Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,262
Aliyewahi kuwa rais wa chama soka Zanzibar (ZFA) Ali Fereji Tamim amefariki dunia visiwani Zanzibar na maziko yanatarajiwa kufanyika leo alasiri visiwani humo.
Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania TFF Wallace Karia ametuma salamu za rambirambi kwa famili, ndugu, jamaa, marafiki na ZFA kufuatia msiba huo.
Katika salamu hizo za rambirambi Rais Karia amemuelezea marehemu Tamim kuwa kama mmoja wa wanamichezo waliotoa mchango mkubwa katika mpira wa miguu hususani visiwani Zanzibar.
Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania TFF Wallace Karia ametuma salamu za rambirambi kwa famili, ndugu, jamaa, marafiki na ZFA kufuatia msiba huo.
Katika salamu hizo za rambirambi Rais Karia amemuelezea marehemu Tamim kuwa kama mmoja wa wanamichezo waliotoa mchango mkubwa katika mpira wa miguu hususani visiwani Zanzibar.