Sexer
JF-Expert Member
- Oct 22, 2014
- 8,204
- 7,892
Habari mbaya, mbunge wa jimbo la geita bwana Donald Max amefariki dunia hivi punde. Pole kwa wananchi wa Geita
Siku za nyuma ilishawahi kuletwa thread JamiiForums akiwa India alipokua anatibiwa kansa ya Ubongo.
https://www.jamiiforums.com/habari-...bunge-donald-max-aingizwa-icu-hali-mbaya.html
=====================
Updates
Siku za nyuma ilishawahi kuletwa thread JamiiForums akiwa India alipokua anatibiwa kansa ya Ubongo.
https://www.jamiiforums.com/habari-...bunge-donald-max-aingizwa-icu-hali-mbaya.html
Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Geita (CCM) Mheshimiwa Donald Kevin Max (58)(picha) amefariki dunia.
Kufuatia taarifa iliyotolewa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Anne Makinda (Mb) kwa Waheshimiwa Wabunge wote pamoja na umma kwa ujumla, Mhe. Max amefariki dunia tarehe 23 Juni, 2015 katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili alikokuwa akipatiwa matibabu.
Kwa mujibu wa taarifa hii, taarifa zaidi juu ya msiba huu zitaendelea kutolewa na Ofisi ya Bunge kwa kushirikiana na familia kadri zitakavyopatikana ikiwa ni pamoja na ratiba ya Mazishi.
"BWANA ametoa, BWANA ametwaa,
Jina la BWANA lihimidiwe." Amina.
Imetolewa na:
Ofisi ya Bunge,
Idara ya Habari, Elimu kwa Umma na
Uhusiano wa Kimataifa,
DODOMA
=====================
Updates
Spika wa Bunge Anna Makinda, ametangaza leo tarehe 24 asubuhi Bungeni kwamba, amefariki jana saa za mchana baada ya kuwa amelazwa kwa muda mrefu. Taarifa za awali ni kwamba Marehemu atazikwa Dar Es Salaam siku ya Jumamosi. Spika kasema taarifa nyingine bado anaendelea kuwasiliana na familia.
Spika kasema kwa mujibu wa kanuni za bunge, Siku ambayo mwezetu ameondoka duniani, tunakua hatuna bunge. Kutokana na kifo hicho basi, Bunge linaahirishwa hadi kesho saa tatu Asubuhi. Kwa wale Wabunge watakao takiwa kwenda kuzika, Ofisi ya katibu inaendelea kufanya utaratibu