Pole sana KakaKiiza na familia nzima kwa msiba huu mkubwa. Tunakuombea kwa Mungu Akupe nguvu na faraja katika kipindi hiki kigumu.
Mungu Ampumzishe mpendwa wetu mahali pema!
Bwana Alitoa, Bwana Ametwaa, Jina la Bwana Lihimidiwe!
maskini kaenda akiwa mjamzito, nimeumia zaidi, i can imagine the pain she felt, MUNGU MWEMA AMSAMEHE MAKOSA YAKE NA IMPENDEZE KUMPOKEA KWAKE MBINGUNI, AMEN!
Pole sana Kakakiiza na familia yako kwa ujumla Inasikitisha sana mpaka mwili umesisimka kwa wogahaya matatizo ya uzazi jamani mungu atusaidie."Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke Siku zake za kuishi si nyingi, naye hujaa taabu. Yeye huchanua kama vile ua, kisha hukatwa; Hukimbia kama kivuli, wala hakai kamwe."Mungu awape moyo wa subira na ujasiri katika kipindi hiki kigumuAmen.
Kifo cha ujauzito ni kifo kitakatifu. Naamini Mungu atampa marehemu upendeleo wa pekee katika makao yake Mbinguni kwani katoa uhai wake katika mchakato wa kuleta uhai kwa kiumbe kipya!!
Raha ya milele ampe ee Bwana, na Mwanga wa milele amwangazie...Apumzike kwa amani!!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.