Tanzia: Mwanamuziki mkongwe, Ahmed Manyema amefariki dunia leo Hospitali ya Mwananyamala

tramadol

JF-Expert Member
Oct 10, 2015
5,383
4,317
Maamuzi mkongwe na muda mrefu Ahamed Manyema ametutoka leo ktk Hospitali ya Mkoa ya Rufaa ya Mwananyamala.

Msiba upo Makutano Mabibo Wilaya ya Kinondoni Jijini Dar es salaam.

Taarifa za kifo chake zimedhibitishwa na Mwanamuziki Mkongwa John Kitine.

Marehemu amefanya kazi ya music na bendi mbalimbali nchini na baadhi ya nyimbo zikirekodiwa Redio Tanzania Dar es salam (RTD) wakati huo leo ni TBC Taifa.

Mzee Ahamed Manyema ni mzaliwa wa Kigoma

manyama.jpg
Mzee Ahamed Manyema a.k.a Majini wa Bahari akiwa ktk msiba wa Shem Karenga enzi za uhai wake
 
Hapana mkuu amefariki Jana usiku.
Nimemsikia Stazo wa Magic FM akimuongelea na akacheza nyimbo zake mbili.
FB_20170407_19_55_20_Saved_Picture.jpg
 
Amefariki leo alfajiri Mwananyama na madaktari walikuwa wanataka kumpa rufaa ya Muhimbili.
Basi mzee Mwinyi Ammy Stazo ametudanganya sisi wasikilizaji wake....nadhani ntamfollow kwenye ukrasa wake wa kijamii ili nimjuze kwamba kafariki leo.
Ahsante kwa taarifa.
 
Back
Top Bottom