TANZIA: Mkuu wa Uhamiaji mkoa wa Kagera, Pendo Butenghe afariki dunia

G Sam

JF-Expert Member
Apr 20, 2013
11,555
35,880
Imeripotiwa muda mfupi uliopita kuwa Pendo Butenghe ambaye ni Mkuu wa Uhamiaji mkoa wa Kagera amefariki dunia usiku wa kuamkia leo baada ya kuugua kwa muda mfupi.

Akithibitisha kifo hicho, Kaimu Mkuu wa Uhamiaji Kagera, Thomas Fush, amesema marehemu alikuwa anasumbuliwa na maradhi ya kushuka sukari mwilini.

Taarifa rasmi za kilichomuua hazijatolewa.

===

Mkuu wa Uhamiaji mkoani Kagera Pendo Butenghe, amefariki usiku wa kuamkia leo, Aprili 29 katika Kliniki ya COSAD kutokana na maradhi ya Shinikizo la Damu na Kisukari

Aidha, inadaiwa marehemu alianza kutumia dawa za kienyeji (kujifukuza) na alipoanza kukosa pumzi na kushindwa kuhema mkewe alimpeleka katika Kliniki hiyo. Aliwekewa drip lakini kupumua ikawa shida zaidi hadi akakutwa na mauti

Kaimu Mkuu wa Uhamiaji Kagera, Thomas Fush, amesema wanasubiria mwongozo wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa na Makao Makuu ya Uhamiaji kujua taratibu za msiba na maziko

Butenghe.jpg
 
Imeripotiwa muda mfupi uliopita kuwa Pendo ambaye ni mkuu wa uhamiaji mkoa wa Kagera amefariki dunia usiku wa kuamkia leo baada ya kuugua kwa muda mfupi.

Kabla ya hapo alikuwa ana matatizo ya sukari ila bado taarifa rasmi za kilichomuua hazijatolewa.
Hili tatizo la upumuaji ni kubwa
 
TANZIA: Mkuu wa Uhamiaji mkoani Kagera Pendo Butenghe, amefariki usiku wa kuamkia leo katika Hospitali ya Rufaa Mkoa - Bukoba, baada ya kuugua kwa muda mfupi. Kaimu Mkuu wa Uhamiaji Kagera, Thomas Fush, amesema marehemu alikuwa anasumbuliwa na maradhi ya kushuka sukari mwilini

Kaimu Mkuu wa Uhamiaji Kagera, Thomas Fush, amesema marehemu alikuwa anasumbuliwa na maradhi ya kushuka sukari mwilini
Capt.PNG
 
Back
Top Bottom