TANZIA: Imamu mkuu wa msikiti wa Mtoro Sheikh Zubeir Bin Yahya afariki dunia

Ghazwat

JF-Expert Member
Oct 4, 2015
23,718
66,262
Imamu mkuu wa msikiti maarufu nchini Tanzania na Afrika mashariki Masjid Mtoro uliopo jijini Dar es salaam eneo la Kariakoo, Sheikh Zubeir bin Yahya Mussa, amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Machi 5, 2019.

Sheikh Zubeir ni miongoni mwa masheikh maarufu jijini Dar es salaam alifahamika sana kutokana kuwa ni Imamu katika msikiti huo, ambao ni katika misikiti mikubwa na maarufu zaidi nchini Tanzania na Afrika mashariki.

Pamoja na Uimamu wake, Sheikh Zubeir aliwavutia watu wengi sana kutokana na darasa zake alizokuwa akiziendesha (akizisomesha), kwa ufundi mkubwa katika msikiti huo wa Mtoro na maeneo mengine.

Sheikh Zubeir alikuwa ni katika masheikh waliojiweka karibu sana na jamii na kuwa na mahusiano mazuri na masheikh wenzake kutoka taasisi mbalimbali.

Sheikh Zubeir alipata elimu yake ya juu katika chuo kikuu cha Madina, (Ummul- Quraa) akiwa pamoja na Sheikh Juma Omar Poli, Sheikh Muharram Juma Doga, Sheikh Abdallah Ahmad Bawazir na wengineo.

Taarifa kuhusu maandalizi na taratibu zote za mazishi ni kwamba; kisomo cha kumuombea kitaanza saa 4: 00 leo asubuhi katika msikiti wa Mtoro na ataswaliwa hapo hapo Masjid Mtoro baada swala ya alasiri kisha kwenda kuzikwa katika makaburi ya Kisutu maeneo ya Upanga jijini Dar es salaam.

•••Mungu amlaze Sheikh Zubeir mahala pema wanapolazwa wema..amein

••••Inna lillah wainna illayh rajiun
IMG_20190305_072319_734.jpeg
FB_IMG_1551732571809.jpeg
 
Innah lilah wainnah ilayh rajiun

Allahumma ghfirlahu warham waafiih waaf'anhu wakrim nuzulahu wawasiih mudghalahu wawasih bilmaai wal'dharb walbard wanaksii minadhunubi walghatwaya kamaa yunakathawb abiyadh mina'danass.

Allahumma ghfirlahu warhamhu waskinu filjannah

Aamiiin,allahumma aamiin

Sent using Jamii Forums mobile app
Sheikh Thomass hebu tutafsirie maana umetuacha njia panda.
Bwana ametoa, bwana ametwaa, jina lake lihimidiwe.

Maendeleo hayana chama
 
Imamu mkuu wa msikiti maarufu nchini Tanzania na Afrika mashariki Masjid Mtoro uliopo jijini Dar es salaam eneo la Kariakoo, Sheikh Zubeir bin Yahya Mussa, amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Machi 5, 2019.

Sheikh Zubeir ni miongoni mwa masheikh maarufu jijini Dar es salaam alifahamika sana kutokana kuwa ni Imamu katika msikiti huo, ambao ni katika misikiti mikubwa na maarufu zaidi nchini Tanzania na Afrika mashariki.

Pamoja na Uimamu wake, Sheikh Zubeir aliwavutia watu wengi sana kutokana na darasa zake alizokuwa akiziendesha (akizisomesha), kwa ufundi mkubwa katika msikiti huo wa Mtoro na maeneo mengine.

Sheikh Zubeir alikuwa ni katika masheikh waliojiweka karibu sana na jamii na kuwa na mahusiano mazuri na masheikh wenzake kutoka taasisi mbalimbali.

Sheikh Zubeir alipata elimu yake ya juu katika chuo kikuu cha Madina, (Ummul- Quraa) akiwa pamoja na Sheikh Juma Omar Poli, Sheikh Muharram Juma Doga, Sheikh Abdallah Ahmad Bawazir na wengineo.

Taarifa kuhusu maandalizi na taratibu zote za mazishi ni kwamba; kisomo cha kumuombea kitaanza saa 4: 00 leo asubuhi katika msikiti wa Mtoro na ataswaliwa hapo hapo Masjid Mtoro baada swala ya alasiri kisha kwenda kuzikwa katika makaburi ya Kisutu maeneo ya Upanga jijini Dar es salaam.

•••Mungu amlaze Sheikh Zubeir mahala pema wanapolazwa wema..amein

••••Inna lillah wainna illayh rajiunView attachment 1038223View attachment 1038224
Watanzania ni mabingwa wa kusifia marehemu

Sent by Diaspora
 
Back
Top Bottom